MANCHESTER CITY KUZIPIGA BAO LIVERPOOL, ARSENAL NA MANCHESTER UNITED

November 05, 2014



Reus celebrates scoring against the Bundesliga champions, who have a history of signing Dortmund stars
Manchester City inajiandaa kuzipiga bao Liverpool, Arsenal na Manchester United kwa kumpa ofa ya pauni milioni 10 kwa mwaka staa wa Borussia Dortmund mwenye umri wa miaka 25, Marco Reus ili atue Etihad.
Reus amekuwa bidhaa adimu inayosakwa na klabu kibao za Ulaya zikiwamo pia Barcelona na Bayern Munich, lakini kwa mujibu wa gazeti la Bild la Ujerumani, Man City ndiyo inaonekana kudhamiria kufanya kweli kwa kuweka mezani ofa hiyo kubwa.
Hivi karibuni Reus alionyesha nia ya kutaka kubaki Borussia Dortmund, lakini kutokana na klabu hiyo kutaabika katika Bundesliga kwa sasa, staa huyo atalazimika kufikiria upya mustakabali wake mwisho wa msimu, hasa kama kikosi cha Jurgen Klopp kitashindwa kufuzu kwa Champions League.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »