Wafanyakazi wa TBL wakipata mafunzo sambamba na burudani za vinywaji baada ya saa za kazi.
Wafanyakazi wa TBL Mwanza wakifuatilia mafunzo ya mahusiano na afya.
TBL Mbeya nao walishiriki mafunzo na mijadala ya mahusiano
Kampuni ya TBL Group chini ya kampuni mama ya ABInBev, imeitumia Siku ya Wapendanao kuandaa semina za wafanyakazi wake kuhusiana na masuala ya mahusiano katika familia, zilizoendeshwa na wataalamu wa masuala ya Saikolojia na ushauri nasaha kutoka taasisi mbalimbali za mafunzo nchini. Semina hizo zilifanyika katika viwanda vyake vilivyopo katika mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya, Kilimanjaro na Arusha.
Kwa kutumia kauli mbiu ya ‘Nogesha Upendo Valentine hii’ wafanyakazi walipata fursa ya kupata mafunzo,na kushiriki mijadala kuhusiana na mahusiano bora katika ndoa na familia sambamba na changamoto mbalimbali zilizopo, pia waliweza kupata majibu na ushauri wa changamoto hizo waliokuwa wakiendesha mafunzo.
--
Cathbert Angelo Kajuna,
Founder and Mananging Director
Kajunason Blog,
P.O Box 6482,
Dar es Salaam.
Tel: +255 787 999 774
Alt: +255 765 253 445
www.kajunason.com
"Everything is Possible Through Peace & Stability''