NA HAFIDHI KIDOH,ARUSHA.
TIMU ya Coastal Union "Wagosi wa Kaya"leo wameanza vema Ligi kuu soka Tanzania bara baada ya kuibamiza JKT Oljoro mabao 2-0,katika mchezo uliochezwa uwanja wa sheirh Amri Abeid Mkoani Arusha.
Katika mchezo ambao ulikuwa mkali na wenye upinzani mkuwa ambapo mpaka timu zote zinakwenda mapumziko Coastal Union walikuwa wakiongoza kwa bao ambalo lilifungwa na Abdi Banda kwenye dakika ya 11.
Baada ya bao hilo,Coastal Union waliweza kuongeza nguvu ya mashambulizi langoni mwa JKT Oljoro na kufanikiwa kuandika bao lao la pili katika dakika ya 36 bao ambalo lilifungwa na mchezaji hatari na mahiri wa kikosi hicho Crispian Odulla.
Licha ya JKT Oljoro kutaka kufurukuta langoni mwa Coastal Union walishindwa kubadilisha matokeo mpaka dakika 90 na kusomeka Coastal Union 2 na JKT Oljoro 0.
EmoticonEmoticon