RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO DKT,SAMIA SULUHU HASSAN AHUDHURIA KONGAMANO LA WANAWAKE ZANZIBAR.

July 05, 2024



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Viongozi mbalimbali mara baada ya kuwasili katika Kongamano la Wanawake wa Kiislamu kuukaribisha mwaka mpya wa Kiilamu 1446 katika ukumbi wa Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.

Baadhi ya Masheikh na Wahadhiri mbalimbali waliohudhuria katika Kongamano la Wanawake wa Kiislamu kuukaribisha mwaka mpya wa Kiilamu 1446 katika ukumbi wa Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.

Baadhi ya akina Mama na Waheshimiwa mbalimbali waliohudhuria katika Kongamano la Wanawake wa Kiislamu kuukaribisha mwaka mpya wa Kiilamu 1446 katika ukumbi wa Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.

Mwenyekiti wa Kongamano Sheikh Samir Zulfikar akizungumza katika Kongamano la Wanawake wa Kiislamu kuukaribisha mwaka mpya wa Kiilamu 1446 katika ukumbi wa Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.

Muhadhiri Sheikh Muharrami Mziwanda kutoka Dare es Salaam akiwasilisha mada kuhusiana na Mama ni mhimilli Mkuu wa kuwepo Maadili katika Jamii katika katika Kongamano la Wanawake wa Kiislamu kuukaribisha mwaka mpya wa Kiilamu 1446 katika ukumbi wa Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.

Muhadhiri Sheikh Othman Maalim kutoka Masjid Nuru Muhamad akiwasilisha mada kuhusiana na Athari ya Fitna katika Jamii katika Kongamano la Wanawake wa Kiislamu kuukaribisha mwaka mpya wa Kiilamu 1446 katika ukumbi wa Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.

Katibu Mtendaji Ofisi ya Mufti Mkuu Zanzibar Sheikh Khalid Ali Mfaume akitoa taarifa ya Mwaka Mpya wa Kiislamu katika Kongamano la Wanawake wa Kiislamu kuukaribisha mwaka mpya wa Kiilamu 1446 katika ukumbi wa Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akitoa hotuba katika Kongamano la Wanawake wa Kiislamu kuukaribisha mwaka mpya wa Kiilamu 1446 katika ukumbi wa Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi na Utawala Bora Mwalim Haroun Ali Suleiman akimkaribisha Mgeni Rasmi katika Kongamano la Wanawake wa Kiislamu kuukaribisha mwaka mpya wa Kiilamu 1446 katika ukumbi wa Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.
……….
Ali Issa- Maelezo Zanzibar.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka wananchi wa Tanzania kufuata misingi ya Dini, ili kuepusha mifarakano.

Hayo ameyasema leo katika hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege wakati wa Kongamano la Wanawake wa Kiislamu kufuatia maadhimisho ya mwaka mpya wa kiislam 1446 al-Hijra lililoandaliwa na Ofisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar.

Amesema misingi hiyo humuweka mtu katika heshma, uadilifu na Imani ya ucha Mungu itakayompelekea kumuogopa Mwenyezi Mungu kwa kuwa mwema na kuepukana na mifarakano.

“Mtu yoyote Mwenye kufuata dini huwa mstarabu na kuepukana na mifarakano ambayo itampeleka kwenye uasi”alisema Dkt. Samia.

Aidha alisema kuwa wapo baadhi ya watu wanaokiuka misingi ya dini zao na kutamka maneno mabaya na matusi kwa viongozi jambo ambalo halikubaliki kwani huleta uvunjifu wa Amani nchini.

Hata hivyo Rais Samia aliitaka Ofisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar kusimamia waganga wajadi ili kuweza kuachana na ramli chonganyishi kwani kufanya hivyo kutasababisha maafa kwa jamii .

Nae Sheikhe Othmani Maalimu akitoa mada juu ya athari ya fitna katika jamii alisema wanadamu waepukane na matumizi mabaya ya Ulimi kwani kufanya hivyo husababisha maafa kwa jamii.

Mapema Katibu Mtendaji Ofisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar, Sheikh Khalid Ali Mfaume amesema Kongamano la Mwaka Mpya wa Kiislamu limeanzia Pemba kwa shughuli mbali mbali Tarehe 26/6/ 2024 na linatarajiwa kufungwa kesho na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussen Ali Mwinyi katika Msikiti wa Jamii Zinjibar Mazizini Zanzibar.
Credit FullshangweBlog

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »