WAZEE WAIOMBA SERIKALI KUWAJENGEA UZIO.

January 30, 2014
Na Elizabeth Kilindi,Muheza.

WAZEE  wanaoishi kwenye kambi ya Ukoma Iliyopo Ngomeni wilayani Muheza wameiomba serikali kuwajenga uzio kwenye kambi hiyo ili kuwanusuru na vibaka wanaowavamia mara kwa mara na kupora mali zao ikiwemo mifugo pamoja na  ujenzi wa vyoo bora.

Ombi hilo wakati  wakipokea Msaada wa nguo na chakula kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU Mkoa wa Tanga  wakati taasisi hiyo ilipo kwenda kutembelea kambi hiyo ili kubaini changamoto zinazowakabili.


Aidha alisema kambi hiyo ipo mbali na makazi ya watu huku wanaoishi ni wengi wao ni wazee hivyo inakuwa rahisi kwa vibaka na wezi kuwavamia mara kwa mara hasa katika kipindi wanacho pelekewa misaada na wasamaria wema kwama wao.

“Tatizo kubwa sisi tunaiomba serikali ituangalie katika swala la kujengewe uzio na uhakika wa maji safi na salama kwani kwasasa hakuna inatulazimu kwenda mwendo mrefu kutafuta maji huku hata bwawa lilichimbo kwa ajili yetu limekauka kwa kukosa mvua”alisema  Mohamed Salimu.

Kwa upande wa Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Muheza Mathew Mganga alisema kuwa kambi hiyo inajumla ya wazee 86 ambao wanatumia  matundu matatu ya vyoo ambayo hayaelingani na idadi ya watu waliopo tu hali inayohatarisha usalama wa afya zao kwa ujumla.

Pia aliongeza kuwa  kwa sasa bajeti inayotolewa na Wizara ya Afya kwa kambi hiyo ni ndogo licha ya Halimashauri kutenga mafungu kwa ajili ya kutatua matatizo madogo yalikuwepo bado hali hasa miundombinu ya majengo sio ya kuridhisha.

Naye Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Tanga Edson Makallo alisema kuwa  iwapo  watendaji kwenye ngazi ngoze wangeweza kusimamia fedha za maendeleo na kuhakikisha zinawafikia walengwa rushwa katika nchi hii ingepungua au kwisha kabisa.

“Kwa kweli lengo letu ni kuhakikisha  tuwajibika katika kuwafikia wananchi wote  na kutoa elimu kuhusu madhara ya rushwa pamoja na kusimamia raslimali za maendeleozinasimamiwa ipasavyo  ikiwa  kupunguza mianya ya rushwa katika huduma za kijamii”alisema Makallo.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »