Na Masanja Mabula -Pemba .
Hatimaye
mashabiki wa vilabu vya Jamhuri na Kizimbani zote za mjini Wete,
wamevunja ukimiya na kuuomba uongozi wa timu hizo kupanga mikakati
itakayoziwezesha timu hizo kubakia kwenye michuano ya ligi kuu ya
Zanzibar msimu ujao .
Wakizungumza
kwa nyakati tofauti , wamesema kuwa mwenendo wa timu hizo kwenye ligi
kuu ya Zanzibar inayoendelea sio wa kuridhisha , jambo ambalo
limezifanya timu hizo kushika nafasi za chini kwenye msimamo wa ligi
hiyo .
Aidha
wameongeza kwamba huwenda Mji wa Wete kukosa timu inayoshiriki ligi
kuu msimu ujao , endapo hatua za makusudi hazitrachukuliwa na viongozi
wa timu hizo kwa kuweka mikakati madhubuti pamoja na kufanya usajili
wakati wa dirisha dogo .
"
Hii itakuwa ni aibu kwa Mji wa Wete kukosa timu ya kushiriki ligi kuu ,
na lwamba viongozi wa vilabu hivyo wanapaswa kufanya usajili wakati wa
dirisha dogo litakapofunguliwa " alisisitiza shabiki mmoja
aliyejitambulisha kwa jina Omar Juma .
Wameeleza
kwamba klabu hizo ambazo zinawawakilisha wananchi wa Mji wa Wete na
Wilaya hiyo kwa ujumla , ambapo mikakati ya makusudi inahitajika ili
kunusuri timu hizo kushuka daraja .
Kombo
Said shabiki wa Timu ya Jamhuri alisema kuwa wanashangaa kuona timu yao
imekuwa kichwa cha mwendawazimu tofauti na ilivyokuwa kwa miaka ya
nyuma ambapo ilikuwa tishio kwa vilabu vya ligi kuu Zanzibar .
"Matatizo
ya timu yetu kufanya vibaya yamechangiwa na viongozi wetu kwa kukubali
kuwatoa wachezaji zaidi ya sita wa kikosi cha kwanza na wao kushindwa
kusajili wachezaji wa kuweza kuziba nafasi hizo " alieleza Kombo .
Hata mmoja wa Viongozi wa Klabu ya Jamhuri ambaye hakutaka jina lake kutajwa alisema kuwa uongozi umekusudia kuvunja benki na
kufanya usajili wa kutisha wakati wa dirisa dogo pindi likifunmguliwa .
Aliwatoa
hofu mashabiki na wapenzi wa klabu hiyo ,kuondoa wasiwasi na kwamba
timu itaendelea kubaki kwenye ligi kuu Zanzibar kwani mapengo
yalijitokeza katika kipindi hichi tayari wamo katika kuyapatia ufumbuzi.


EmoticonEmoticon