Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani (UVCCM),Charangwa Seleman Makwiro.
Mwenyekiti
 wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani 
(UVCCM),Charangwa Seleman Makwiro akizungumza na wajumbe wa baraza la 
vijana wa CCM wa Wilaya ya Bagamoyo wakati wa ziara yake leo mkoani 
Pwani. Kulia ni Mwenyekiti wa UVCCM wa Wilaya ya Bagamoyo,Mkwayu Makota 
na Katibu UVCCM Mkoa wa Pwani,Ramadhan Kapeto. Picha zote na Elisa 
Shunda
Mwenyekiti
 wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani 
(UVCCM),Charangwa Seleman Makwiro akizungumza na wajumbe wa baraza la 
vijana wa CCM wa Wilaya ya Bagamoyo wakati wa ziara yake leo mkoani 
Pwani.
Katibu UVCCM Mkoa wa Pwani,Ramadhan Kapeto akifafanua jambo katika mkutano huo.
Mwenyekiti
 wa UVCCM wa Wilaya ya Bagamoyo,Mkwayu Makota akizungumza katika mkutano
 huo.Kushoto ni Mwenyekiti UVCCM Mkoa wa Pwani,Charangwa Seleman Makwiro
 na Katibu UVCCM Mkoa wa Pwani,Ramadhan Kapeto.
Mwenyekiti
 wa UVCCM wa Wilaya ya Bagamoyo,Mkwayu Makota akizungumza katika mkutano
 huo.Kushoto ni Mwenyekiti UVCCM Mkoa wa Pwani,Charangwa Seleman Makwiro
Diwani
 wa Kata ya Msata,Selestin Semiono (katikati) akichangia hoja kuhusu 
kumuomba Mwenyekiti Charangwa Makwiro kusaidia vijana wapate kazi katika
 miradi na fursa zinazotokea katika maeneo yao katika mkutano huo. Walio
 pembeni kwake ni Wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji UVCCM Mkoa wa 
Pwani,Rashid Likunja (Kulia) na Erasto Makala (Kushoto). 
Mwenyekiti
 wa UVCCM wa Wilaya ya Bagamoyo,Mkwayu Makota wakiteta jambo katika 
mkutano huo.Kushoto ni Mwenyekiti UVCCM Mkoa wa Pwani,Charangwa Seleman 
Makwiro 
Wajumbe
 wa Baraza la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya 
Bagamoyo wakimsikiliza kwa makini Mwenyekiti UVCCM Mkoa wa 
Pwani,Charangwa Seleman Makwirowakati alipokuwa akizungumza nao katika 
mkutano huo.
Mwenyekiti
 wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani 
(UVCCM),Charangwa Seleman Makwiro akimkabidhi Mwenyekiti wa UVCCM wa 
Wilaya ya Bagamoyo,Mkwayu Makota (Kulia) kadi za umoja wa vijana 100 kwa
 ajili ya kusajili wanachama wapya. Anayeshuhudia ni Kulia ni na Katibu 
UVCCM Mkoa wa Pwani,Ramadhan Kapeto.
Mwenyekiti
 wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani 
(UVCCM),Charangwa Seleman Makwiro akimkabidhi Mwenyekiti wa UVCCM wa 
Wilaya ya Bagamoyo,Mkwayu Makota (Kulia) vitabu vya kanuni 100 za Chama 
Cha Mapinduzi (CCM) kwa ajili ya viongozi wa kata za wilaya hiyo kwa 
ajili ya utendaji kazi wao kwa ufanisi katika kutoa maamuzi. 
Anayeshuhudia Kulia ni Katibu UVCCM Mkoa wa Pwani,Ramadhan Kapeto.
Wajumbe
 wa Baraza la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya 
Bagamoyo wakimsikiliza kwa makini Mwenyekiti UVCCM Mkoa wa 
Pwani,Charangwa Seleman Makwirowakati alipokuwa akizungumza nao katika 
mkutano huo.
Mwenyekiti
 wa UVCCM Mkoa wa Pwani,Charangwa Selemani Makwiro (katikati) akiwa 
kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa baraza la UVCCM Wilaya ya Bagamoyo 
leo baada ya kumalizika kwa mkutano wao.
NA ELISA SHUNDA,BAGAMOYO.
WANACHAMA
 wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wa Wilaya ya Bagamoyo
 wametakiwa kutembea kifua mbele huku wakijiamini na kuwaelezea vijana 
wenzao miradi mbalimbali mikubwa inayofanyika hapa nchini chini ya 
uongozi wa Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais,Dk.John Magufuli katika 
kutimiza malengo ya Tanzania ya Viwanda kwa kujenga barabara za juu (Fly
 Over),uboreshaji wa miundombinu,mradi wa umeme vijijini (REA),elimu 
bure shule za msingi na sekondari,ujenzi wa mradi mkubwa wa reli ya 
kisasa ya Standard Gauge,ununuzi wa ndege za Bombadier pamoja na 
kutumbua watumishi vyeti feki.
Hayo 
yamesemwa na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa 
wa Pwani (UVCCM),Charangwa Makwiro wakati akizungumza na vijana wa UVCCM
 wilayani Bagamoyo leo kwenye muendelezo wa ziara yake ya kutembelea 
wilaya zote za mkoa wa Pwani ambapo amewashukuru na kuwakumbusha vijana 
hao kuishi katika ndoto ya Rais Dk.John Magufuli na malengo ya kuifanya 
nchi kuwa Tanzania ya Viwanda katika hotuba waliyozungumza katika 
mkutano mkuu wa vijana hao uliofanyika mjini Dodoma hivi karibuni ambapo
 katika mkutano huo ulimwezesha Kheri James kuwa mwenyekiti wa UVCCM 
Taifa.
“Nimekuja
 katika Wilaya hii ya Bagamoyo kwa ajili ya kutoa shukrani zangu kwa 
ninyi vijana wenzangu kwa kuniamini na kunipigia kura za ndiyo 
zilizoniwezesha kushinda nafasi hii ya uenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Pwani 
hivyo basi nitatumia akili zangu,nguvu,uwezo,rasilimali na elimu 
niliyonayo katika kuhakikisha natatua changamoto za vijana wa mkoa wetu 
wa Pwani leo kichama naonekana nawawakilisha vijana wa Chama Cha 
Mapinduzi peke yake lakini ukweli ni kwamba nitakachokipigania mimi 
kitawaletea faida vijana wote wa mkoa huu hivyo kwa yale nitakayokuwa 
nayapambania kwa vijana nanyi muwe bega kwa bega mniunge mkono katika 
kufanikisha changamoto za vijana” Alisema Mwenyekiti Makwiro.
Aidha 
Mwenyekiti Makwiro amewasisitiza vijana hao kutembea kifua mbele kwa 
kuisemea serikali ya awamu ya tano iliyopo chini ya Mwenyekiti wa CCM 
Taifa na Rais.Dk.John Magufuli kulingana na miradi mbalimbali mikubwa 
anayoitekeleza nchini wao kama vijana wa Chama Cha Mapinduzi ambao ndo 
jeuri ya chama hicho wanapaswa kuzungumza na vijana wenzao kuwakumbusha 
kila siku mambo mema yanayofanywa na kiongozi huyo ambapo watu wasio na 
mapenzi mema na taifa hili wanajaribu kupotosha ukweli na kumsema vibaya
 Rais huyo na wasaidizi wake katika ngazi mbalimbali.
“Vijana 
ndo nguvu ya chama hivyo kwa kutumia utashi wenu ni vyema sasa vijana wa
 Bagamoyo na Mkoa wa Pwani kwa ujumla tupambane kumsemea Rais John 
Magufuli na serikali yake katika mambo mbalimbali ya miradi mikubwa ya 
nchi waliyoifanya ambapo wanatekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)
 tutumie vyema mitandao ya kijamii ya facebook,Instagram na Twitter 
katika kujenga hoja;
“Kuna 
mambo mengi yanayofanywa na serikali ya awamu ya tano mfano ujenzi wa 
barabara za juu (Fly Over),uboreshaji wa miundombinu,mradi wa umeme 
vijijini (REA),elimu bure shule za msingi na sekondari,ujenzi wa mradi 
mkubwa wa reli ya kisasa ya Standard Gauge pamoja na ununuzi wa ndege za
 Bombadier pamoja na utumbuaji wa watumishi hewa na wazembe makazini 
tusemee miradi hii tuachane na watu wasiotaka kusema ukweli juu ya 
utendaji kazi usio na mashaka wa rais wetu” Alisema Makwiro.
 
