CCM TANGA YAMPONGEZA JK

December 26, 2013
Na Mbaruku Yusuph,Tanga.
Imewekwa Desemba 26 saa 12:25 Mchana.
 
CHAMA cha Mapinduzi CCM,Mkoani Tanga kimempongeza Mh;Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuridhia maamuzi ya  bunge ya kuwataka Mawaziri wanne kujiuzulu nyadhifa zao.

Akizungumza na TANGA RAHA ofisini kwake Katibu wa CCM Mkoa Tanga,Gastav Muba  kuwa msimamo uliowekwa na Bunge kwa Mawaziri hao wanne wa kuwajibishwa ni sahihi kwa lengo la kulinda maslahi ya chama na  mwananchi kwa ujumla.

Aidha alisema kuwa wananchi wanapaswa kufahamu  kila maamuzi magumu yanayochukuliuwa na serikali si kwa utashi wa chama tu ,bali ni kwa ajili maslahi ya wananchi amabao kwa namna moja au nyingine ndio wanaoumia.

            “Nani hatambui kuwa wananchi ndio wenye nchi?.Wananchi ndio msingi mkuu wa nchi kwa nini serikali isichukue hatua kali kwa watumishi wasio waadilifu?”Alihoji bwana Muba.

Muba alizidi kufafanua kuwa hatua hiyo imekuja muda muafaka kwa Chama kwa kuwajengea imani wanachama wake ambao ni kundi kubwa linalo pata madhila pindi panapotokea uvunjifu wa haki za binaadamu hapa nchini
.
Alisema kitendo cha Mh; Rais kuridhia uwajibishwaji kwa Mawaziri hao ni ukomavu kwa Chama na kulinda maslahi ya mwananchi kitu ambacho kitakiletea tija chama na wala si udhaifu katika chama kama habari zinavyo zagaa hapa nchini.

            “Unajua ikiwa Waziri au Mawaziri,wameshindwa kusimamia vema utekelezaji wa majukumu yao na kuwasimamia waliochini ya wizara zao katika sekta yoyote serikalini,Si udhaifu wa chama bali ni mapungufu ya mtu mwenyewe binafsi  na kujisahau kama amebeba dhima kubwa ya kuwatumikia wananchi na hakuna sababu ya kuleyana”Alisema katibu huyo.

Hata hivyo aliwapongeza Wabunge wote bila ya kuangalia tofauti ya vyama vyao,Mawaziri na Mh: Raisi kwa kubeba dhamana kubwa ya kusimamia vema maslahi ya mwananchi ambae ndio msingi mkubwa katika chi yoyote duniani.

Aliwaomba wananchi wote Mkoani Tanga kuwa na imani na  chama chao  na kuacha kusikiliza propaganda zinazoenezwa mitaani kuwa chama sasa kimepoteza uwelekeo hakuna kitu kama hicho,kuwajibishwa kwa Mawaziri hakupelekei kupoteza uwelekeo kwa CHAMA.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »