MELI YENYE WATALII ZAIDI YA 100 YATIA NANGA HIFADHI YA MAGOFU YA KALE KILWA KISIWANI

February 04, 2024

 



Watalii hao wakiongozwa na Kampuni ya Utalii ya Takim Holidays walipokelewa na kukaribishwa kwa ngoma za asili ya watu wa Kilwa Kisiwani iitwayo kitupolo ambayo iliwafanya waonekane wakifurahi muda wote.

Ngome ya Mreno, Msikiti mkubwa na mkongwe, Makaburi ya Malindi na Makutani Palace ni miongoni mwa maeneo yaliyotembelewa na watalii hao ikiwa ni pamoja na kupata fursa ya kujifunza tamaduni za watu wa Kilwa kisiwani.

Historia na upekee wa Hifadhi hii ya Magofu ya Kilwa kisiwani na Songo Mnara imekuwa kivutio kikubwa cha watalii kutoka Kona mbalimbali za Dunia ambao hutembelea Hifadhi hiyo Karibu Kila Mwaka.

TAWA inatarajia kuendelea kupokea Meli nyingine zaidi katika kipindi cha Mwezi Februari na Machi, 2024, na hii yote ni kutokana na Kazi kubwa iliyofanywa na muongoza watalii “Tour Guide” namba moja Nchini Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »