Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Shaka Hamdu Shaka, akikagua miundombinu ya barabra iliyoharibiwa na mvua kubwa iliyonyesha wilayani humo.
.....................................
Na Dotto Mwaibale
Uongozi ni dhamana aliyopewa kiongozi husika kwa ajili ya
kusimamia shughuli za maendeleo pamoja na changamoto mbalimbali za wananchi zinapo
jitokeza na siyo kukaa ofisini na kuwatuma au kuwaagiza wakuu wa idara kwenda
kuzishughulikia.
Disemba 26 2025 mvua
kubwa zilinyesha katika Tarafa ya Kidete wilayani Kilosa mkoani Morogoro na
kuharibu baadhi ya miundombinu ya barabara na mashamba na kuwaacha wananchi
wasijue la kufanya.
Kutokana na wilaya hiyo kuwa na kiongozi bora na mchapakazi ambaye anaguswa na changamoto za wananchi Desemba
30, 2025 Mkuu wa wilaya hiyo Shaka Hamdu Shaka akimbatana na kamati ya Ulinzi
na Usalama ya wilaya bila ya kuchelewa walienda kukagua maeneo yote yaliyoathirika
na mvua hiyo ili kuona ukubwa wa changamoto hiyo ili Serikali iifanyie kazi na
maisha ya wananchi yaendelee kama kawaida baada ya miundombinu iliyoharibiwa na
mvua hiyo kurekebishwa.
Mvua hiyo iliyoambatana na upepo imesababisha athari kwa
wakazi wa kata mbili za Dumila na Magole ikiwa ni pamoja na nyumba za makazi na
biashara kuathiriwa pamoja na baadhi ya
miundombinu ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na baadhi ya taa za
barabarani.
Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Shaka Hamdu Shaka aliyetembelea maeneo
yalioathirika na mvua hizo alisema serikali inafanya tathmini ya haraka ili
kujua athari zilizojitokeza.
DC Shaka alisema kuwa zaidi ya nyumba 120 zikiwemo za makazi
pamoja na maghala mawili ya kuhifadhia
nafaka yamekumbwa na maafa hayo.
Aidha amesema kuwa mpaka sasa hakuna athari ya kibinadamu
iliyojitokeza kutokana na upepo huo huku akitoa wito kwa wananchi wote wa
kilosa kuchukua taadhari kipindi hiki cha mvua.
Ukaguzi wa maeneo yaliyoathiriwa na mvua hizo ukiendelea.
Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Shaka Hamdu Shaka, akikagua maeneo hayo.
ukaguzi ukiendelea
Kazi ya ukaguzi ikiendelea
EmoticonEmoticon