KIKAO CHA TPLB KUFANYIKA OKT. 26, 2017

October 23, 2017
Kamati mpya ya Uongozi ya Bodi ya Ligi Kuu (TPLB) inafanya kikao chake cha kwanza Alhamisi, Oktoba 26 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Moja ya ajenda katika kikao hicho ni kuteua Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi, na kamati nyingine mbalimbali.
TPLB ilifanya uchaguzi Jumapili, Oktoba 15 mwaka huu na kupata uongozi mpya chini ya Mwenyekiti wake Clement Sanga.
Viongozi wengine waliochaguliwa ni Shani Mligo (Makamu Mwenyekiti) na wajumbe Hamisi Madaki, Ramadhani Mahano, Almasi Kasongo na Edgar Chibura.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »