WATANZANIA WAASWA KUCHANGIA UJENZI WA VYUMBA VYA MADARASA.

October 02, 2013

NA OMARY MLEKWA,HAI
WATANZANIA wametakiwa kujitokeza katika kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa   kwa ajili ya watoto  wenye ulemavu ili kuwapatia fursa ya  kupata elimu sawa na watoto wasiokuwa na ulemavu badala ya kutegemea serikali pekee

Akizungumza katika ziara ya kutembelea watoto wenye ulemavu wa akili katika kata ya Machame Mashariki, katibu wa chama cha watu wenye ulemavu wa akili wilayani Hai, Anjella Mallya hali ya miuondo mbinu katika shule nyingi hapa nchini hairuhusu kuwapa fursa watoto wenye ulemavu

Alisema hali hiyo imesababishwa na jamii kuwatenga na kuwabagua wenye ulemavu katika suala nzima la kielimu kwa kutegemea serikali pekee katika kukabiliana na tatizo hilo jambo ambalo limekuwa likichangia zaidi watoto wengi kushindwa kupata haki zao za msingi katika elimu

“Ni  jukumu letu sote kuwatazama watu wenye walemavu kama watu wengine na tusiwachife watoto wenye ulemavu badala yake jamii ihakikishe inaboresha mangira ya watoto hao kwa kina kama ilivyo kwa watoto wengine ”alisema Mallya

“Tuwasaidie na kuwajali kwa kuhakikisha wanapata elimu katika
mazingira rafiki, ili waweze kuchagia maendeleo katika taifa kwani nao wana uwezo wa kujitegemea iwapo tutawaunga mkono, bila kusahau kuwa ulemavu hauombwi wala kununuliwa bali unakuja tu,” alisisitiza .

Alisema endapo jamii ikishirikiana na Serikali kuwa na majengo maalumu ya kwa ajili ya watoto wenye ulemavu itasaidia kuwavutia watoto hao kusoma kwani mazingira wanayosemea katika shule za kawaidia yamekuwa si rafiki nao
 

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »