Kocha Mkuu wa Mbeya City Fc,
Kinnah Phiri ametangaza majina ya nyota 18 watakaoivaa Simba Sports Club
kwenye mchezo wa ligi kuu ya Vodacoma Tanzania bara uliopangwa
kuchezwa jumapili hii kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam
Mapema leo Phiri ameuambia
mtandao huu kuwa anatua jijini Dar na kikosi cha nyota hao ambao
aliwaandaa maalumu kwa mchezo huo wa mwishoni mwa juma akiwa na imani
kubwa kuwa wataiwezesha City kuibuka na ushindi kutokana na kuiva
vizuri kimazoezi na mafunzo waliyoyapata katika wiki nzima ya
maandalizianya .
“Nina imani nao kuwa,wamefanya
vizuri sana kwenye mazoezi ya wiki hii, sina shaka na wao kutupatia
matokeo kwa sababu wako sawa tayari kwa mchezo,tutacheza kwenye mfumo
mpya ambao haujawahi kuonekana tukicheza, hii ni kwa sababu tumedhamiria
kupata ushindi kama ambavyo timu imekuwa ikifanya kila inapokutana na
Simba”, alisema.
Miongoni mwa nyota walio kwenye
orodha ya kuivaa Simba siku hiyo ya jumapili ni pamoja na mlinzi Hassan
Mwasapili, mlinda lango Haningtony Kalyesubula pia wamo Temi Felix,
Haruna Shamte,Yohana Moriss,Kenny Ally na wakali wengine 12 ambao
wamepewa majukumu kadhaa kuhakikisha City inaandikisha pointi tatu
muhimu mbele ya timu hiyo ya Msimbazi.