Na Masanja Mabula -Pemba
Timu
ya soka ya Mwenge imeanza kuonyesha nia ya kutaka kurithi nafasi ya
Timu ya Jamhuri kucheza ligi kuu ya Zanzibar kwa msimu ujao baada ya
kuifundisha soka timu ya Maendeleo Manta (Wazee wa Kununua ) mabao 2-1
katika mfululizo wa michezo la ligi daraja la kwanza Taifa Pemba
uliofanyika kwenye uwanja wa Polisi Finya .
Mwenge
ambayo kwa sasa inashika nafasi ya Pili kwenye msimamo wa ligi hiyo kwa
kufikisha alama 16 ikiwa nyuma ya wanajeshi wa H/Rock wenye alama 19
iliutawala mchezo kwa dakika zote .
Katika
Mpambano huo uliochezeshwa vyema na mwamuzi Asaa Ali ilishughudia
mchezaji Idd Ramadhaman akiinyima bao la kuongoza timu yake ya mwenge
manao dakika ya 25 baada ya kushindwa kuunganisha vyema mpira uliopigwa
na Mchezaji Ali Salim .
Wakiutumia
msemo wa kwamba "Penye fungu ndipo paongezwapo " Mwenge walifanikiwa
kuandika bao la kwanza katika dakika ya 42 ya kipindi cha kwanza kupitia
mchezaji Idd Ramadhaman baada ya kuwazidi ujanja walinzi wa Maendeleo
Manta .
Mwenge
walifanikiwa kuongeza bao la pili katika dakika ya 53 kwa bao la kichwa
lililofungwa na mchezaji Ali Salim Kareka ambaye alifunga bao hilo
baada ya kuunganisha vyema kona iliyochongwa na Madenge kutoka winga wa
kushoto .
Nalo
bao la kufutia machozi la timu ya Manedeleo Manta lilipatikana katika
dakika 66 likifungwa na Mchezaji Massoud Ali kwa shuti kali la Mguu wa
Kushoto kufuatia uzembe uliofanywa na walinzi wa Timu ya Mwenge .