HAMISI JAFFARY MWENYEKITI MPYA KIKAPU TANGA

October 14, 2013

Na Oscar Assenga,Tanga.
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Kikapu mkoa wa Tanga (TRBA),Hamisi Jaffary amefanikiwa kutetea kiti chake katika uchaguzi mkuu wa chama hicho uliofanyika jana,katika ukumbi wa Bandari mkoani hapa.

Uchaguzi huo ambao ulisimamiwa na Afisa Utamaduni wa Jiji la Tanga Peter Semfuko ulikuwa na upinzani mkubwa kwa baadhi ya nafasi ambazo zilikuwa zikigombewa na wagombea zaidi ya wawili.

Akitangaza matokeo hayo,Semfuko alimtangaza Jaffary kushika nafasi hiyo baada ya kupata kura 23 za ndio kati ya 24 ambazo zilipigwa na wajumbe wa mkutano huo wa uchaguzi kwenye wadhifa ambao alikuwa akigombea peke yake.

Katika uchaguzi huo nafasi ya Makamu Mwenyekiti ilichukuliwa na Rajab Ahmed “Babla”kwa kupata kura 23 huku kura I ikisema hapana ambapo pia hakuwa na mpinzani.

Nafasi ya Katibu Mkuu ilichukuliwa na Calistus Zakaria kwa kumbwaga mpinzani wake Patric Semindu kwa kupata kura 15 kati 6 alizipata mgombea mwenzake.

Kwenye uchaguzi huo nafasi ya Katibu Msaidizi ilichukuliwa na Gilo Mwanakatwe aliyepata kura 19 kati 2 alizopata mpinzani wake Said Ramadhani huku nafasi ya mweka hazina ikichukuliwa na Twahiru Mdimu aliyepata kura 19.

Nafasi nyengine ni wajumbe wa kamati ya utendaji waliochaguliwa ni Ally Senkole,Hassani Sakala,Omari Kupe na Frank Masumba.
Katika nafasi ya mwakilishi wa wachezaji mkutano mkuu Taifa kwa mkoa wa Tanga ilichukuliwa na Saa Mumy Mohamed aliyepata kura 14 kati ya 6 alizopat mpinzani wake Adam Issa Semkonde.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »