RAIS JONATHAN AAPA KULA SAHANI MOJA NA WAPIGANAJI WA KUNDI LA BOKO HARAMU

April 15, 2014
NA MWANDISHI WETU,ABUJA.
Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan ameapa kuwa nchi yake itapambana na mauaji na ukatili unaofanywa na wapiganaji wa kundi lenye itikadi kali za Kiislamu la Boko Haram. 


Kauli hiyo ameitoa wakati alipotembelea kituo cha mabasi cha Nyanya ambacho kimeshambuliwa na kusababisha mauaji ya watu wapatao 71 na wengine kadhaa kujeruhiwa. 


Rais Jonathan amesema wamepoteza maisha ya watu kadhaa na kwamba suala la Boko Haram linaleta sura mbaya katika historia ya kipindi cha maendeleo. 


Amesema suala la Boko Haram ni la muda tu na kwamba watalitatua. Msemaji wa Jeshi la Polisi la Nigeria, Frank Mba, amesema shambulio la leo limeteketeza mabasi makubwa 16 ya abiria na mabasi madogo 24 ya abiria. 

Mwaka 2011, Boko Haram walishambulia majengo ya ofisi za Umoja wa Mataifa mjini Abuja na kusababisha mauaji ya watu 21 na kuwajeruhi wengine 60.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »