Na Mwandishi Wetu,Tanga.
TIMU ya Coastal Union “Wagosi wa Kaya”leo imeendelea na
mazoezi yake katika uwanja wa Mkwakwani mkoani hapa ikijiandaa na msimu mpya wa
Ligi kuu Tanzania bara ambao utaanza mwezi ujao.
Mazoezi hayo ambayo yalianza majira ya saa nane mchana
yalikuwa kivutio kikubwa kwa wapenzi na mshabiki mbalimbali wa soka mkoani hapa
ambao mara nyingi hufuatilia mazoezi hayo kutoka pande zote za mkoa huu.
(KOCHA Mkuu wa Coastal Union Hemed Morroco kushoto akiteta jambo na Pius Kisambae huku Seleman Kassim Selembe akishuhudia)
Wachezaji ambao walionekana kuwakonga nyoyo mashabiki wa soka hapa wapenzi ni Haruna Moshi “Boban”,Christian Odula wa Nigeria,Jerry Santos,na wachezaji wengine chipukizi waliowasili kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini.
Akizungumza na Blog hii mara baada ya kumalizika mazoezi
hayo,Kocha Mkuu wa timu hiyo,Hemed Morroco alisema maandalizi ya kuelekea msimu
mpya yanaendelea vizuri kwani wachezaji wana hari na nguvu mpya.
Morroco alisema mechi ya kwanza ambayo atatumia kuangalia
kikosi hicho ni kati yao na URA ya Uganda mchezo unaotarajiwa kucheza Jumatano
wiki hii kwenye uwanja wa Mkwakwani mkoani hapa.
(Mashabiki wakifuatilia mazoezi ya timu hiyo leo jioni uwanja wa Mkwakwani)
Alisema watakapomaliza mechi hiyo wataelekea Mombasa Kenya kucheza na Bandari lengo likiwa kukipa makali kikosi hicho ambacho kimepania msimu ujao kuchukua kombe la Ligi kuu hapa nchini.
Alisema watakapomaliza mechi hiyo wataelekea Mombasa Kenya kucheza na Bandari lengo likiwa kukipa makali kikosi hicho ambacho kimepania msimu ujao kuchukua kombe la Ligi kuu hapa nchini.
Mwisho.
EmoticonEmoticon