MAHAKAMA YAMHUKUMU ‘MSANII LULU’ MIAKA 2 JELA KWA KIFO CHA KANUMBA

November 13, 2017
_98725855_9c3337b4-dc8f-4663-868e-b031f8808aac
Leo Novemba 13, 2017 Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Dar es Salaam, imemuhukumu msanii maarufu wa filamu nchini, Elizabeth Michael “Lulu” kutumikia kifungo cha miaka miwili gerezani baada ya kupatikana na hatia ya mauaji ya bila kukusudia ya msanii mwenzake marehemu Steven KanumbaHukumu hiyo imesomwa na Jaji Sam Rumanyika ambaye amesema, ameridhika na ushahidi wa mashahidi wanne wa upande wa mashtaka na wazee wa baraza waliotoa maoni yao kuwa kweli mshtakiwa Lulu aliuwa bila ya kukusudia.Lulu ametiwa hatiani chini ya kifungu cha sheria Namba 195 cha cha mwenendo wa mashtaka ya jinai.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »