JKT RUVU WAIPIGISHA KWATA COASTAL UNION,WAICHAPA KIMOJA TU

April 12, 2014


NA SAFARI CHUWA,TANGA.
Bao la Gido Chawala lililofungwa dakika ya 17 lilitosha kuwapa ushindi Jkt Ruvu kwenye mechi yao ya Ligi kuu ya Vodacom Tanzania dhidi ya Coastal Union ya Tanga mchezo uliochezwa kwenye dimba la CCM Mkwakwani hii leo.



Bao hilo lilitokana na penati iliyotolewa na mwamuzi wa mchezo huo Adrew Sahmba kutoka mkoani Pwani kuamuru ipigwe kutokana na mshambuliaji wa Coastal Union,Selemani Kassim Selembe kuunawa mpira eneo la hatari.





Hata hivyo baada ya kuingia bao hilo,Coastal Union walijitahidi kupambana kufa na kupona ili kutaka kulirudisha bao hilo bila mafanikio ya aina yoyote yale ambapo pia Mchezo huo ambao ulikuwa wa kawaida kwa timu zote kucheza na kushambuliana kwa zamu.



Kipindi cha pili kilianza kwa kasi kwa timu zote kufanya mabadiliko ambapo Coastal Union iliwatoa Sulemain Kassim Selembe,Mohamed Ally na Hamadi Juma na kuwaingiza Mohamed Soud,Yayo Lutimba na Rayzin Haji ambao kuingia kwao kuliweza kuongeza nguvu licha ya kutokuweza kubadili matokeo.



Mpaka dakika 90 zinamalizika matokeo yaliweza kusomeka kuwa Coastal Union 0,JKT Ruvu 1.




Jkt Ruvu leo iliwakilishwa na Shabani Dihile,Damas Makwaya, Edward Charles,Chacha marwa,kasimba luambano,Thomas ndimbo, haruna adolf,paul ndauka,samweli kamutu na gido chawala,.



Coastal union iliwakilishwa na Fikirini bakari,hamadi juma,abdi banda,yusuph chuma,mbwana bakari,razack khalfani,Mohamed ally,ally iddi,Mohamed mtindi,Mohamed rajabu na suleiman kassim selembe.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »