SERIKALI YAZINDUA KIWANDA DARASA CHA KUBANGUA KOROSHO CHA CAMARTEC MANYONI

September 30, 2025

 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah,akikata utepe kuashiria uzinduzi wa  Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho cha Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC)  kilichopo kijiji cha Masigati wilayani Manyoni Mkoani Singida,hafla iliyofanyika leo Septemba 30,2025.

Na.Alex Sonna-MANYONI

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah, amesema uanzishwaji wa Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho cha Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC) kilichopo kijiji cha Masigati wilayani Manyoni ni hatua muhimu katika kuongeza thamani ya zao la korosho na kukuza ajira kwa wananchi hususan wanawake na vijana.

Akizungumza leo Septemba 30,2025  wakati wa uzinduzi wa kiwanda hicho, Dkt. Abdallah amesema  Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuliwezesha zao la korosho kupitia utafiti, pembejeo zenye punguzo na mafunzo kwa wakulima, hivyo kuhitajika uwekezaji sambamba wa kuongeza thamani.

“Serikali imetoa zaidi ya shilingi milioni 494 kufanikisha uanzishwaji wa kiwanda hiki. Lengo letu ni kuhakikisha wakulima na wajasiriamali hawabaki wauzaji wa malighafi pekee, bali wanapata nafasi ya kuzalisha bidhaa mbalimbali zenye thamani kubwa zaidi,” amesema Dkt. Abdallah.

Aidha ametaja bidhaa zinazoweza kupatikana kutokana na ubanguaji na uchakataji wa Korosho kuwa ni pamoja na siagi ya korosho, juisi ya mabibo, mvinyo wa mabibo, mafuta ya ganda la korosho, kuni mbadala na mabibo makavu ambapo  bidhaa hizo zina soko kubwa ndani na nje ya nchi, na zitasaidia kuongeza mapato kwa wananchi na Taifa kupitia fedha za kigeni.

Dkt. Abdallah amesema kuwa  Kiwanda hicho pia kitaleta suluhu ya changamoto za ukosefu wa teknolojia na elimu ya amali ya kuchakata korosho na mabibo, jambo ambalo limekuwa likiwakwamisha wakulima na wajasiriamali wadogo.

“Kukosekana kwa viwanda vya kuchakata kumetufanya tubaki wauzaji wa korosho ghafi pekee, hali iliyodumaza bei ya zao hili. Bidhaa zilizoongezwa thamani zina soko pana na ndizo zenye faida kubwa,” Amesisitiza.

Amesema kuwa mbanguaji wa korosho kwa kutumia teknolojia za kawaida ana uwezo wa kubangua kati ya kilo 40 hadi 80 kwa masaa nane, na kutoa kilo 10 hadi 20 za korosho zilizokamilika, hali ambayo inaonyesha nafasi kubwa ya kiwanda hicho kuwa kichocheo cha ujasiriamali na ajira.

Hata hivyo , amewataka wananchi wa Manyoni na Watanzania kwa ujumla kuchangamkia fursa za mafunzo na ujasiriamali zitakazotolewa kupitia kiwanda hicho,zitasaidia kuongeza kipato, kukuza ajira na kuimarisha ushindani wa soko la korosho nchini.

“Ni imani yangu kuwa wananchi wataendelea kumuunga mkono Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan katika jitihada za kuendeleza sekta ya viwanda kwa manufaa ya Taifa,” amesema Dkt. Abdallah

Pia  Dkt. Abdallah amehitimisha kwa kusisitiza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi kuhakikisha viwanda vya aina hiyo vinaanzishwa katika maeneo mengine ya uzalishaji wa korosho ili Tanzania isinufaishe tu kwa kuuza ghafi, bali pia bidhaa kamili zinazotokana na korosho na mabibo.

Kwa upande wake  Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Dkt Vincent Mashinji amesema Wilaya yake itaendelea kushirikiana na Wizara ya Viwanda na Biashara Pamoja na Wizara nyingine za kisekta katika kuendeleza na kukuza Sekta ya Viwanda na Biashara hususani katika kuendeleza Viwanda vidogo vya Kati na vikubwa ili kuongeza Ajira, Pato la Taifa na kukuza uchumi kwa ujumla.

Awali akitoa taarifa ya kiwanda hicho Mkurugenzi Mkuu wa CAMARTEC, Injinia Godfrey Mwinama ameeleza chimbuko la kiwanda hicho ni utafiti wa uhitaji wa zana za kilimo na teknolojia za vijijini ambnao umekuwa ukifanyika mara kwa mara na Serikali kupitia utafiti huo ulibaini kuwa ubanguaji wa korosho nchini,hususani kwa wakulima na wabanguaji wadogo ni changamoto.

"Lengo kuu la kiwanda hicho ni kutoa mafunzo,hivyo kiwanda kina kazi kubwa ya kuhakikisha watanzania wenye nia ya kuwekeza,kujiari au kuajiriwa kwenye ubanguaji wa korosho wanapata elimu sahihi ya amali katika eneo hilo"amesema

Naye  Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi ya Camartec, Prof. Valerian Silayo,amesema kuwa kiwanda hicho cha kubangua korosho ni miongoni mwa hatua zinachukuliwa na Serikali katika kutatua changamoto kwenye kuchakata mazao ya kilimo,Mifugo,Uvuvi na Misitu.

"Serikali kupitia CAMARTEC inaendelea kufanya utafiti utakaopelekea  kutatua changamoto za upotevu wa mazao mbalimbali kwa kubuni teknolojia sahihi zenye ufanisi na uhimili wa korosho"Amesema Prof.Silayo

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah, akipokelewa mara baada ya kuwasili katika  Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho cha Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC) kwa ajili ya kukizindua kilichopo kijiji cha Masigati wilayani Manyoni Mkoani Singida.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah, akipokelewa mara baada ya kuwasili katika  Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho cha Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC) kwa ajili ya kukizindua kilichopo kijiji cha Masigati wilayani Manyoni Mkoani Singida.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah,akikata utepe kuashiria uzinduzi wa  Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho cha Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC)  kilichopo kijiji cha Masigati wilayani Manyoni Mkoani Singida,hafla iliyofanyika leo Septemba 30,2025.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah,akizindua  Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho cha Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC)  kilichopo kijiji cha Masigati wilayani Manyoni Mkoani Singida,hafla iliyofanyika leo Septemba 30,2025.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah,akiangalia jinsi korosho zinavyobanguliwa mara baada ya kuzindua  Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho cha Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC)  kilichopo kijiji cha Masigati wilayani Manyoni Mkoani Singida,hafla iliyofanyika leo Septemba 30,2025.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah,akiangalia jinsi korosho zinavyobanguliwa mara baada ya kuzindua  Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho cha Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC)  kilichopo kijiji cha Masigati wilayani Manyoni Mkoani Singida,hafla iliyofanyika leo Septemba 30,2025.

 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah,akiangalia jinsi korosho zinavyobanguliwa mara baada ya kuzindua  Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho cha Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC)  kilichopo kijiji cha Masigati wilayani Manyoni Mkoani Singida,hafla iliyofanyika leo Septemba 30,2025.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah,akiangalia jinsi korosho zinavyobanguliwa mara baada ya kuzindua  Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho cha Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC)  kilichopo kijiji cha Masigati wilayani Manyoni Mkoani Singida,hafla iliyofanyika leo Septemba 30,2025.

 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah,akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Dkt Vincent Mashinji  wakati wa hafla ya uzinduzi wa   Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho cha Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC)  kilichopo kijiji cha Masigati wilayani Manyoni Mkoani Singida, iliyofanyika leo Septemba 30,2025

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah,akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa  Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho cha Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC)  kilichopo kijiji cha Masigati wilayani Manyoni Mkoani Singida, iliyofanyika leo Septemba 30,2025.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah,akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa  Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho cha Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC)  kilichopo kijiji cha Masigati wilayani Manyoni Mkoani Singida, iliyofanyika leo Septemba 30,2025.

Sehemu ya washiriki wakisikiliza hotuba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah (hayupo pichani) wakati wa hafla ya uzinduzi wa  Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho cha Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC)  kilichopo kijiji cha Masigati wilayani Manyoni Mkoani Singida, iliyofanyika leo Septemba 30,2025.

Sehemu ya washiriki wakisikiliza hotuba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah (hayupo pichani) wakati wa hafla ya uzinduzi wa  Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho cha Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC)  kilichopo kijiji cha Masigati wilayani Manyoni Mkoani Singida, iliyofanyika leo Septemba 30,2025.

Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mhe. Dkt Vincent Mashinji,akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa  Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho cha Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC)  kilichopo kijiji cha Masigati wilayani Manyoni Mkoani Singida, iliyofanyika leo Septemba 30,2025.

Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mhe. Dkt Vincent Mashinji,akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa  Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho cha Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC)  kilichopo kijiji cha Masigati wilayani Manyoni Mkoani Singida, iliyofanyika leo Septemba 30,2025.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Bi.Anastazia Tutuba Ruhamvya ,akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa  Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho cha Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC)  kilichopo kijiji cha Masigati wilayani Manyoni Mkoani Singida, iliyofanyika leo Septemba 30,2025.

Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi ya Camartec, Prof. Valerian Silayo,akizungumza  wakati wa hafla ya uzinduzi wa  Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho cha Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC)  kilichopo kijiji cha Masigati wilayani Manyoni Mkoani Singida, iliyofanyika leo Septemba 30,2025.

 Mkurugenzi Mkuu wa CAMARTEC, Injinia Godfrey Mwinama,akitoa taarifa ya kiwanda hicho  wakati wa hafla ya uzinduzi wa  Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho cha Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC)  kilichopo kijiji cha Masigati wilayani Manyoni Mkoani Singida, iliyofanyika leo Septemba 30,2025.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah,akikabidhi vyeti kwa wahitimu wa mafunzo katika   Kiwanda Darasa cha Kubangua Korosho cha Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (CAMARTEC)  kilichopo kijiji cha Masigati wilayani Manyoni Mkoani Singida, iliyofanyika leo Septemba 30,2025.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »