RAIS DKT. SAMIA AWAAPISHA VIONGOZI MBALIMBALI IKULU NDOGO ZANZIBAR

July 05, 2024


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.  Samia Suluhu Hassan akihutubia Viongozi pamoja na wageni mbalimbali waliohudhuria hafla ya Uapisho iliyofanyika Ikulu ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 05 Julai, 2024. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.  Samia Suluhu Hassan akiwa na Makamu wa Rais Dkt. Philip Isdor Mpango, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka pamoja na Viongozi walioapishwa katika Ikulu Ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 05 Julai, 2024. Kutoka kulia ni Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Selemani Said Jafo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Ashatu Kachwamba Kijaji, Katibu Mkuu wa Madini Mhandisi Yahya Ismail Samamba pamoja na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)Yusuph Juma Mwenda.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.  Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Dkt. Selemani Said Jafo kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 05 Julai, 2024. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.  Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Dkt. Ashatu Kachwamba Kijaji kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 05 Julai, 2024. 

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.  Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhandisi Yahya Ismail Samamba kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 05 Julai, 2024. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.  Samia Suluhu Hassan akimuapisha Yusuph Juma Mwenda kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 05 Julai, 2024.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »