KWA MARA YA KWANZA AZAM FC MABINGWA WAPYA LIGI KUU BARA 2014 TANGU 1965

April 14, 2014


 Wachezaji wa Azam Fc, wakishangilia ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mbeya city katika mchezo wao wa Ligi Kuu uliochezwa jana Jijini Mbeya na kutangaza ubingwa rasmi kwa kufikisha jumla ya Pointi 59 wakiwaacha Yanga ambao nao pia waliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya JKT Orjolo walicheza jana jijini Arusha na kufikisha jumla ya Pointi 55 huku wakiwa wamesalia na mchezo mmoja dhidi yao na Simba utakaochezwa Aprili 19, ambao hata wakishinda hawataweza kufikia pointi za wapinzani wao katika mbio hizo Azam, ambao nao pia wamesalia na mchezo mmoja ambao hata wakishinda au kushinda hauna faida wala hasara kwao.
BAADA ya Azam kufanikiwa kutwaa taji la ubingwa jana jijini Mbeya kwa kuwalaza wenyeji wao Mbeya City, imeweka rekodi ya kuwa klabu ya tisa kunyakua taji hilo nchini tangu mwaka 1965.

Azam imetwaa ubingwa huo ikiwa na jumla ya Pointi 59 ikiwa imecheza michezo 25, huku wapinzani wao katika mbio hizo, Yanga wakibaki nafasi ya pili baada kuwabamiza Oljoro JKT mabao 2-1 katika mchezo wao uliopigwa kwenye Uwanja wa Sheikh AMri Abeid jijini Arusha na kufikisha jumla ya Pointi 55.

Azam waliweza kushika nafasi ya pili misimu miwili mfululizo nyuma ya Simba na Yanga, ambapo msimu huu wameonyesha uchu wa kuitamani na kumudu kuiwania vyema nafasi ya kwanza na hatimaye kufanikiwa.

Ukiondoa Yanga na Simba walionyakua mataji mara nyingi, Azam itaingia kwenye orodha ya walionyakua ubingwa huo ikifuata nyayo za Cosmopolitan iliyofanya hivyo kwa mara ya kwanza mwaka 1967.

Baada ya Cosmo waliofuata walikuwa ni Mseto ya Morogoro waliofanya hivyo mwaka 1975, kisha Pan Africans iliyoweka rekodi mwaka 1982, ikafuatiwa na Tukuyu Stars iliyonyakua mwaka 1986 na kufuatiwa na Wagosi wa Kaya, Coastal Union mwaka 1988.

Klabu ya Mtibwa Sugar ilikuja kuweka rekodi ya kunyakua taji hilo la Ligi Kuu misimu miwili mfululizo mwaka 1999 na 2000 kabla ya Simba na Yanga kupokezana taji hilo tangu hapo hadi msimu huu ambapo inaelekea wazi Azam wanaingia kwenye orodha hiyo.


 Azam imeweka rekodi hiyo ya kuwa timu ya tisa kunyakua taji hilo na kuisimamisha Yanga iliyoshikilia taji hilo la 24, ikiongoza orodha ya klabu zilizonyakua mara nyingi ikifuatiwa na Simba iliyotwaa mara 18.

ORODHA KAMILI YA MABINGWA WA LIGI KUU TANGU 1965-
    1965 Sunderland (Simba)
    1966 Sunderland
    1967 Cosmopolitan
    1968 Yanga
    1969 Yanga
    1970 Yanga
    1971 Yanga
    1972 Yanga
    1973 Simba 
    1974 Yanga
    1975 Mseto 
    1976 Simba 
    1977 Simba 
    1978 Simba 
    1979 Simba 
    1980 Simba 
    1981 Yanga
    1982 Pan Africans
    1983 Yanga
    1984 Simba 
    1985 Yanga
    1986 Tukuyu Stars
    1987 Yanga
    1988 Coastal Union
    1989 Yanga
    1990 Simba 
    1991 Yanga
    1992 Yanga
    1993 Yanga
    1994 Simba 
    1995 Simba 
    1996 Yanga
    1997 Yanga
    1998 Yanga
    1999 Mtibwa Sugar
    2000 Mtibwa Sugar
    2001 Simba 
    2002 Yanga
    2003 Simba 
    2004 Simba 
    2005 Yanga
    2006 Yanga
    2007 Simba 
    2007/08 Yanga
    2000-09 Yanga
    2009-10 Simba SC
    2010-11 Yanga
    2011-12 Simba SC
    2012-13 Yanga 
    2013-14 Azam Fc

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »