Showing posts with label siasa. Show all posts
Showing posts with label siasa. Show all posts

DEVOTA MBURARUGABA NA SAMIRA AMOUR WAIBUKA KIDEDEA UCHAGUZI UBUNGE VITI MAALUM KURA ZA MAONI

August 01, 2025 Add Comment

 




Wa kwanza kulia ni Devotha Daniel aliyepata kura 1,308 katika kura za maoni nafasi ya ubunge viti maalumu , kushoto ni Samira Khalfan aliyepata kura 1,250.



Devotha Daniel Mshindi wa kwanza Uchaguzi wa UWT mkoa wa Kagera 
Devotha Daniel akipewa pongezi 



Na Mariam Kagenda , Kagera


Devotha Daniel Mburarugaba na Samira Khalfan Amour wameibuka washindi kati ya wagombea nane walioshiriki katika uchaguzi wa kura za maoni nafasi ya ubunge wa viti maalumu mkoa wa Kagera kupitia Umoja wa wanawake Tanzania (UWT).

Akitangaza matokeo hayo, Msimamizi wa uchaguzi huo ambaye ni mjumbe wa baraza ku
u UWT Taifa Yasmin Bachu amesema uchaguzi huo ulikuwa na wagombea nane, jumla ya wapiga kura walikuwa 1,483 ambapo kura moja ilihalibika hivyo kura halisi zilikuwa 1,482.

"Aliyeongoza kwa kura nyingi ni Devotha Daniel aliyepata kura 1,308 na wa pili Samira Khalfan aliyepata kura 1,250 wengine ni pamoja na Anitha Korongo kura 153, Elizabeth Ngaiza kura 94, Anitha Bunono kura 52, Anitha Nyamzinga kura 44, Herieth Lugaju kura 37 na Evastina Godian kura 26" amesema Bachu


Bachu amewashauri wajumbe wa UWT mkoa wa Kagera kuwa, wakati wa kampeini za Dk.Samia Suluhu Hassan wapaze sauti na kuunganisha nguvu za kumuombea kura zitoshe pia kushinda majimbo yote ya mkoa wa Kagera ili kuwawezesha washindi hao wawili kuingia bungeni.


Wagombea wamesema uchaguzi uliandaliwa kwa mazingira safi na Usalama wa hali ya juu na kuwaomba wenzao ambao kura hazikutosha kuendelea kuungana na waliochaguliwa kufanya kazi pamoja kwani wote ni wana chama wa chama cha Mapinduzi (CCM)


Devotha Daniel amewaomba wajumbe kuungana na kuondoa makundi kwani uchaguzi huo umepita wawe kitu kimoja wote walikuwa wazuri sasa wanajenga nyumba moja, hivyo itasaidia waweze kutafuta kura za Dk.Samia na majimbo yote nane kwa urahisi kwani ndilo jambo kubwa lililopo mbele yao kwasasa.

Mshindi mwingine Samira Khalfan ameshukuru kamati ya CCM Taifa kurudisha jina lake na kumuona anafaa katika nafasi hiyo, pia akawaasa wagombea wenzake ambao hawakufanikiwa kupata ushindi wasikate tamaa maana kwenye chama hicho zipo nafasi nyingi hivyo zinapotokea wasiache kugombea maana wote wanahitaji kutafuta kura usiku na mchana ili CCM ishinde.


Naye mwenyekiti wa UWT mkoa wa Kagera Hajat Faidhah Kainamula amesema katika zoezi la kupata mgombea lipo suala la kupata na kukosa kuchaguliwa jambo la muhimu kwa sasa ni wajumbe kushikamana ili kuleta maendeleo mazuri ndani ya chama na siyo malumbano.

"Tuondoe chuki, baada ya uchaguzi kinachotakiwa katika chama ni mshikamano wenye kutenda,utekelezaji na kupata mafanikio mazuri yatakayoleta maendeleo" amesema Kainamula


Katibu wa UWT mkoa wa Kagera Rehema Zuberi amesema awali watia nia wa nafasi ya viti Maalumu walijitokeza wakiwa 13 mmoja kati ya hao hakurudilisha fomu.

KAMATI KUU CCM YAPEWA KONGOLE MCHAKATO UTEUZI WA WAGOMBEA

July 31, 2025 Add Comment

 


 Mfanyabiashara, Haidary Gulamali  akiwa katika moja ya mikutano yake ya chama.

................................

Na Dotto Mwaibale

KAMATI Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa chini ya Mwenyekiti wake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imepongezwa kwa kumaliza mchakato wa uteuzi wa wagombea nafasi ya ubunge, udiwani na Ujumbe wa baraza la uwakilishi.

Jana Julai 28, 2025 kamati hiyo ilimaliza mchakato wa awali wa uteuzi wa nafasi ya kugombea Ubunge, Udiwani na baraza la uwakilishi katika Uchaguzi unaotarajiwa kufanyika oktoba mwaka huu.

Mchakato huo umepongezwa na wana CCM na wagombea wenyewe kufuatia hatua iliyochukuliwa na chama hicho ya kuifanyia marekebisho madogo katiba yake kwa kuomba ridhaa kwa wajumbe ya kuongeza idadi ya wagombea kutoka watatu hadi zaidi kulingana na kamati hiyo ilivyoona inafaa.

 Tayari mchakato wa uteuzi wa wagombea katika majimbo yote umekwisha kamilika na kutangazwa na Katibu wa NEC, Itikadi na Mafunzo wa chama hicho Taifa, Amos Makalla.

Kinachofuata sasa ni kwa majina hayo kwenda kwa wajumbe kupigia kura na baadae kurudishwa mbele ya kamati hiyo kwa ajili ya kumpata mgombea mmoja katika jimbo husika.

Katika Jimbo la Ilongero mkoani  Singida wagombea saba wamechaguliwa ili wakapigiwe kura na wajumbe wa jimbo hilo.

Wagombe hao ni Ramadhani Abeid Ighondo mbunge aliyemaliza muda wake ambaye anatetea nafasi hiyo kwa kipindi cha pili, Lazaro Nyalandu ambaye alishawahi kuwa mbunge wa jimbo hilo kupitia CCM ambapo, Aprili 30, 2021 alirejea tena CCM katika mkutano mkuu maalum wa chama hicho tawala  uliofanyika Jijini Dodoma.

 

Nyalandu alijitoa CCM Oktoba 30, 2017 akiwa Mbunge wa hilo zamani likiitwa Singida Kaskazini na baadaye kujiunga na Chadema ambako alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa chama hicho Kanda ya Kati. 

   Baada ya kuona kazi nzuri iliyofanywa na Serikali chini ya Rais Samia ndipo alipoamua kurejea CCM na mwaka huu wa uchaguzi ameamua kugombea tena nafasi hiyo kwa mara tatu.

Mgombea mwingine ni Mfanyabiashara, Haidary Gulamali ambaye amewahi kugombea nafasi hiyo kwa vipindi viwili lakini  ameingia kipindi cha tatu kujaribu bahati yake kwa mara nyingine kutokana na kuwiwa zaidi kuwatumikia wananchi wa jimbo hilo.

Wengine waliochaguliwa na kamati hiyo kwa ajili ya kupigiwa kura na wajumbe ni pamoja na Mungwe Mgoo, Abdallah Haji, Maulid Sombi na Yustina Inyasi.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipokuwa akimkabidhi   nakala ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020-2025 mgombea ubunge wa CCM wa jimbo la Singida Kaskazini (ILONGERO), Ramadhan Ighondo, katika mkutano wa kampeni, uliyofanyika kwenye viwanja vya Ilongero, Septemba 15, 2020. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
Lazaro Nyalandu akihutubia katika moja ya mikutano yake
 

WATENDAJI UCHAGUZI WATAKIWA KUTOA TAARIFA KWA VYAMA VYA SIASA

July 21, 2025 Add Comment

 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jacobs Mwambegele akizungumza wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kwa watendaji wa uchaguzi mkuu kutoka mikoa ya Shinyanga na Simiyu leo Julai 21, 2025. Mafunzo hayo yamefanyika mkoani Shinyanga.  
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jacobs Mwambegele akizungumza wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kwa watendaji wa uchaguzi mkuu kutoka mikoa ya Shinyanga na Simiyu leo Julai 21, 2025. Mafunzo hayo yamefanyika mkoani Shinyanga.


Washiriki wa mafunzo hayo ambayo yanawajumuisha waratibu wa uchaguzi, wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya jimbo kutoka majimbo yote ya Mikoa ya Shinyanga na Simiyu. 
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume, Ndg. Cyprian Mbugano akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo ambapo pia alitoa mada. 
Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani (Mstaafu) Mbarouk Salim Mbarouk akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo kama hayo kwa Kisiwani Pemba, Zanzibar ambapo amewaasa watendaji hao kufanya kazi kwa kuzingatia Katiba, Sheria, Kanuni, miongozo na maelekezo mbalimbali yaliyotolewa na yatakayotolewa na Tume.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Uchaguzi, Ndg Adam Mkina ambaye ni Mkurugenzi wa INEC ofisi ya Zanzibar akizungumza jambo. 
Washiriki wa mafunzo hayo ambayo yanawajumuisha waratibu wa uchaguzi, wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya jimbo kutoka majimbo yote ya Kisiwani Pemba, Zanzibar.

*****************
Na. Mwandishi wetu, Shinyanga
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imewataka watendaji wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kutoa taarifa mapema kwa vyama vya siasa kuhusu utaratibu wa kuwaapisha mawakala.
 
Hayo yamesemwa mkoani Shinyanga leo Julai 21, 2025 na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jacobs Mwambegele wakati akifungua mafunzo kwa watendaji wa uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi oktoba mwaka huu kwa tarehe itakayotangazwa na Tume.
 
“Wakati wa kuapisha mawakala, toeni taarifa mapema kwa vyama vya siasa kwa mujibu wa sheria, kanuni na maelekezo ya Tume na kuvipatia vyama vya siasa orodha ya vituo vya kupigia kura ili kuviwezesha kupanga mawakala,” amesema Jaji Mwambegele.
 
Amewasisitiza watendaji hao kuhakikisha vifaa vya uchaguzi wanavyopokea kutoka Tume, wanavihakiki, kuvikagua na kuhakikisha vinasambazwa kwenye vituo vyote na kila mkuu wa kituo anapata vifaa vyote vya uchaguzi vinavyohitajika mapema.
 
Amewataka kuhakikisha kuwa siku ya uchaguzi wanaweka utaratibu utakaowezesha kila kituo cha kupigia kura kufunguliwa saa 1:00 kamili asubuhi na kufanya mawasiliano na Tume pale ambapo ushauri utahitajika kuhusiana na masuala ya uchaguzi.
 
Akifungua mafunzo kama hayo Kisiwani Pemba, Zanzibar, Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani (Mstaafu) Mbarouk Salim Mbarouk amewaasa watendaji hao kufanya kazi kwa kuzingatia Katiba, Sheria, Kanuni, miongozo na maelekezo mbalimbali yaliyotolewa na yatakayotolewa na Tume.
 
 “Jitahidini na mjiepushe kuwa vyanzo vya malalamiko kutoka kwa vyama vya siasa na wadau wa uchaguzi. Hakikisheni mnazingatia ipasavyo Katiba, Sheria, Kanuni, miongozo na maelekezo mbalimbali yaliyotolewa na yatakayotolewa na Tume,” amesema Jaji Mwambegele.
 
Amewataka kuwashirikisha wadau wa uchaguzi kwenye maeneo wanayopaswa kushirikishwa kwa mujibu wa Katiba, Sheria, Kanuni, miongozo na maelekezo ya Tume.
 
Amewakumbusha kuhusu wajibu wao wa kuhakikisha wanavitambua vituo vya kupigia kura mapema ili kubaini mahitaji maalum ya vituo husika na kuhakikisha kunakuwa na mpangilio mzuri ambao utaruhusu uchaguzi kufanyika kwa utulivu na amani.
 
“Ajira za watendaji wa vituo zizingatie kuajiri watendaji wenye weledi, wanaojitambua, wazalendo, waadilifu na wachapakazi na kuachana na upendeleo kwa ndugu na jamaa ambao hawana sifa za kufanya shughuli za uchaguzi,” amesema Jaji Mbarouk.
 
Mafunzo hayo yanafanyika kwa siku tatu kwenye mikoa mbalimbali nchini kwa siku tatu na yanawajumuisha waratibu wa uchaguzi, wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya jimbo.

Tume imeyagawa mafunzo hayo kwenye awamu mbili ambapo awamu hii ya pili inahusisha mikoa ya Simiyu, Shinyanga, Kusini Pemba, Kaskazini Pemba, Mwanza, Mara, Dar es Salaam, Pwani, Rukwa, Katavi, Manyara, Arusha, Songwe na Mbeya.
 
Awamu ya kwanza ilifanyika tarehe 15 hadi 17 na ilihusisha watendaji kutoka mikoa ya Morogoro, Singida, Dodoma, Kaskazini Unguja, Kusini Unguja, Mjini Magharibi, Geita, Kagera, Mtwara, Lindi, Tabora, Kigoma, Tanga, Kilimanjaro, Ruvuma, Iringa na Njombe.
Hakimu mkazi Mfawidhi wa Wilaya ya Shinyanga, Mhe. Goodselda Kalumuna akitoa maelezo kabla ya kuwaapisha washiriki hao wa mafunzo kwa watendaji wa Uchagzi Mkuu ambapo aliwaongoza kula kiapo cha kujitoa uanachama na kutunza siri wakati wote wa utekelezaji wa majukumu yao ya Uchaguzi. 


Washiriki wamafunzo kutoka Shinyanga na Simiyu wakila kiapo cha kujitoa uanachama wa vyama vya siasa na kutunza siri. 

Washiriki wamafunzo kutoka Kisiwa cha Pemba, Zanzibar wakila kiapo cha kujitoa uanachama wa vyama vya siasa na kutunza siri. 

MCC PINDA ATAKA HAKI UTEUZI WA WAGOMBEA UBUNGE ,UDIWANI

July 12, 2025 Add Comment

  



    

Na Paskal Mbunga,TANGA

WAZIRI Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Mizengo Pinda amewahimiza viongozi waliopewa dhamana ya mamlaka ya kusimamia mchakato wa uteuzi wa wagombea kuhakikisha wanatenda haki kwa wale wote waliojitokeza kwenye kinyang’anyiro hicho .

Pinda aliyasema hayo  mara baada ya kutembelea ukarabati wa ofisi ya Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga ambao umefikia asilimia 99 ya kazi iliyofanywa ikiwa ni ndoto za Mwenyekiti wa CCM Mkoa huo Rajab Abduhaman kuona jengo hilo linakuwa na muonekana mzuri kwa ajili ya kuwahudumia wana CCM.

Akiwa katika eneo hilo mara baada ya kutembelea ukarabati wa jengo hilo aliupongeza uongozi wa CCM kutokana na kazi nzuri walioifanya ya kukarabati jengo hilo na hivyo kuwa na muonekana mpya.

Alisema wakati nchi ikielekea kwenye mchakato wa uchaguzi mkuu Octoba mwaka huu tayari maandalizi yameshaanza na waliochukua fomu Udiwani na Ubunge wameshafanya na kazi ya chama ni kuhimiza viongozi waliopewa dhamana ya mamlaka ya kusimamia mchakato watende haki.

“ Bahati nzuri kamati yenu mlisimamie kikamilifu ili mtu asipate sababu ya kupiga kelele wakati hakuna sababu ya kufanya hivyo kwa wananchi tunaomba wakati wa kupiga kura tumieni haki yenu tena kwa uhuru wenu wenyewe”Alisema

Aidha alisema pia kupitia utaratibu uliowekwa kabla ya kutoka kwenda kupambana na vyama vyengine lazima wampate mgombea wa chama atakayekwenda kupambana na vyama vyengine vya siasa tumieni haki yenu vizuri mtupe mgombea ambaye mnaamini anaweza kutuvusha kwa haraka zaidi.

Hata hivyo Waziri Mkuu Mstaafu Pinda alisema kwamba wanaendelea kumshukuru Rais Dkt Samia Suluhu na kumpongeza kwa kazi nzuri anayoifanya nchi ipo kwenye utulivu na amani na mambo yanasonga mbele.

“Tanga kuna maneno nimesikia Rais hana deni na sisi na octoba tunatiki niombeni wana Tanga na wana CCM hilo jambo lipo mbele yenu na Tanga mlikuwa wapambanaji sana lazima jitihada kuhakikisha mnaongoza kwenye kura za Rais na Ubunge kwenye chaguzi zijazo”Alisema

Pinda aliwataka viongozi wa mkoa huo kuendelea kuchapa kazi pamoja na mshikamano kwa kuhakikisha wanaendelea kudumisha amani na ulitulivu ambao wanao mpaka sasa kutokana na kwamba haukudondoka tu angani bali umejengwa hivyo waendelee kumuomba mwenyezi Mungu aendelee kuisimamia.

Awali akizungumza Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajabu Abdurhaman amesema ukarabati wa ofisi hiyo ni maelekezo ya Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho Dkt Samia Suluhu kuhakikisha mali za chama yakiwemo majengo ya chama ya ofisi na menginevyo wanayalinda na kuyafanyia ukarabati mkubwa ili yaendelee kutumika miaka mingi kadri inavyowezekana.

Aidha alisema kwamba alifanya ziara kwenye mkoa wa Tanga na katikati pita pita yake aliona jengo lao namna lilivyokuwa na kutoa maelekezo kuhakikisha jengo hilo linafanyiwa ukarabati mkubwa na hayo ni matunda ya Mwenyekiti wa Taifa na maelekeo yake.

“Tulipopata maelekezo hayo tukasema lazima tufanye kwa sababu haki na heshima ya CCM kwenye nchi na mkoa wa Tanga ni kubwa haiwezekani viongozi wa CCM wanaovyoonekana uzuri lakini mahali wanapofanyia kazi hapafanani na nasi tukasema hapana lazima watii maelekezo hayo na tunashukuru wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa na Kamisaa wao kwa umoja na mshikamano wao ndio umewezesha kutekeleza maelekezo hayo ya Rais”Alisema

Naye kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi ,Dkt Batilda Burian amesema wao wamefarijika uwepo wa Waziri Mkuu huyo na wanamshukru Mwenyekiti Taifa kwa kazi kubwa aliyoifanya wakati wa ziara yake na wana Tanga wanaendelea kumshukuru kwa mambo mengi makubwa ya kimaendeleo aliyofanya kwa mkoa huo.

“Kutokanana na hilo tunasema kwamba Mama Hana deni na Octoba tunatiki na kura zitajaa na kumwagika kutokana na kasi kubwa ya maendeleo aliyoyafanya katika mkoa wa Tanga na hivyo kuufungua kiuchumi”Alisema

Hata hivyo,Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga Mfaume Kizigo alisema chama hicho kimepata kiongozi wa uhakika na kinachoonekana hapo ni sehemu ya maendeleo makubwa yaliyofanywa na Mwenyekiti huyo kutokana na kila wilaya amejenga nyumba za watumishi kuanzia chama na Jumuiya zake zote na amefanya hivyo kila alipokwenda kuishauri kamati ya siasa.



Mwisho.

PINDA ATAKA HAKI MCHAKATO WA WAGOMBEA

July 11, 2025 Add Comment





Na Oscar Assenga,TANGA

WAZIRI Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Mizengo Pinda amehimiza viongozi waliopewa dhamana ya mamlaka ya kusimamia mchakato wa uteuzi wa wagombea kuhakikisha wanatenda haki kwa wale wote waliojitokeza kwenye kinyang’anyiro hicho .

Pinda aliyasema hayo leo mara baada ya kutembelea ukarabati wa ofisi ya Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga ambao umefikia asilimia 99 uliofanywa ikiwa ni ndoto za Mwenyekiti wa CCM Mkoa huo Rajab Abduhaman kuona jengo hilo linakuwa na muonekana mzuri kwa ajili ya kuwahudumia wana CCM.

Akiwa katika eneo hilo mara baada ya kutembelea ukarabati wa jingo hilo aliupongeza uongozi wa CCM kutokana na kazi nzuri walioifanya ya kukarabati jengo hilo na hivyo kuwa na muonekana mpya.

Alisema wakati nchi ikielekea kwenye mchakato wa uchaguzi mkuu Octoba mwaka huu tayari maandalizi yameshaanza na waliochukua fomu Udiwani na Ubunge wameshafanya na kazi ya chama ni kuhimiza viongozi waliopewa dhamana ya mamlaka ya kusimamia mchakato watende haki.

“ Bahati nzuri kamati yenu mlisimamie kikamilifu ili mtu asipate sababu ya kupiga kelele wakati hakuna sababu ya kufanya hivyo kwa wananchi tunaomba wakati wa kupiga kura tumieni haki yenu tena kwa uhuru wenu wenyewe”Alisema

Aidha alisema pia kupitia utaratibu uliowekwa kabla ya kutoka kwenda kupambana na vyama vyengine lazima wampate mgombea wa chama atakayekwenda kupambana na vyama vyengine vya siasa tumieni haki yenu vizuri mtupe mgombea ambaye mnaamini anaweza kutuvusha kwa haraka zaidi.

Hata hivyo Waziri Mkuu Mstaafu Pinda alisema kwamba wanaendelea kumshukuru Rais Dkt Samia Suluhu na kumpongeza kwa kazi nzuri anayoifanya nchi ipo kwenye utulivu na amani na mambo yanasonga mbele.

“Tanga kuna maneno nimesikia Rais hana deni na sisi na octoba tunatiki niombeni wana Tanga na wana CCM hilo jambo lipo mbele yenu na Tanga mlikuwa wapambanaji sana lazima jitihada kuhakikisha mnaongoza kwenye kura za Rais na Ubunge kwenye chaguzi zijazo”Alisema

Pinda aliwataka viongozi wa mkoa huo kuendelea kuchapa kazi pamoja na mshikamano kwa kuhakikisha wanaendelea kudumisha amani na ulitulivu ambao wanao mpaka sasa kutokana na kwamba haukudondoka tu angani bali umejengwa hivyo waendelee kumuomba mwenyezi Mungu aendelee kuisimamia.

Awali akizungumza Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajabu Abdurhaman amesema ukarabati wa ofisi hiyo ni maelekezo ya Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho Dkt Samia Suluhu kuhakikisha mali za chama yakiwemo majengo ya chama ya ofisi na menginevyo wanayalinda na kuyafanyia ukarabati mkubwa ili yaendelee kutumika miaka mingi kadri inavyowezekana.

Aidha alisema kwamba alifanya ziara kwenye mkoa wa Tanga na katikati pita pita yake aliona jengo lao namna lilivyokuwa na kutoa maelekezo kuhakikisha jengo hilo linafanyiwa ukarabati mkubwa na hayo ni matunda ya Mwenyekiti wa Taifa na maelekeo yake.

“Tulipopata maelekezo hayo tukasema lazima tufanye kwa sababu haki na heshima ya CCM kwenye nchi na mkoa wa Tanga ni kubwa haiwezekani viongozi wa CCM wanaovyoonekana uzuri lakini mahali wanapofanyia kazi hapafanani na nasi tukasema hapana lazima watii maelekezo hayo na tunashukuru wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa na Kamisaa wao kwa umoja na mshikamano wao ndio umewezesha kutekeleza maelekezo hayo ya Rais”Alisema

Naye kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi ,Dkt Batilda Burian amesema wa wamefarijika uwepo wa Waziri Mkuu huyo na wanamshukru Mwenyekiti Taifa kwa kazi kubwa aliyoifanya wakati wa ziara yake na wana Tanga wanaendelea kumshukuru kwa mambo mengi makubwa ya kimaendeleo aliyofanya kwa mkoa huo.

“Kutokanana na hilo tunasema kwamba Mama Hana deni na Octoba tunatiki na kura zitajaa na kumwagika kutokana na kasi kubwa ya maendeleo aliyoyafanya katika mkoa wa Tanga na hivyo kuufungua kiuchumi”Alisema

Hata hivyo,Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga Mfaume Kizigo alisema chama hicho kimepata kiongozi wa kwelikweli na kinachoonekana hapo ni sehemu ya maendeleo makubwa yaliyofanywa na Mwenyekiti huyo kutokana na kila wilaya amejenga byumba za watumishi kuanzia chama na Jumuiya zake zote na amefanya hivyo kila alipokwenda kuishauri kamati ya siasa.



Mwisho.