ZIARA YA NAIBU WAZIRI WA VIWANDA,BIASHARA NA UWEKEZAJI MHE.INJINIA MANYANYA MKOANI TANGA

February 15, 2018

1
Naibu Waziri Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Injinia Stella Manyanya akikagua maabara ya Vipimo vya sampuli ya bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa na Kiwanda cha Tanga Fresh.
2
Magari maalumu ya kusafirishia bidhaa za kiwanda cha Tanga Fresh katika mikoa mbalimbali,
3
Muonekano wa Kiwanda cha Tanga Fresh kilichopo Mkoani Tanga.
5
Naibu Waziri Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Injinia Stella Manyanya akizungumza na ndugu Amour Alli meneja wa kampuni ya GBP iliyopo mkoani Tanga.
6
Meneja wa Kampuni ya Mafuta ya GBP ndugu Amour Alli akimuonesha Mhe. Naibu Waziri Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Injinia Stella Manyanya sehemu ya upanuzi wa bohari hiyo ya mafuta na jinsi itakavyochochea ukuaji wa uchumi wa nchi.
7
Ziara ya Naibu Waziri Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Injinia Stella Manyanya kutembelea kampuni ya GBP inayojihusisha na usambazaji wa mafuta, Mhe. Waziri ataendelea na Ziara yake mkoani Tanga kukagua Viwanda vilivyobinafsishwa kuona utendaji wake na kutoa maagizo ya kuanza uzalishaji mara moja.
8
Ziara ya Naibu Waziri Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Injinia Stella Manyanya alipotembelea kampuni ya usambazaji wa mafuta ya GBP iliyopo Mkoani Tanga.
9
Naibu Waziri Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Injinia Stella Manyanya akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza ziara ya kutembelea Viwanda vilivyobinafsishwa mkoani Tanga leo tarehe 15/2/2018.
10
Naibu Waziri Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Injinia Stella Manyanya akiwa katika kiwanda cha saruji cha Kilimanjaro kilichopo mkoani Tanga, lengo la ziara hii ni kuona uzalishaji wa Viwanda mbalimbali mkoani Tanga na pia kujua changamoto na kuzifanyia kazi.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »