ZIMAMOTO JNIA KUTOA MAFUNZO ENDELEVU

March 10, 2018
 Kamishna Msaidizi wa Zimamoto, Hamis Telemkeni (mbele) akitoa maelezo kwa  washiriki wa mafunzo ya jinsi ya kuzima moto yaliyofanyika kwenye Kituo cha Zimamoto na Uokoaji cha Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) leo.
 Mkaguzi Zimamoto Theresia Tengia  (kushoto) na Sajini Maria Gulam (kulia) wakionesha wafanyakazi wa ofisi mbalimbali zinazoendesha shughuli zake kwenye Kuiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), moja ya kifaa aina ya blanketi linalosaidia kuzima na kufunika  moto endapo utatokea bila kumuathiri kwa kuungua.
 Sajini Maria Gulam (mbele) akionesha namna ya kutumia mtungi wa kuzimia moto kwa washiriki wa mafunzo ya uzimaji moto na uokoaji yaliyofanyika leo kwenye Kituo cha Zimamoto kilichopo katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA).
 Bi. Julieth Fonga (kushoto) wa Kampuni ya General Aviation Services iliyopo Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), akielekezwa na Afisa Usalama wa Zimamoto na Uokoaji, Leonard Chami namna ya kuzima moto kwa kutumia mtungi, wakati wa mafunzo yaliyofanyika leo kwenye kituo cha Zimamoto na Uokoaji cha JNIA.
 Afisa TEHAMA, Bw. Geofrey Youze akifanya zoezi la kuzima moto katika mafunzo yaliyofanyika leo kwenye Kituo cha Zimamoto na Uokoaji cha Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA).
Sajini Maria Gulam leo katika mafunzo ya zimamoto na uokoaji yaliyofanyika katika Kituo cha Zimamoto na Uokoaji cha Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), akionesha namba ya kupiga endapo Mwananchi atakuwa amepata tatizo la moto, ili apate msaada wa haraka.  

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »