MABAO mawili ya dakika ya 80 na 83 yaliyofungwa na Bakari Kondo wa JKT Ruvu yalitosha kuwahakikishia ushindi kwenye mechi yao na Mgambo JKT iliyochezwa leo kwenye uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.
Uzembe wa Mabeki wa Mgambo Jkt ndio kitu pekee ambacho kiliwapelekea kupoteza mchezo wa leo wa ligi kuu soka Tanzania bara licha ya wachezaji wake kucheza kwa kujituma na kuonyesha kandanda nzuri na la kusisimua.
Dakika ya 5 ya mchezo huo,JKT ruvu watajilaumu wenyewe kwa kukosa bao la wazi baada ya kupata penati iliyotokana na mchezaji wa Mgambo Shooting Salum Kipanga kuunawa mpira eneo la hatari na mwamuzi wa mchezo huo Dominick Nyamisana kutoka Dodoma kuamuru ipigwe penati.
Penati hiyo ilipigwa na Stanley Nkomola ambaye alishindwa kuitendea haki baada ya kupiga mpira huo nje ya lango la Mgambo shooting.
Mchezo huo uliokuwa mkali na wenye upinzani mkubwa ambapo mpaka timu zote zinakwenda mapumziko hakuna timu iliyoweza kuona lango la mwenzie ambapo kipindi cha pili kilianza kwa kasi.
Ambapo katika kipindi hicho Mgambo shooting waliweza kufanya mabadiliko kadhaa kwenye kikosi chake kwa kuwatoa Mohamed Samatta na kuingia Fully Maganga aliyeongeza nguvu ya mashambulizi langoni mwa JKT ruvu bila mafanikio yoyote yale.
Wakionekana kujipanga na kucheza kwa umakini JKT ruvu waliweza kuutawala mchezo huo kwa kiwango cha hali ya juu kwa wachezaji wake kucheza pasi fupi fupi na ndefu ambapo walifanikiwa kuandika mabao yao mfululizo ambapo la kwanza lilifungwa dakika ya 80 na lengine likifungwa dakika 83.
EmoticonEmoticon