“CHIPUNGAHELO aipigia saluti Kokoliko Digner”

July 21, 2013


(Mkurugenzi wa Kampuni ya Kokoliko Disgner, Aisha Kisoki “Mama Sophia akiwa bize ofisni kwake hivi karibuni)

Na Mwandishi Wetu, Tanga.

RAIS wa Miss Utalii nchini, Gidion Chipungahelo amesema kampuni ya Kokoliko Disgner ndio kampuni pekee waliyoamua kuipa kibali cha kuwavalisha washiriki wa Miss Utalii hapa nchini na nje ya nchi lengo likiwa ni kutambua mchango wao kwenye tasnia hiyo.

Akizungumza jana, Chipungahelo alisema licha ya kuwavalisha na kuwabuni mavazi washiriki wa miss Utalii hapa nchini lakini watawatangaza kitaifa na kimataifa kwenye mashindano ya Tourist Model of the world itakayofanyika mwezi septemba mwaka huu nchini Japan kwa kuwa nao.

Chipungahelo alisema suala lengine ambalo kampuni hiyo itakalolifanya ni kuondoka nao hapa nchini kwenda kushuhudia shindano la Miss Utalii Dunia ambalo litafanyika Equatorial Guinner desemba 10 mwaka huu.

 “Mchango wa kampuni hiyo ni mkubwa sana hasa kwenye suala zima la ubinunifu wa mavazi hivyo hii itakuwa fuksa adimu kwao kuwaonyesha mavazi yao na mitindo mbalimbali kwenye nchi hizo “Alisema Chipungahelo.

Alisema safari nyegine ya tatu ambao watakuwa nao ni kwenye shindano la Miss tournament Umoja wa Mataifa ambalo litafanyika Florida nchini Marekani na kueleza watashirikiana na kampuni ya Sophia production ,kokoliko kwa ajili ya kwenda kuwatangaza  kama wabunifu wa mavazi wa kitanzania.

Aliongeza kwa kuishukuru Kokoliko disgner kwa kushirikiana na kampuni ya Sophia Production kwa kubuni na kutengeneza mavazi yaliyopelekea kuchangia warembo walioshiriki mashindano hayo kutoka hapa nchini kufanya vizuri.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kampuni ya Kokoliko Disgner, Aisha Kisoki “Mama Sophia”alisema kampuni hiyo itaendelea kuwabunia mavazi washiriki hapa nchini lengo likiwa ni kutangaza asili ya watanzania.

Mwisho.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »