Showing posts with label afya. Show all posts
Showing posts with label afya. Show all posts

BALOZI YAKUB APONGEZA MUHIMBILI KUPELEKA WATOA HUDUMA ZA KIBINGWA WENGI NCHINI COMORO

October 01, 2025 Add Comment


Balozi wa Tanzania nchini Comoro Saidi Yakub ameipongeza Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa kupeleka idadi kubwa ya madaktari bingwa bobezi katika kambi ya matibabu nchini humo  ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa agizo la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, alilolitoa wakati wa ziara yake visiwani humo.

Akizungumza hii leo katika mahojiano maalumu na Afisa Habari kutoka Idara ya Habari ya MNH,  Balozi Yakub amesema hospitali hiyo imepeleka jumla ya madaktari bingwa saba wa mgonjwa mbalimbali ukilinganisha na taasisi nyingine zinazoshiriki kambi hiyo.

" Hospitali ya Muhimbili imetuletea zaidi ya madaktari saba na katika wataalam hao watakuwa katika mgonjwa ya figo, ngozi, macho, meno,  masuala ya uzazi kwa akina mama pamoja na magonjwa ya kinamama"



Aidha, Balozi Yakub ameongeza kuwa licha ya kambi ya matibabu kuanza kuanza Oktoba 04, 2025, tayari  zaidi ya watu 1000 wamekwisha kujisajili ili kupata huduma za kibingwa na ubingwa bobezi.

UTENDAJI KAZI WA WIZARA YA NISHATI NA TAASISI ZAKE WAIMARIKA

September 27, 2025 Add Comment




📌 *Wapanda kutoka asilimia 95 hadi 96.16 katika kipindi cha robo mwaka*

📌 *Mhandisi Mramba asema ongezeko hilo linaakisi utoaji wa huduma kwa wananchi*

📌 *Apongeza Taasisi kuendelea kuboresha utoaji huduma kwa Wananchi.*

📌 *Asisitiza mitandao ya kijamii kutumika ipasavyo utoaji elimu Nishati Safi ya kupikia.*

Imeelezwa kuwa, utendaji kazi wa Wizara ya Nishati kupitia Taasisi inazosisimamia umezidi kuimarika na kufikia asilimia 96.16 katika kipindi cha robo nne ya mwaka 2024/2025.

Hayo yamefahamika wakati wa kikao cha Tano cha Tathmini ya utendaji kazi wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake kwa robo nne ya mwaka 2024/2025 kilichofanyika jijini Dodoma na kuongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Mhandisi Felchesmi Mramba.Tathmini hiyo ya utendaji kazi iliyofanywa na Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini katika Wizara ya Nishati imeonesha kuwa katika kipindi cha robo ya nne ya mwaka 2024/2025 utendaji kazi wa Taasisi zilizochini ya Wizara ya Nishati umeimarika kwa zaidi ya asilimia 96 kutoka asilimia 95 katika kipindi cha robo ya tatu ya mwaka 2024/2025.

Kufuatia tathmini hiyo, Mha. Mramba amewapongeza Watendaji wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake kwa kuendelea kuboresha utendaji kazi kupitia utekelezaji wa miradi na utoaji huduma kwa wananchi hali inayoleta matokeo chanya katika Sekta ya Nishati.“Tathmini hizi zinaakisi kile tunachokitekeleza kwani huduma zimeendelea kuboreshwa pamoja na kuimarika zaidi, sisi kama Wizara tumeendelea kuhakikisha kuwa tunatoa huduma bora kwa wananchi”.Ameeleza Mha. Mramba

Katika kikao hicho, Mha. Mramba amelipongeza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa kuendelea kutoa taarifa kwa wananchi kwa wakati jambo ambalo limeleta ongezeko la kuimarika kwa utoaji huduma.Aidha, kuhusu Nishati Safi ya Kupikia, amesisitiza kutumia mitandao ya kijamii katika kuitangaza nishati hiyo hususani matumizi ya majiko yanayotumia umeme kidogo akieleza kuwa mitandao ya kijamii inanguvu kubwa ya kufikisha habari kwa watu wengi na kwa muda mfupi lengo likiwa ni kutimiza adhma ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha kuwa wananchi wanahama kutoka matumizi ya Nishati isiyo safi ya kupikia kwenda kwenye matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Vilevile,amekipongeza Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini cha Wizara ya Nishati kwa kutekeleza jukumu lao kwa ufanisi huku akisisitiza kuwa Kitengo hicho kipewe ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yake ikiwa ni pamoja na kuhakikisha Idara, Vitengo na Taasisi zinawasilisha taarifa za utendaji kazi kwa wakati ili kitengo hicho kiongeza ufanisi zaidi katika kazi ya tathmini na hivyo kuboresha utendaji kazi.Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio amezipongeza Taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Nishati pamoja na Idara na Vitengo vya Wizara ya Nishati kwa utendaji kazi wenye kuleta matokeo chanya kama ambavyo tathmini ya utendaji kazi ilivyoonesha kuwa ufanisi wa kazi umeendelea kuboreshwa na kuimarika zaidi.

Awali, Akiwasilisha taarifa ya tathmini ya utendaji kazi kwa Wizara na Taasisi zake, Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini, Wizara ya Nishati, Bi. Anita Ishengoma alisema kuwa kutoka zoezi la tathmini lianze kufanyika, limeleta ufanisi hasa katika utekelezaji wa miradi mbalimbali pamoja na mipango ya Wizara kwani utendaji kazi wa Taasisi umeongezeka.Amesema kuwa Idara/Vitengo zilizofanya vizuri zaidi katika tathmini iliyofanyika katika Wizara ya Nishati kwa kipindi cha robo nne ya mwaka 2024/2025 ni Idara ya Umeme na Nishati Jadidifu (nafasi ya kwanza), Kitengo cha Manunuzi -(Nafasi ya Pili) na - Kitengo cha Tehama ( Nafasi ya Tatu).

Aidha, Taasisi zilizofanya vizuri zaidi katika utendaji kazi kwa tathmini iliyofanyika katika kipindi cha robo nne ya mwaka 2024/2025 ni Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) - nafasi ya kwanza), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) -nafasi ya Pili) na Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA)- nafasi ya Tatu).

Mikoa ya Kitanesco iliyofanya vizuri katika utendaji kazi kwa tathmini iliyofanyika katika kipindi cha robo nne ya mwaka 2024/2025 ni Manyara (nafasi ya kwanza), Kinondoni Kusini ( nafasi ya Pili) na Simiyu ( nafasi ya Tatu).

Ilielezwa kuwa utendaji kazi wa mikoa ya kitanesco kwa ujumla umeimarika kwani hamna mkoa ambao utendaji wake umekuwa chini ya asilimia 91.83.

Katika Kikao hicho pia Taasisi ziliweza kuwasilisha taarifa za utendaji kazi wake.

kikao hicho kilihudhuriwa na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara, Wakurugenzi wa Vitengo Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Wizara mbalimbali, Menejimenti ya Wizara ya Nishati na Taasisi zake pamoja na Mameneja wa Kanda wa TANESC
MUHAS  YAPEWA JUKUMU KUU KUANDAA WATAALAMU BINGWA WA MOYO NA MISHIPA YA DAMU

MUHAS  YAPEWA JUKUMU KUU KUANDAA WATAALAMU BINGWA WA MOYO NA MISHIPA YA DAMU

September 22, 2025 Add Comment

 

Na.Mwandishi Wetu

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, amesema kuwa utekelezaji wa Awamu ya Pili ya Mradi wa Kituo cha Umahiri cha Magonjwa ya Moyo na Mishipa ya Damu katika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) utakuwa chachu ya kukuza ujuzi wa wataalamu wa afya nchini.

Prof. Nombo alitoa kauli hiyo Septemba 2025 Jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa kikao cha kwanza cha Kamati ya Uendeshaji ya mradi huo, kilichofanyika katika Kituo cha Umahiri kilichopo Mloganzila. Alieleza kuwa mradi huo ni ushahidi wa wazi wa namna Serikali inavyowekeza katika kuimarisha elimu ya afya na kuhakikisha taifa linapata wataalamu mahiri wa kutoa huduma bora kwa wananchi.

“MUHAS ni taasisi inayotoa utaalamu wa kisayansi na kuandaa wataalamu wa afya kwa kiwango cha juu. Kituo hiki ni mahali pa kufundisha mabingwa na bobezi katika sayansi ya moyo na mishipa ya damu. Tunaona vifaa vinavyotumika ni vya kisasa, hivyo tunatarajia wananchi kunufaika kwa kiwango kikubwa kupitia huduma zitakazotolewa hapa,” alisema Prof. Nombo.

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), Prof. Appolinary Kamuhabwa, ameishukuru Serikali kwa uwekezaji mkubwa katika Kituo cha Umahiri cha Magonjwa ya Moyo na Mishipa ya Damu kilichopo Mloganzila, pamoja na ushirikiano wa kimataifa uliowezesha chuo hicho kupata ufadhili wa vifaa vya kisasa vya kufundishia na kujifunzia.

Prof. Kamuhabwa amesema kuwa mchango wa Serikali na wadau wa maendeleo kutoka mataifa mbalimbali umeimarisha uwezo wa MUHAS katika kutoa mafunzo ya kibingwa na kuendeleza tafiti za kisayansi.

Mradi huo unatarajiwa kuongeza uwezo wa kitaalamu wa MUHAS katika kutoa mafunzo ya vitendo na huduma za kibingwa, sambamba na kuimarisha miundombinu ya kisasa kwa ajili ya tafiti na mafunzo ya afya ya moyo na mishipa ya damu.

DKT. BITEKO AZINDUA TEKNOLOJIA YA KUONDOA UVIMBE MWILINI BILA UPASUAJI

August 27, 2025 Add Comment




📌 Ni kwa mara ya kwanza kufanyika Afrika Mashariki na Kati


📌 Aipa kongole Hospitali ya Kairuki kwa kutoa punguzo la asilimia 50 kwa wagonjwa 50 wa kwanza


📌 Asema Serikali itaendelea kuweka msukumo ushirikiano na Sekta binafsi


📌 Awaasa Watendaji Wizara ya Afya kutoogopa kujifunza pale Sekta binafsi inapofanya vizuri


📌 Wagonjwa 300  wanufaika na teknolojia ya utoaji uvimbe bila upasuaji


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ameziindua teknolojia ya kuondoa uvimbe mwilini bila upasuaji inayofahamika kama High-Intensity Focused Ultrasound (HIFU) katika Hospitali ya Kairuki ikiwa ni mara ya kwanza kwa huduma hiyo kuzinduliwa katika nchi za Afrika Mashariki na Kati.

Akizindua huduma hiyo Agosti 27, 2025 jijini Dar es Salaam, Dkt. Biteko amepongeza Watendaji wa hospitali ya Kairuki pamoja na muasisi wake Hubert Kairuki na Mkewe kwa uthubutu wao katika masuala mbalimbali ikiwemo utoaji wa huduma hiyo ya HIFU ambayo imeiweka Tanzania katika rekodi ya kutoa uvimbe bila kufanya upasuaji  barani Afrika suala ambalo pia litaongezea nchi mapato.

Ameeleza kuwa awali huduma ya HIFU barani Afrika likuwa ikipatikana katika nchi tatu tu ambazo ni Misri, Nigeria na Afrika Kusini.

Aidha, ameipongeza Hospitali ya Kairuki kwa kutoa punguzo la asilimia 50 la gharama za matibabu ya utoaji uvimbe bila upasuaji kwa wagonjwa 50 wa kwanza ndani ya kipindi cha mwezi mmoja kuanzia leo ikiwa ni kielelezo cha Watendaji wa hospitali hiyo kuonesha utu kwa Watanzania, kuacha alama njema na kuunga  mkono dhamira ya Serikali ya kutoa huduma kwa watanzania kwa gharama nafuu.

Dkt. Biteko amesema kuwa kufanyika kwa tukio hilo muhimu  ni kielelezo cha Serikali ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuipa msukumo sekta binafsi na kuikuza ili kutoa huduma za matibabu kwa wananchi kwa ufanisi na kusogeza karibu huduma ambazo hapo awali zilikuwa hazipatikani ndani ya nchi hivyo ameahidi kuwa Serikali itaendelea kuunga mkono Sekta binafsi.

·Aidha, ameipongeza Hospitali ya Kairuki kwa kuanzisha Idara ya huduma za dharura ambayo ina uwezo wa kuhudumia wagonjwa zaidi ya 9,000 kwa mwaka. 

Katika hatua, nyingine, Dkt. Biteko amewataka Watendaji katika Wizara ya Afya kutoogopa kujifunza kutoka Sekta binafsi pale inapofanya vizuri na wawape ushirikiano wakati wote siyo nyakati za ukaguzi tu kwani lengo la Serikali ni kufikisha huduma bora kwa wananchi kwa ushirikiano wa Serikali na sekta hiyo.


Kuhusu ombi la Hospitali ya Kairuki la kujengewa barabara ya lami ya mita 300 kuelekea kwenye hospitali hiyo ili kurahisisha utoaji huduma kwa wananchi ameelekeza Manispaa ya Kinondoni kufanyia kazi ombi hilo.

Dkt. Mwinyikondo Amir, kutoka Wizara ya Afya akimwakilisha Waziri wa Afya, amesema kuwa tukio hilo ni ishara ya ushirikiano uliopo kati ya sekta binafsi na Serikali katika kutoa huduma bora kwa wananchi.

Amesema Wizara ya Afya imekuwa na ushirikiano mkubwa na Hospitali ya Kairuki katika masuala mengi ikiwemo matumizi ya Bima ya Afya na kwamba pande zote mbili zinatambua kuwa zina wajibu wa kutekeleza dira ya maendeleo ya 2050 inayoelekeza uwepo wa jamii yenye afya bora.


Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Afya na Elimu Kairuki, Kokushubila Kairuki ameishukuru Serikali kwa kutambua mchango wa sekta binafsi katika kuboresha huduma za afya nchini.


Amesema sekta ya afya imekuwa na maendeleo makubwa chini ya uongozi wa  Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan na kwamba  hospitali hiyo itaendelea kuunga  mkono juhudi hizo hasa ikiwa ni utekelezaji wa Dira 2050 inayolenga kujenga Taifa lenye uchumi imara na afya bora.


Amesema gharama za kuweka teknolojia hiyo ya HIFU ni shilingi Bilioni 12 na milioni 300.

 

Aidha amesema kutoka huduma ya HIFU ianze kutolewa tayari wananchi 300 wamepata huduma za uchunguzi huku 298 wakipata matibabu.


 Awali, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Kairuki,  

Dk. Onesmo Kaganda alisema uzinduzi wa HIFU ni tukio la kihistoria kwakuwa ni mara ya kwanza kwa huduma hiyo  kuzinduliwa  katika nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.


Amesema teknolojia hiyo barani Afrika  imeanzishwa katika nchi tatu tu ambazo ni Misri, Nigeria na Afrika Kusini.


Ameeleza kuwa HIFU ni Teknolojia ya kisasa inayotumia Mawimbi Sauti (Sound Waves) b kutibu aina mbalimbali za uvimbe mwilini bila upasuaji, ikiwemo uvimbe wa saratani na usiokuwa wa saratani katika maeneo kama Matiti, Kongosho, Kizazi kwa Wanawake, na Tezi Dume kwa wanaume.


Ameeleza  faida za huduma hiyo kuwa ni pamoja na kutokuwa na kovu kwa kuwa hakuna upasuaji, mgonjwa hawekewi nusu kaputi na mgonjwa hupona kwa muda mfupi na kurejea katika shughuli zake, matibabu hayahitaji kumwongezea damu mgonjwa hata kwa wagonjwa wenye upungufu wa damu, pia kupunguza gharama za kwenda nje ya nchi kutafuta matibabu.


Ameongeza kuwa, faida nyingine ya HIFU ni pamoja na tiba shufaa ambayo husaidia dawa za saratani kufanyakazi vizuri mwilini, kufubaza kukua kwa saratani mwilini (slowdown disease progression) na kupunguza maumivu kwa wagonjwa wa saratani. 


Amesema mtambo huo ulianza kufanya kazi desemba 2023 ambapo mpaka sasa wagonjwa 303 wamefanyiwa uchunguzi na 298 kupatiwa matibabu na kumekuwa na matokeo chanya ya wagonjwa hao.

Amesema kuwepo kwa teknolojia hiyo ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Afya za kuifanya  Tanzania kuwa kitovu cha utalii Tiba Kusini mwa jangwa la Sahara.

Pia, amemshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuweka mazingira wezeshi ya ushirikiano kati ya Serikali na Taasisi Binafsi.

Kuhusu Idara ya Huduma za Dharura iliyozinduliwa katika Hospitali ya Kairuki amesema itakuwa  na uwezo wa kuhudumia wagonjwa zaidi ya 9000 kwa mwaka na pia imejizatiti kwa magonjwa ya dharura pindi yatakapotokea.


Mwisho

GIZ YATOA MSAADA WA VIFAA TIBA VYENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 975 KATIKA HALMASHAURI ZA MKO WA TANGA

May 01, 2025 Add Comment



Na Oscar Assenga, TANGA

SERIKALI ya Ujerumani kupitia shirika la  ufadhili wa kimataifa nchini humo (GIZ) limetoa msaada wa  vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi Milion 975 vitakavyotumika katika hospitali 20 zilizopo kwenye hamashauri mbalimbali Mkoani Tanga hii ikiwa ni  utekelezaji wa programu yake ya  kusaidia na kuimarisha sekta ya afya hapa nchini.

GIZ ambayo inashirikiana na  Wizara ya afya pamoja ofisi ya Rais tawala za mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI)kwa lengo la kuboresha utoaji wa huduma  bora kwa mama na mtoto pamoja na afya ya uzazi  utekelezaji wake umeleta mabadiliko chanya  katika vituo vya afya vilivyoguswa na mpango huo ambao umeanzishwa muda mrefu.



Akipokea vifaa hivyo Mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batilda Buriani ameipongeza Serikali ya Ujerumani  kupitia shirika la GIZ  ambapo kupitia msaada huo unakwenda kuongeza juhudi za Serikali katika kupambana kupunguza na kuondoa kabisa vifo vya wajawazito, wakinamama pamoja na watoto wachanga waliopo chini ya miaka mitano.

Alisema lengo kubwa la Rais ni kupunguza vifo vya wakina mama wajawazito na watoto wachanga chini ya miaka mitano na wameona mafanikio vifo vimepungua kwa kiasi kikubwa sana sasa wamewasaidia kupata vifaa hivyo ili kuongeza vifaa tulivyonavyo na kuhakikisha kwamba watoto wetu wanaozaliwa njiti , wanaozaliwa  na manjano , wanaozaliwa na changamoto ya upumuaji , wanakuwa salama wanapongeza na kuwashukuru kwa msaada huo



Aliongeza kuwa licha ya vifaa hivyo vilivyotolewa bado kuna uhitaji kutokana na idadi kubwa ya wananchi wanaohitaji kupatiwa huduma mbalimbali ambapo ametumia nafasi hiyo kuwaomba shirika la GIZ kuangalia uwezekano wa kuendelea kuwezesha upatikanaji wa wa vifaaa vingine.

" Tumekuwa na mazungumzo na tumekubaliana kwamba waongeze vifaa hivi ni kweli tumepata vingi lakini bado uhitaji ni mkubwa  tunaomba hivi vifaa vilivyopo viongezeke zaidi kutokana na idadi kubwa ya wahitaji tulionao katika vituo na hospitali zetu za halmashauri tuna imani kuwa tutaongezewa ili kuhakikisha kwamba huduma za wakina mama na watoto zinakwenda karibu zaidi na wananchi ikiwemo huduma za kibobezi" aliongeza.



Awali alizungumza Meneja wa  mradi huo hapa nchini Kai Strahler-Pohl  alipongeza juhudi za Serikali katika kuendelea kukabiliana na kupunguza  vifo vya watoto wachanga , kuboresha matokeo ya afya wakina mama na watoto, sambamaba na kuimarisha miundombinu ya vituo vya afya.

Alisema mpango huo umelenga katika  kuwezeshwa uwepo wa  vifaa tiba vya kutosha kwaajili ya kuanzisha vitengo vipya vya utoaji wa huduma  za utunzaji wa watoto wachanga (NCU) katika hospitali za wilaya zote zilizopo Mkoani Tanga .



" Tunafurahi sana kuimarisha  huduma katika halmashauri zote za mkoa wa Tanga hasa kuweza kuzipatia hospital vitengo  vya utunzaji wa watoto wachanga vinavyofanya kazi kikamilifu takribani wakazi 870,000 sasa wanaweza kuwa na uhakika  kwamba Kila mtoto mchanga mvulana na msichana atatunzwa  vizuri karibu na makazi yao"

" Tunathamini ushirikiano wa Serikali kupitia Wizara ya afya  , TAMISEMI, mikoa halmashauri za wilaya zote  pamoja na Serikali ya Ujerumani kukamilisha hili" alisema Meneja huyo.


Awali akizungumza Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt. Frank Shega alilishukuru shirika la GIZ kwa msaada huo ambao pia umeenda sambamaba na utoaji wa mafunzo ya utendaji wa kazi kwa baadhi ya watumishi kwa lengo la kuwaongezea maarifa na ujuzi katika utoaji wa huduma.



"Tunawashukuru na kuwapongeza sana wenzetu wa GIZ kwa  kutupatia msaada wa vifaa  hivi ambavyo vinakwenda kutusaidia kuhakikisha kuwa tunakuwa na vizazi hai na vyenye afya bora wamekuwa pia wakitoa mafunzo kwa watumishi kwaajili ya kuongeza weledi tumekuwa nao kwa muda mrefu na wamekuwa wadau wetu ambao wamwtusaidia sana" alisema Dkt Shega

Mwisho.

PAC YAIPONGEZA MSD KWA KUJENGA GHALA LA KISASA LA KUHIFADHIA BIDHAA ZA AFYA

March 14, 2025 Add Comment

 

 

Na Mwandishi Wetu.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) chini ya Mwenyekiti wake, Mhe. Naghenjwa Kaboyoka (pichani) imetembelea  na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa ghala la kisasa la kuhifadhia bidhaa za afya linalojengwa na Bohari ya Dawa (MSD) katika eneo la Kizota, Mkoani Dodoma.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mhe. Kaboyoka ameipongeza MSD kwa kazi kubwa inayoifanya ya ujenzi wa ghala kubwa na kisasa ambalo litakwenda kutatua changamoto za utunzaji wa bidhaa za afya kwa kiasi kikubwa. 

"Kazi mnayoifanya inaonekana, leo tumeona uwekezaji mkubwa wa ghala la hili kubwa na la Kisasa ambalo lina Ubora wa kimataifa, serikali imewekeza hapa zaidi ya Bilioni 23.7 kujenga ghala hili lenye mita za mraba 7,200 sisi kama kamati tunategemea kuona changamoto za utunzaji wa bidhaa za afya zinapungua”.
Aidha pamoja na kupongeza ujenzi wa maghala Mhe. Kaboyoka amepongeza namna MSD inavyosambaza mashine za kusafisha damu kwa wagonjwa wa Figo ambazo zimepelekea kupunguza ghalama za huduma hiyo kwa wananchi. “Siku izi magonjwa ya figo yamekuwa mengi hadi watoto wadogo wanapata ugonjwa huo tunaishukuru MSD kwa kupunguza gharama ya huduma hii baada ya MSD kuanza kusambaza mashine za kusafisha damu sasahivi tunaona huduma hiyo imepungua gharama kwa kiasi kikubwa. 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya MSD Bi. Rosemary Silaa amesema MSD itaendelea na ujenzi wa Maghala mapya kwa lengo la kutatua changamoto za utunzaji wa bidhaa za afya ambapo baada ya ujenzi huu wa Dodoma na Mtwara MSD itaanza ujenzi wa maghala mapya mkoani Chato, Kilimanjaro, Dar es Salaam, Mwanza na Ruvuma.   MSD kwasasa inauwezo wa kutunza bidhaa hizo kwenye mita za mraba 56,000 huku MSD ikiwa na uhitaji wa mita za mraba 100,000 kukidhi mahitaji yake ya utunzaji.

PAC imetembelea  na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa ghala la kisasa la kuhifadhia bidhaa za afya linalojengwa na Bohari ya Dawa (MSD) katika eneo la Kizota, Mkoani Dodoma.