Na Masanja Mabula -Pemba
.
Kocha Mkuu wa Timu
Jamhuri Said Mohammed ameamua kuikacha timu hiyo baada ya kudai kuwa hakuna
utulivu ndani ya timu hali ambayo imepelekea kuweko na makundi kati ya Viongozi
jambo ambalo limepelekea matokeo mabaya kwenye michuano ligi kuu ya
Zanzibar .
Akizungumza na mwandishi
wa habari hizi , kocha huyo mwenye leseni ya daraja la C linalotambuliwa na
Shirikisho la Mpira la Afrika ( CAF) amesema kuwa uwamuzi wa kuicha timu
umekuja baada ya kuona kuwa baadhi ya viongozi wanahusika katika kuihujumu timu
.
Amesema kuwa pamoja na
mapungufu yaliyopo ndani ya kikosi cha timu hiyo Kongwe Visiwani hapa , lakini
baadhi ya viongozi wamehusika moja kwa moja katika matokeo mabaya uwanjani .
"Haiwezekani
kiongozi unasema kwa kuwaambia wachezaji kuwa tunnakwenda uwanjani kufungwa ,
badala ya kuwa wewe uwe ni chachu kuwahamisha wachezaji kufanya vizuri , kama
sio hujuma ni nini mwandishi ? alihoji .
Aidha ameeleza kwamba
kwa mujibu wa timu inavyocheza mpira uwanjani , hakuna sababu ya kuwa tushike
nafasi ya chini kwenye msimamo , na kutokana na hali hiyo nimeona bora niachie
ngazi kuonoa timu hiyo .
" Mimi nafanya kazi
kwa bidii , maarifa na nguvu zote , lakini kutokana na hali hii ndiyo
maana nimeamua kuachia ngazi , naamini sasa viongozi watatambua kwamba hujuma
zao hazilengi katika kuimarisha timu bali zinabomoa " alieleza .
Akizungumzia malengo
yake ya badaye kocha Said amesema kuwa kwa sasa hana mpnago wa kufundisha timu
kutokana ambapo anataka kutuliza akili yake baada ya kutumia muda mwingi katika
klabu ya Jamhuri .
"Unajua nimetoka
kufundisha timu yenye mashabiki wengi , kwa sasa siwezi kukurupuka na kuamua
kutafuta timu ya kufundisha kwa kipindi hiki " alifahamisha .
Akizungumza na gazeti
hili , Meneja wa Timu hiyo Abdalla Mohammed Elisha amekiri kupokea taarifa za
kocha huyo kujiuzulu , na kuongeza kwamba sababu za kocha kuachia ngazi
hazielewi .
"Ni kweli kocha
wetu ameiacha timu kuanzia jana (juzi) lakini sababu zilizomfanya aiache timu
mtafute na muulize yeye , mimi sizielewi na naamini ni uwamuzi wake
mwenyewe "
Elisha amekanusha kwamba
kocha huyo haelewani na baadhi ya viongozi wa timu hiyo na kwamba uwamuzi wa
kuachia ngazi ni wake binafsi .
Tayari zipo taarifa
kwamba kocha huenda akajiunga na timu ya Konde Star inayoshiriki ligi daraja la
kwanza Taifa Pemba ambayo alikuwa anaifundisha kabla hajajiunga na timu ya
Jamhuri .
EmoticonEmoticon