Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA), Dk Agnes Kijazi
(kulia) akizungumza alipokuwa akifungua semina ya kwa baadhi ya
waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari juu ya uandishi
wa habari za hali ya hewa. Wengine kutoka kulia ni Bi. Mariam Mwakilishi
wa Mkurugenzi wa Huduma Saidizi wa TMA na Mkurugenzi Huduma za Utabiri
TMA, Dk. Hamza Kabelwa.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA), Dk Agnes Kijazi
(kulia) akizungumza alipokuwa akifungua semina ya kwa baadhi ya
waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari juu ya uandishi
wa habari za hali ya hewa. Wengine kutoka kulia ni Mkurugenzi Matumizi
Matumizi ya Hali ya Hewa, Dk. Ladslaus Chang'a , Meneja Ofisi Kuu ya
Utabiri, Samwel Mbuya, pamoja na Mkurugenzi Huduma za Utabiri TMA, Dk.
Hamza Kabelwa.
MAMLAKA ya Hali ya
Hewa nchini Tanzania leo imewapa semina baadhi ya waandishi wa habari
kutoka vyombo mbalimbali vya habari juu ya uandishi wa habari za hali ya
hewa. Akizungumza wakati akifungua semina hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa
Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA), Dk Agnes Kijazi alisema semina hiyo ni
utaratibu wa TMA kuwajengea uwezo wanahabari ili waweze kuwa mabalozi wa
zuri wa kutoa elimu kwa umma juu ya matumizi mazuri ya taarifa za
utabiri wa hali ya hewa zinazotolewa na TMA kwa wananchi.
Alisema
wanahabari inabidi wazielewe vizuri, kuzichambua na kuwafikishia taarifa
za utabiri wa hali ya hewa kiusahihi wananchi jambo ambalo litasaidia
wananchi na sekta mbalimbali kujipanga kukabiliana na ama athari
zitokanazo na utabiri wa hali ya hewa.
"...Semina kama hizi kwanza
zinasaidia wanahabari kuelewa masuala mbalimbali yatokanayo na taarifa
zetu za utabiri, kisha wao kuelimisha jamii zaidi kuhusiana na taarifa
zetu kupitia vyombo vyao mbalimbali vya habari. Kundi hili likielewa
vizuri nao watakuwa mabalozi wazuri kufikisha ujumbe kupitia kalamu
zao," alisema Dk Agnes Kijazi.
Aidha pamoja na mafunzo hayo, TMA
pia ilipokea mrejesho na ushauri kutoka kwa wanahabari ili kuboresha
zaidi namna ya utoaji wa taarifa za utabiri wa hali ya hewa kwa umma.
Picha ya pamoja ya washiriki wa semina kwa baadhi ya waandishi wa
habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari juu ya uandishi wa habari za
hali ya hewa.
______________________________ ______________________________ _______________________
Joachim Mushi, Mwenyekiti wa Tanzania Bloggers Network (TBN) na Mhariri Mkuu wa Thehabari.com.
Mail address:- mushi@thehabari.com/ jomushi79@yahoo.com/ info@thehabari.com
Mobile:- 0717 030066 / 0756 469470
Web:- www.thehabari.com
http://joemushi.blogspot.com
Mail address:- mushi@thehabari.com/ jomushi79@yahoo.com/ info@thehabari.com
Mobile:- 0717 030066 / 0756 469470
Web:- www.thehabari.com
http://joemushi.blogspot.com
EmoticonEmoticon