MASOKO YASIYO RAMSI MGANDINI YADAIWA KULIKOSESHA SOKO MAPATO

February 20, 2018
MASOKO yasiyokuwa rasmi yanayolizunguka soko la Mgandani Jijini Tanga yanadaiwa kusababisha upatikanaji wa mapato kuwa madogo.

Hatua hiyo imepelekea uongozi wa soko hilo kuiomba Halmashauri ya Jiji hilo kuingilia kati kutumia nguvu za ziada ili kuweza kuwaondoa wafanyabiashara hao ambao wanauza bidhaa zao kwenye mazingira hatarishi.

Akizungumza na Tovuti hii mwishoni mwa wiki Katibu wa Soko hilo, Ridhiwani Mwinyiheri alisema licha ya hivyo lakini pia wafanyabiashara hao wamepelekea biashara kwa walipoo kwenye vizimba ndani ya soko hilo kukosa wateja.

“Jambo hilo tukilifumbia macho linaweza kukwamisha mipango yetu hivyo tunaiomba Halmashauri ya Jiji la Tanga kuangalia namna mzuri ya kuhakikisha wafanyabiashara hao wanaondoka kwenye maeneo hatarishi ya barabarani “Alisema

“Lakini pia kuwepo kwao nje ya soko kumepelekea hata biashara kuwa ngumu kwani baadhi ya wateja wanaofika hapa huishia nje hivyo kwa wale wanaouzia ndani wanakuwa wakikosa wateja”Alisema.

Hata hivyo aliopngeza hivi sasa soko hilo limekuwa na msongamano mkubwa wa wafanyabiashara ambao wengine wanalazimika kupanga bidhaa zao chini kutokana na ongezeko ambalo limesababisha kwa asilimia kubwa na vijana waliomaliza darasa la saba na kidato cha nne.

“Licha ya hivyo lakini pia hali hiyo imesababishwa na wafanyabiashara wenyewe kwa sababu anamuingiza msaidizi wake sokoni hapo baadae anamtafutia sehemu ya kupanga bidhaa zake”Alisema.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »