Mkutano huu wa siku mbili unawakutanisha viongozi wa Serikali, wawekezaji na wadau wa sekta ya nishati kujadili mustakabali wa nishati barani Afrika, fursa za uwekezaji, pamoja na suluhisho endelevu kwa maendeleo ya sekta hiyo.
Katika mkutano huo, Naibu Waziri ameambatana na wataalam kutoka TANESCO, PURA pamoja na REA ambao watashiriki kwenye majadiliano kuhusu upatikanaji wa umeme kwa wote, uwekezaji katika ‘Energy Mix’ pamoja na usimamizi na maendeleo endelevu ya rasilimali za gesi na mafuta.







EmoticonEmoticon