AMUUA MKEWE NAYE KUJIUA.

October 17, 2013
Na Oscar Assenga,Handeni.
MKAZI wa Kijiji cha Kwedichocho wilayani Handeni mkoani Tanga Aweso Athumani (38) amemuua mkewe Saumu Athumani (24) kwa risasi naye kujiua kwa kujipiga risasi kisongoni kwa kutumia bunduki aina ya Gobole tukio ambalo limeacha simanzi kwa wakazi wa eneo hilo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Constatine Massawe alisema tukio hilo limetokea octoba 16 mwaka huu majira ya saa kumi na moja asubuhi wakati wakiwa nyumbani kwao ndipo alipofanya tukio hilo na kukimbilia msituni.
Massawe alisema baada ya kukimbia msituni na ndipo alipofanya tukio hilo la kujiua mwenyewe kwa kujipiga risasi shingoni na baadae wananchi walipokwenda eneo hilo waliuona mwili wake na kutoa taarifa kuhusu tukio hilo.
Kamanda Massawe alisema baada ya polisi kufika eneo la tukio wakauchukua mwili huo na kuufanyia uchunguzi wakagundua wamepigwa risasi na kuwakabidhi ndugu zao kwa ajili ya taratibu za mazishi.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »