AMINA OMARI TANGA.
MKUU wa Mkoa wa Tanga,Said Magalula ameitaka bodi ya
Usajili wabunifu wa Majengo na wakadiriaji wa Majenzi nchini kutowafumbia macho
baadhi yao wanaotaka kuchafua sifa ya taaluma hiyo kwa kushindwa kutimiza
wajibu wao badala yake wahakikisha wanachukulia hatua kali za kisheria ikiwemo
kufutiwa leseni.
Magalula alitoa wito huo juzi wakati akifungua
semina endelevu ya 24 ya Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na
Wakadiriaji Majenzi inayofanyika mjini
hapa iliyowahusisha wataalamu kutoka sehemu mbalimbali hapa nchini.
Alisema kuwa uchukuaji wa hatua hizo kali utawafanya
wenye tabia za aina hiyo kuacha mara moja kutokana na kuwa endapo watafanya
hivyo wataweza kukumbana na adhabu ikiwemo kulipishwa faini ili iweze kuwa
fundisho kwa wengine.
“Nisema tu hatua
mnazozichukua katika kusimamia sheria pamoja na kuwafutia usajili na
kuwalipisha faini wale wanaokiuka maadili ya taalumu itasaidia hii ni njia
nzuri kwa sababu itaongeza ufanisi kwa baadhi yao kuepuka kufanya vitendo
visivyotakiwa “Alisema RC Magalula.
Alisema kuwa katika mkakati wa kuwajengea uwezo
wataalamu wazawa,aliwashauri kuungana na kuomba kazi kwa pamoja ikiwemo kuacha
ubinafsi kwani hilo limekuwa tatizo kubwa kwa watanzania wengi hali ambayo
imepelekea kulalamika kuwa serikali kuwa haiwajali.
Aidha aliwataka wataalamu kuhakikisha wanajitangaza
kwa kufuata sheria pamoja na kuonyesha jamii kazi zao zinazotokana na ubora ili
kuweza kuwapa utofauti wa kazi iliyofanywa na mtaalam na ile iliyofanywa na mtu
asiyekuwa na taaluma.
Mkuu huyo wa mkoa aliipongeza bodi hiyo kwa kuanza
kujenga mahusiano na taasisi zingine za nchi za Afrika Masharika na nchi za
SADC kwa lengo la kupata uzoefu zaidi katika utekelezaji wa majukumu yenu
itakayowezesha kupanua wigo wa kupata kazi.
“Nipongeza
juhudi hizi nikiamini kuwa mahusiano hayo yatakuwa ya manufaa kwenu kama bodi
na wataalamu wenu …lakini pia kwa manufaa kwa Taifa kwa ujumla kwa kuzingatia
nia dhabiti ya serikali kushirikiana na Mataifa mbalimbali katika kukuza Uchumi…
Awali akizungumza
kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Mwenyekiti wa Bodi ya ya wabunifu
wa Majengo na wakadiriaji wa Majenzi,Tonnie Ambwene Mwakyusa alisema kuwa lengo
la semina hiyo ni kuwakutanisha wataalamu katika sekta ya ujenzi hususani
wabunifu wa majengo,wakadiriaji majenzi,wataalamu wa mpango wa miji na
wahandisi ili kujifunza na kubadilisha ujuzi.
Alisema kuwa katika utendaji kazi wa wataalamu wao
wamekuwa wakikumbana changamoto mbalimbali zikiwemo uelewa mdogo kwa baadhi ya
waendelezaji kuhusu umuhimu wa kutumia wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi
katika kubuni na kutekeleza miradi yao.
Aliongeza kuwa bodi hiyo kwa kuliona hilo inaendelea
kuchukua hatua za kutembelea miradi ya ujenzi na kuelimisha waendelezaji wa
miradi na wadau wengine ambao wanakiuka sheria kwa ikiwemo kuwachukulia hatua
kali kwa kuwasimamisha ujenzi wa mradi na kufunguliwa mashtaka mahakamani.

EmoticonEmoticon