NAIBU WAZIRI MAWASILIANO AFASHASTA,AZINDUA MFUMO WA ANUANI ZA MAKAZI ARUSHA

December 19, 2017
SUMATRAAA
Na Mahmoud Ahmad Arusha
Naibu waziri wa mawasiliano na uchukuzi  Afashasta Nditie amezindua Mkutano mkuu wa kujadili mfumo wa Anuani za makazi uliofanyika mkoani Arusha ambao umewakutanisha  wadau mbali mbali wa mawasiliano kutoka barani Africa .
Akizungumza na wadu hao Naibu waziri Nditie amesema  kuwa   mfumo huo kwa hapa nchini  upo vizuri na anaamini kuwa mamlaka husika ipo makini katika  kukamilisha hatua iliyobaki ambayo itaifanya  Tanzania kufika mbali.
Aliongeza kuwa mbali na jitihada mbalimbali zinazofanyika kuweza kufikia kila moja lakini bado kuna changamoto mablimbali za kuwepo na mitaa mingi isiyokuwa na majina ili kuweza kurahisisha huduma ya posta mlangonii.
Kwa upande wake Kaimu Posta  mkuu wa shirika la Posta  Tanzania  Hassani Mwang’ombe amesema  kuwa  hivi sasa wako katika mpango wa huduma ya posta mlangoni ili kuweza kurahisisha barua zote kumfikia kila mmoja mwananchi mahali anakoishi ili kuweza kupata mawasiliano.
Hata hivyo amesema kuwa watanzania watajiskia vizuri na kuona furaha pindi watakapo ona  huduma ya posta inawafikia mpaka milangoni mwao kwani siwananchi wote wanaweza kumudu kwenda mahli paliko huduma ya posta ili kuweza kuwasaidia maelfu ya wakazi walio wengi.
Kwa upande wake katibu mkuu wa Papu Younoss Djibrine alisema kuwa nimwanzo mzuri wa na njia nzuri kwa nchi ya Tanzania kuweza kuanza huduma hii ya anuani na majina ya mtaa ambapo hata united nation nihaki ya kila mmoja kuweza kupata utambuzi wanakoishi lli kuweza kuwafuikia kirahisi zaidi.
Aliongeza kuwa nchi nyingi za afrika zinachangamoto mbalimbali kiwemo kukosa anuiani za makazi yao hali ambayo kuwafikia inakuwa vigumu sana lakini kuna haja za makusudi kuweza nchi husika kuweza kuanzisha utaratibu huo.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »