NAIBU WAZIRI NISHATI SUBIRA MGALU ASEMA VIJIJI 54 MKOANI PWANI KUNUFAIKA NA MRADI WA UMEME WA REA AWAMU YA TATU

December 19, 2017
1
Naibu Waziri wa Wizara mpya ya nishati Subira Mgalu akizungumza na watendaji wa shirika la umeme Tanesco Mkoa wa Pwani pamoja na wakandarasi baada ya kukagua mradi  wa REA awamu ya tatu  uliopo maeneo ya sofu  mlandizi Wilayani Kibaha mkoani Pwani alipofanya ziara yake ya kikazi ya siku moja  kwa ajili ya kujionea mwenendo mzima wa ujenzi.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
2
Naibu Waziri wa nishati Subira Mgalu wa kati kati akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Tanesco Mkoa wa Pwani Martin Madulu wa kushoto katika alipotembelea kituo cha usambazaji wa umeme kilichopo Mlandizi.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
3
Naibu Waziri wa Wizara mpya ya nishati Subira Mgalu akipata ufafanuzi kutoka kwa wakandarasi wa mradi wa umeme wa REA awamu ya tatu katika eneo la Msufini Mlandizi Wilayani Kibaha Mkoa wa Pwani.
4
Naibu waziri mpya wa Nishati Subira Mgalu akisikiliza kwa umakini maelezo kutoka kwa Meneja wa  tanesco Mkoa wa Pwani Martin Madulu wa kushoto mara baada ya kutembelea kituo cha umsambazaji wa umeme kilichopo Mlandizi ikiwa ni ziara yake ya kikazi yenye lengo la kukagua miradi ya nsihati ya umeme (PICHA ZOTE NA VICTOR MASANGU)
…………………………………………………………………………..
NA VICTOR MASANGU, PWANI
VIJIJI vipatavyo 54 katika mkoa wa Pwani  ambavyo  wananchi wake walikuwa katika hali ya sintofahamu  kutokana na kukaa gizani kwa kipindi cha muda mrefu hatimaye wanatarajia kupata na kunufaika na   nishati ya umeme wa uhakika ifikapo mwezi machi mwaka 2018  baada ya  kukamilika kwa mradi wa  kusambaza umeme vijiji (REA) awamu ya tatu.
Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa wizara ya nishati Subira Mgalu baada ya kufanya ziara yake ya kikazi ya siku moja  katika Wilaya ya Bagamoyo pamoja na Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani  kwa ajili ya  kutembelea baadhi ya miradi ya REA ambayo inatekelezwa kwa awamu ya tatu pamoja na kujionea changamoto mbali mbali zinazowakabili.
Pia  Magalu amesema kuwa lengo la serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dk. John Pombe Magufuli ni kuhakikisha inapeleka huduma ya uhakika kwa wananchi  wake pamona na maeneo mengine yenye kutoa huduma za kijamii na kubainisha kuwa wanatarajia ifikapo mwaka 2021 vijiji vtote nchini view vimefikiwa na huduma ya nishati ya umeme.
Aidha Naibu Waziri huyo alipotembelea kituo cha uzalishaji wa umeme kilichopo maeneo ya Mlandizi aliliagiza Shirika la ugavi wa umeme Tanesco  kuhakikisha wanajipanga vizuri ili kuweza  kupunguza malalamiko ambayoyamekuwa yakitolewa na   baadhi ya wananchi  kuunguza vitu vyao majumbani  kutokana  na  tatizo la kukatika katika umeme kila mara bila ya kutoa taarifa.
“Jamani viongozi wangu wa Tanesco kumekuwepo na baadhi ya malalamiko ambayo yamekuwa yakitolewa na wateja kuhusina na hii hali ya kukatika katika kwa umeme mara kwa mara bila ya taarifa hali amabyo inasababisha wakati mwingine wananachi hao kuunguza vitu vyao hivyo katika hili mimi nawaomba mbadilike na mlifanyie kazi katika kuhakikisha lawama hizi zinaondoka kabisa na nina imani mtalifanyia kazi,”alisema Mgalu.
Kwa upande wake Meneja wa Shirika la ugavi wa umeme (Tanseco ) Mkoa wa Pwani Martin Madulu amesema kuwa   kukamilika kwa  mradi huo wa REA awamu ya tatu utakuwa ni mkombozi mkubwa katika suala zima la nishati  ya umeme kwani wanatarajia kuwafikiza zaidi ya  wateja  5000, na kuongeza kuwa mradi huo umegharimu kiasi cha shiingi bilioni 5.
Meneja Madulu aliongeza kuwa lengo la Tanesco ni kuhakikisha kwamba wanaboresha zaidi  huduma ya nishati ya umeme hususan katika maeneo ya vijijini kwa lengo la kuweza  kuwafikia wananchi wengie ambao wataweza kupata fursa ya kutumia nishati hiyo katika kuendeshea shughuli zao mbali mbali za kimaendeleo.
Mhandisi  mkuu ambaye anayesimamia miradi ya umeme wa vijijini (REA) katika Mkoa wa Pwani  Leo Mwakatobe amesema licha ya kujitahidi katika  kunga miundombinu mipya kwa ajili ya nishati hiyo wanakabiliwa na chanagmoto kubwa ya kuwepo kwa baadhi ya wananchi kugoma kuhama kwa ajili ya kupata njia ya kupitsiha  mradi huo hivyo kuwapa wakati mgumu katika utekelazaji wa majukumu yao.
“Katika miradi hii ya kusambaza umeme vijijini kwa kweli baadhi ya maeneo bado tunakabiliwa na changamoto kubwa ya wananchi kuwa wagumu kupisha eneo kwa ajii ya kuweza kupata njia ya kupitisha nishati ya umeme, hivyo inatupa wakat mgumu sana katika kufanya kazi zetu na wengi wao wanadai fidia ya kulipwa lakini katika maradi huu hauna fidia kitu kikubwa ni kutupa ushirikiano katika kufanikisha zoezi hili,”alisema Mhandisi Mwakatobe.
KUKAMILIKA kwa mradi wa umeme vijijini awamu ya tatu (REA) katika Mkoa wa Pwani  utaweza kuvinufaisha vijiji vipatavyo 154 ambavyo baadhi ya vingine vilishapatiwa umeme huo katika awamu ya kwanza  pamoja na  ya  pili.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »