MANCHESTER UNITED KAZI WANAYO KWA DE GEA …Real Madrid wapotaka mtu wao huwa hawazuiliki

November 05, 2014



De Gea celebrates after the final whistle against Everton following a Man of the Match performance
Manchester United inaonekana kukabiliwa na kibarua kizito cha kupigania kumbakisha kundini kipa wake namba moja, David de Gea, baada ya Real Madrid kuelezwa kumfungia kazi kuhakikisha anatua Santiago Bernabeu.
De Gea amekuwa na mafanikio makubwa licha ya United kuwa na mwendo mbaya, na umahiri wake umewatia mzuka mabingwa hao wa Ulaya kutaka kumsajili.
Kipa huyo mwenye miaka 23, mkataba wake wa sasa Old Trafford unakwenda hadi mwaka 2016 na kwa mujibu wa gazeti la Sun la Uingereza, Real Madrid ina matumaini ya kumtia mikononi kwa punguzo la bei katika usajili wa kiangazi kijacho kama mbadala wa muda mrefu wa Iker Casillas.
De Gea – kipa wa zamani wa Atletico Madrid anaaminika kuwa tayari kuhamia Bernabeu na mabosi wa Real Madrid wanaelezwa kuwa na matumaini ya kufanikisha dili lao kama Man United itafeli kucheza Champions League kwa mwaka wa pili mfululizo.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »