RAIS DKT SAMIA ATOA MAELEKEZO KWA WAZIRI MCHENGERWA

February 23, 2025


Na Oscar Assenga, HANDENI.

RAIS Dkt Samia Suluhu amemuagiza Waziri wa Tamisemi Mohamed Mchengerwa kuhakikisha wanapeleka kiasi cha Milioni 240 kwa ajili ya kujenga eneo maalumu la Upasuaji wa Mifupa katika Hospitali ya Halmashauri ya wilaya ya Handeni.

Dkt Samia aliyasema hayo leo mara baada ya kufungua Hospitali ya Halmashauri ya wilaya ya Handeni eneo la Mkata ikiwa ni ziara ya siku saba katika Mkoa wa Tanga yenye lengo la kukagua miradi ya maendeleo, kuweka mawe ya msingi na kuzungumza na wananchi.

Alisema kwa sababu wanataka Handeni kuwa eneo maalumu kwa ajili ya Hospitali ya Mifupa pamoja na kuwepo na tiba mbalimbali lakini libaki kuwa maalumu kwa ajili ya mifupa

Aidha alisema kwamba mpaka sasa Hospitali hiyo imeshapokea wajawazito 900 na 300 walijifungua kwa upasuaji na iwapo isingekuwepo lazima kungekuwa na Rufaa na hivyo uwepo wa hospitali hiyo umeokoa maisha ya watu wengi.

Alisema hospitali hiyo ipo barabarani na wakiweka lami kipande kinachotoka Barabarani kwenda hosputali itakuwa karibu na wameamua kujenga aeneo la kufanya upasuaji wa mifupa na nimeelekeza Waziri Tamisema aleta fedha milioni 240 ili kujenga eneo la mifupa likamilike,

“Ukiangalie kuna maeneo ya upasuaji mawli eneo la upasuaji ,upauaji wa jumla na mifupa na hakuna wodi na wanalazwa na wagonjwa wengine hivyo ni vema sehemu ya mifupa ikabakia pekee yake na Handeni ikiwa Hospitali maalumu kwa ajili ya mifupa na mambo mengine na watu wengine wake na wagonwa wengine wa mifupa na maeneo mengine waje kupata huduma”Alisema

Rais Dkt Samia aliawapongeza wana kijiji na uongozi wa kijiji cha Mkata Mashariki kwa kutoa eneo la ekari 32 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali hiyo huku akieleza jambo hilo ni la kuigwa kwani kama wangesubiri Serikali itoe eneo pengine mradi ungeweza kuchelewa.

“Mbali na hayo awamu ya sita Serikali katika wilaya ya Handeni wamepeleka Bilioni 4.37 kwa ajili ya Hospitali hiyo na fedha walizipeleka kwa ajili ya kujenga vituo vya afya na zahanati 16 kwa hiyo ni dhamira ya serikali kuwakinga wananchi wasipatwe na magonjwa .

“Ikitokea wanahitaji matibabu wapate huduma za uhakika zilizokaribu nao ndio maana wameendelea ujenzi wa Hospitali hiyo na kuleta vifaa vya kisasa kwa mkoa wa mzima “Alisema

Alisema kwamba wananchi wa handeni wanamshukuru kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuliunganisha Taifa na wannachi ikiwemo kuwapeleka wadau ambao waliwashika mkono wakajenga majengo mbalimbali na kuifanya hospitali hiyo kwa bora na yenye viwango vya hospitali ya mkoa.

Mchengerwa alisema ujenzi wa jengo hilo ni mpango wa Serikali kuendelea kusogeza huduma karibu na wananchi na maelekezo ya Rais Dkt Samia Suluhu ya kuelekeza kwamba yajengwe majengo kwa ajili ya kuwahudumia wananchi wa handeni na hiyo ni kazi kubwa ya kuunganisha Taifa na mahusiano na watu mbalimbali duniani.

“Wananchi walipata bahati ya kupata wadau wa maendeleo kutushika mkono na kujenga majengo mbalimbali na kuifanya Hospitali yetu kuwa bora na yenye viwango vya Hospitai ya mkoa na kazi hiyo imekwenda kuokoa maisha ya watoto, wakina mama wanaokwenda kujifungua na maisha ya wapiti njia”Alisema

Hata hivyo alisema kwamba Serikali imewezesha ujenzi wa Majengo 15 ya huduma za maabara, majengo muhimu za huduma za nje, huduma za dharura, huduma za mionzi,jingo la huduma za wuzazi ,jengo la dawa na kipindi cha muda mfupi umweza kuokoa maisha ya wakina mama na watoto.

“Mhe Rais Sekta ya Afya inafanya kazi kubwa ya kuokoa maisha ya wakina mama na watoto na wilaya ya Handeni hakuna kifo cha mama na mtoto na wahudumu katika sekta hii wamebadilika na wanafanya kazi kwa bidii kuhakikisha wanaokoa maisha ya watanzania.

Hata hivyo alisema katika Mkoa wa Tanga fedha ambazo zilitolewa na Serikali kwenye sekta ya afya wametoa Bilioni 65.6.


Share this

Related Posts

Latest
Previous
Next Post »