Naibu Waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia James Wambura (katikati)
akipokelewa na Katibu Mkuu Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Bw. Mwesigwa Celestine (kulia) alipofanya ziara katika katika ofisi za
TFF na kuzungumza na wachezaji wa timu ya taifa ya mpira wa miguu ya
wanawake (Twiga Stars) leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Kaimu
Mkurugenzi Maendeleo ya Michezo Bw. Makoye Nkenyenge
Katibu Mkuu Shirikisho la Mpira
wa Miguu Tanzania (TFF) Bw. Mwesigwa Celestine (kulia) akimuonyesha
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia James
Wambura (wapili kulia) moja ya ofisi zinazotumiwa na TFF wakati Mhe.
Waziri alipofanya ziara katika katika ofisi hizo leo Jijini Dar es
Salaam. Wapili kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Maendeleo ya Michezo Bw.
Makoye Nkenyenge
Katibu Mkuu Shirikisho la Mpira
wa Miguu Tanzania (TFF) Bw. Mwesigwa Celestine (aliyesimama) akizungumza
na ugeni ulioongozwa na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na
Michezo kutembelea ofisi za TFF pamoja na kuzungumza na wachezaji wa
Twiga Stars leo Jijini Dar es Salaam. Watatu kulia ni Naibu Waziri wa
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia James Wambura, kulia
ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Michezo Bw. Makoye Nkenyenge
Naibu Waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia James Wambura akizungumza na
wachezaji wa Twiga Stars (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam baada
ya kutembelea ofisi za TFF na kukutana na wachezaji hao kuwahamasisha
wazidi kufanya vizuri katika mashindano mbalimbali ndani na nje ya nchi.
Kushoto ni Katibu Mkuu Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Bw.
Mwesigwa Celestine
Naibu Waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia James Wambura (wanne kushoto)
katika picha ya pamoja na viongozi na wachezaji wa Twiga Stars leo
jijini Dar es Salaam baada ya kufanya ziara katika ofisi za TFF na
kuzungumza na wachezaji hao kuwahamasisha wazidi kufanya vizuri katika
mashindano mbalimbali ndani na nje ya nchi. Watatu kushoto ni Katibu
Mkuu Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Bw. Mwesigwa Celestine
na wanne kulia ni mwenyekiti wa chama cha mpira wanawake Bibi. Amina
Karuma
Wafanyakazi wa TFF katika picha
ya pamoja na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.
Anastazia James Wambura (wanne kushoto) alipotembelea ofisi za TFF leo
jijini Dar es Salaam. Wapili kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Maendeleo ya
Michezo Bw. Makoye Nkenyenge na wapili kulia ni Katibu Mtendaji Baraza
la Michezo la Taifa (BMT) Bw. Henry Lihaya.
Picha na: Genofeva Matemu – Maelezo
…………………………………………………………………………………………………………..
Na: Shamimu Nyaki – Maelezo
Naibu waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura ameipongeza timu ya
Taifa ya wanawake ya mpira wa miguu (Twiga Stars) kwa kufanya vizuri
katika michezo mbalimbali wanayoshiriki ndani na nje ya nchi
iliyopelekea kushika nafasi ya nane katika bara la Afrika kwa mwaka
2015.
Pongezi hizo amezitoa leo jijjini
Dar es Salaam wakati alipozungumza na wachezaji hao katika ofisi za
Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) ambapo wameweka kambi kwa
ajili ya kujianda na Mchezo wao dhidi ya Zimbabwe utakaochezwa mwezi
wa tano mwaka huu.
Mhe. Wambura amewataka wachezaji
hao kujituma kwa bidii, kuwa na nidhamu pamoja na kuzingatia maadili ya
nchi yetu kwa kuwa wao ni mwanga wa jamii ili waweze kufika mbali kama
mchezaji Mbwana Samatta.
“Mnapokuwa kambini zingatieni
maadili, kanuni, sheria zilizopo na kuamini michezo ni ajira kwenu na
inaweza kubadili maisha yenu kwa kujiunga katika vikundi mbalimbali vya
uwezeshaji” Alisema Mhe. Wambura.
Aidha Katibu Mkuu wa Shrikisho la
mpira wa miguu nchini (TFF) Bw. Mwesigwa Celestine akitoa taarifa fupi
ya utendaji wa Shirikisho hilo amesema kuwa kwa upande wa wanawake TFF
inafanya juhudi za kuanzisha ligi ya Taifa ya mpira wa Wanawake kutoa
mafunzo kwa makocha wa mpira wa wanawake pamoja na kufuatilia vipaji vya
watoto wa kike waliopo mashuleni.
Bw. Celestine ameeleza changamoto
mbalimbali zilizopo ndani ya shirikisho hilo ikiwemo baadhi ya sheria
na kanuni zinazosimamia masuala ya mpira wa miguu Tanzania na FIFA
zimekuwa zikitofautiana na sheria za nchi kwa kuwa hazijafanyiwa
marekebisho ili ziweze kua na uwiano ambapo Mhe. Naibu Waziri ameahidi
kuzishughulikia.
Kwa upande wake kapteni wa Timu
ya Taifa ya wanawake ya Mpira wa Miguu (Twiga Stars) Bibi. Sophia
Mwasikile amemshukuru Naibu Waziri kwa pongezi alizowapa na kuahidi kuwa
wataendelea kufanya vizuri zaidi na kuitangaza nchi vizuri kupitia
mchezo huo na kushika nafasi ya juu zaidi ndani na nje ya Afrika.
Timu ya mpira wa miguu ya
Wanawake Twiga Stars imekuwa ni timu pekee Tanzania inayofanya vizuri
katika michuano inayoshiriki japokuwa haina wadhamini hivyo ni wakati wa
wadhamini kujitokeza kuisaidia timu hiyo ili iweze kufanya vizuri
zaidi.