RAIS DKT SAMIA SULUHU AHUDHURIA HALFA YA UWASILISHWAJI TAMKO LA PAMOJA LA MARIDHIANO YA KISIASA ZANZIBAR KATIKA VIWANJA VYA IKULU ZANZIBAR

July 09, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi wakati wakiwasili katika viwanja vya Ikulu Zanzibar kwa ajili ya kuhudhuria hafla ya uwasilishaji wa Tamko la Pamoja la Muafaka wa Kisiasa baina ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na ACT-Wazalendo, tarehe 09 Julai, 2026. 







Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo Taifa Mhe. Othman Masoud Othman pamoja na Marais Wastaafu wa Zanzibar, Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein, Amani Abeid Karume wakishuhudia utiaji saini wa ajenda zilizokubaliwa na pande zote mbili kwa ajili ya kufanyiwa kazi baada ya Tamko la Pamoja la Muafaka wa Kisiasa baina ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na ACT-Wazalendo, katika viwanja vya Ikulu Zanzibar, tarehe 09 Julai, 2026. Kushoto anaye saini ni Naibu Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo- Zanzibar Omary Ally Shehe pamoja na Naibu Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM- Zanzibar Dkt. Mohammed Said Dimwa


Share this

Related Posts

Previous
Next Post »