Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

DKT.BITEKO AWAASA WATANZANIA KUPIGA KURA OCTOBA 29

October 05, 2025 Add Comment


📌 *Rais Samia kuzulu Bukombe wiki ijayo*


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ametoa wito kwa Watanzania waliojiandikisha kupiga kura kujitokeza kwa wingi Oktoba 29 mwaka huu, ili kuwachagua viongozi wao katika  nafasi ya Urais, Ubunge na Udiwani.


Dkt. Biteko amesema hayo leo Oktoba 5, 2025 alipopewa nafasi ya kusalimia wakati ibada ya jumapili katika Kanisa la AICT Ushirombo, Bukombe mkoani Geita.

“ Natoa wito kwa wote wakiojiandikisha kupiga kura, Oktoba 29 wajitokeze kwa wingi kwa sababu kura yako ni haki ya kikatiba na ina uhusiano wa moja kwa moja na maendeleo yako,” amesema Dkt. Biteko.


Amebainisha kuwa katika zoezi la upigaji kura kutakuwa na vituo vingi vya kupiga kura ili kurahisisha ushiriki wa wananchi.


Fauka ya hayo, Dkt. Biteko amewaeleza waumini wa Kanisa hilo la AICT kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan wiki ijayo atakuwa wilayani Bukombe hivyo amewaomba kujitokeza na kushiriki katika mapokezi yake.

“Naomba mpokee salamu nyingi za Mhe. Rais Samia ambaye Oktoba 12 atakuwepo katika Wilaya yetu ya Bukombe, nawaomba mjitokeze kwa wingi kwa ajili ya kumkaribisha kwa kuwa Mhe. Rais anatupenda sana.” Amemaliza Dkt. Biteko. 


Mwisho

WAZIRI MKUU AMWAKILISHA RAIS DKT.SAMIA UAPISHO RAIS WA MALAWI

October 05, 2025 Add Comment


⬛Rais Mutharika awahakikishia wananchi kuwa Serikali yake itawaletea maendeleo


⬛Awasisitiza viongozi kushirikiana na kuwatumikia Wamalawi


WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Oktoba 04, 2025 amemwakilisha Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye uapisho wa Rais Mteule wa Malawi, Peter Mutharika uliofanyika katika uwanja wa Kamuzu, Blantyre nchini humo.


Mheshimiwa Rais Mutharika wa Chama cha Democratic Progressive (DPP) alimshinda mpinzani wake Rais Mstaafu Lazarus Chakwera wa The Malawi Congress Party (MCP) kwa asilimia 56.8.


Mutharika aliwahi kuwa Rais wa nchi hiyo kati ya mwaka 2014 hadi 2020 alipoangushwa na Mheshimiwa Chakwera, hivyo Mheshimiwa Rais Mutharika anarudi tena katika kiti hicho cha Urais baada ya miaka mitano.

Akizungumza baada ya kuapishwa Mheshimiwa Rais Mutharika amesema nchi ya Malawi ni kwa ajili ya Wamalawi wote, hivyo amewataka viongozi wajitokeze na washirikiane katika kuwatumikia watu na si matumbo yao, watoto wao au marafiki zao.


“Sote tunahitaji mabadiliko na ninawaahidi mabadiliko na kama nchi hii tunataka kuibadilisha ni lazima yatoke kwetu sisi Wamalawi. Ameongeza kuwa Serikali yake itahakikisha wananchi wanahudumiwa katika nyanja zote za kimaendeleo na kwa pamoja tutaijenga Malawi.”

WAKURUGENZI WA RASILIMALIWATU KUHAKIKI RASIMU YA KANUNI ZA KUDUMU KATIKA UTUMISHI WA UMMA

October 02, 2025 Add Comment

Mwakilishi wa Katibu Mkuu ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, SACP. Ibrahim Mahumi akizungumza na Wakuu wa Idara za Utawala na Utumishi kutoka katika Wizara, Mamlaka za Serikali za Mitaa, Sekretarieti za Mikoa, na Taasisi wakati akifungua kikao kazi kilicholenga kuhakiki Rasimu ya Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma Toleo la Nne la Mwaka 2025 kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Sehemu ya Wakuu wa Idara za Utawala na Utumishi kutoka katika Wizara, Mamlaka za Serikali za Mitaa, Sekretarieti za Mikoa, na Taasisi wakiwa katika kikao kazi kilichoandaliwa na Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI kwa lengo la kuhakiki Rasimu ya Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma Toleo la Nne la Mwaka 2025 kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.



Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Bw. Cyrus Kapinga akifuatilia maoni mbalimbali yaliyokuwa yakiwasilishwa wakati wa kikao kazi kilicholenga kuhakiki Rasimu ya Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma Toleo la Nne la Mwaka 2025 kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Katikati ni Mwenyekiti wa kikao kazi hicho ambaye ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu, Wizara ya elimu, Sayansi na Teknolojia, Bw. Michael John.



Sehemu ya Wakuu wa Idara za Utawala na Utumishi kutoka katika Wizara, Mamlaka za Serikali za Mitaa, Sekretarieti za Mikoa, na Taasisi wakiwa katika kikao kazi kilichoandaliwa na Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI kwa lengo la kuhakiki Rasimu ya Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma Toleo la Nne la Mwaka 2025 kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.



Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu, Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Bi. Prisca Lwangili akiwasilisha maoni yake wakati wa kikao kazi cha kuhakiki Rasimu ya Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma Toleo la Nne la Mwaka 2025 kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.



Afisa Rasilimaliwatu Mwandamizi, Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Anne Yusuph akiwasilisha Rasimu ya Mapendekezo ya Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma Toleo la Nne la Mwaka 2025 wakati wa kikao kazi kilicholenga kuhakiki Rasimu hiyo kilichofanyika jijini Dodoma



Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia kikao kazi cha kuhakiki Rasimu ya Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma Toleo la Nne la Mwaka 2025 kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Sehemu ya Wakuu wa Idara za Utawala na Utumishi kutoka katika Wizara, Mamlaka za Serikali za Mitaa, Sekretarieti za Mikoa, na Taasisi wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa kikao kazi kilicholenga kuhakiki Rasimu ya Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma Toleo la Nne la Mwaka 2025 kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Mkurugenzi Msaidizi kutoka Idara ya Mishahara na Marupurupu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Gubas Vyagusa (aliyesimama) akiwasilisha maoni yake wakati wa kikao kazi kilicholenga kuhakiki Rasimu ya Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma Toleo la Nne la Mwaka 2025 kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Mhasibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Tumwimbilege Ilomo akifuatilia kikao kazi kilicholenga kuhakiki Rasimu ya Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma Toleo la Nne la Mwaka 2025 kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Wengine ni Wakuu wa Idara za Utawala na Utumishi kutoka katika Wizara, Mamlaka za Serikali za Mitaa, Sekretarieti za Mikoa, na Taasisi

Sehemu ya Wakurugenzi Wasaidizi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakifuatilia kikao kazi cha kuhakiki Rasimu ya Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma Toleo la Nne la Mwaka 2025 kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Wengine ni Wakuu wa Idara za Utawala na Utumishi kutoka katika Wizara, Mamlaka za Serikali za Mitaa, Sekretarieti za Mikoa, na Taasisi

Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, SACP. Ibrahim Mahumi (katikati mstari wa kwanza) akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Idara za Utawala na Utumishi kutoka katika Wizara, Mamlaka za Serikali za Mitaa, Sekretarieti za Mikoa, na Taasisi mara baada ya kufungua kikao kazi kilicholenga kuhakiki Rasimu ya Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma Toleo la Nne la Mwaka 2025 kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, SACP. Ibrahim Mahumi (katikati mstari wa kwanza) akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Idara za Utawala na Utumishi kutoka katika Wizara, Mamlaka za Serikali za Mitaa, Sekretarieti za Mikoa, na Taasisi mara baada ya kufungua kikao kazi kilicholenga kuhakiki Rasimu ya Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma Toleo la Nne la Mwaka 2025 kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Mkaguzi wa Ndani, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bi. Martha Wililo (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Msaidizi Anuai za Jamii na Mratibu wa VVU, Ukimwi na Magonjwa Yasiyoambukiza, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Mwanaamani Mtoo (kulia) wakifuatilia maoni kutoka kwa Wakuu wa Idara za Utawala na Utumishi kutoka katika Wizara, Mamlaka za Serikali za Mitaa, Sekretarieti za Mikoa, na Taasisi wakati wa kikao kazi kilicholenga kuhakiki Rasimu ya Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma Toleo la Nne la Mwaka 2025 kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.


Na. Veronica E. Mwafisi-Dodoma


Mwakilishi wa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, SACP. Ibrahim Mahumi amesema Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma (Standing Order) ni nyenzo muhimu katika Usimamizi wa Utawala na Rasilimaliwatu ndani ya taasisi za Umma.

SACP. Mahumi amesema hayo, wakati akifungua kikao kazi cha wadau kilicholenga kuhakiki Rasimu ya Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma Toleo la Nne la Mwaka 2025 kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

SACP. Mahumi amesema, kupitia Sera ya Menejimenti na Ajira, Sheria ya Utumishi wa Umma Sura 298 na Kanuni zake za 2022 pamoja na miongozo ya Kiutumishi inayotolewa na Serikali ni vitendea kazi muhimuvinavyotumika kusimamia Utumishi wa Umma ili kuwa na ufanisi.

Kupitia kikao kazi hicho SACP. Mahumi amewataka Wakuu wa Idara za Utawala na Utumishi kuona namna ya kutoa maoni na ushauri ili kuboresha zaidi Sera na Kanuni zinazotakiwa kufanyiwa mabadiliko.

Kadhalika, SACP. Mahumi amesema, mabadiliko ya Sera na Kanuni mbalimbali katika Utumishi wa Umma, pia zimeleta mabadiliko katika eneo la Upimaji wa Utendaji kazi ambao awali ulikuwa unajulikana kama (OPRAS) ambayo kwa sasa unajulikama kwa jina la PEPMIS, mabadiliko ya Sheria ya Utumishi wa Umma pamoja na Nyaraka mbalimbali ambazo zinatoa maelekezo tofauti na ya awali ambayo yalikuwa yakifanyiwa kazi.


Akihitimisha hotuba yake, SACP. Mahumi amesema, matokeo ya kikao kazi hicho yalenge katika kutoa mwelekeo chanya wa nyaraka sahihi kupitia Sera na Kanuni zitakazoboreshwa.
WATUMISHI IDARA YA KAZI NA AJIRA WAASWA KUONGEZA UFANISI

WATUMISHI IDARA YA KAZI NA AJIRA WAASWA KUONGEZA UFANISI

October 01, 2025 Add Comment

 

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu Bi. Mary Maganga amewataka  watumishi wa idara ya Kazi na Kitengo cha Ajira  kuongeza ubunifu wakati wa kutimiza majukumu yao ,wito alioutoa Morogoro leo Oktoba 01,2025 wakati alipofungua kikao kazi.

 Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu Bi. Mary Maganga amewataka  watumishi wa idara ya Kazi na Kitengo cha Ajira  kuongeza ubunifu wakati wa kutimiza majukumu yao ,wito alioutoa Morogoro leo Oktoba 01,2025 wakati alipofungua kikao kazi.

 

Sehemu ya watumishi wa Idara ya Kazi na Kitengo cha huduma za ajira wakiwa kwenye kikao kazi leo Oktoba 01,2025 mjini Morogoro.

Sehemu ya Wakuu wa Idara na Vitengo (waliokaa mbele) toka Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi ,Vijana, Ajira na wenye Ulemavu wakiwa kwenye kikao kazi cha kujadili masuala ya Kazi na Ajira mjini Morogoro leo Oktoba 01,2025.

Kamishna wa Kazi Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi ,Vijana, Ajira na wenye Ulemavu Bi.Suzan Mkangwa akieleza madhumuni ya kikao kazi cha kujadili masuala ya kazi na ajira kilichofanyika Morogoro leo Oktoba 01,2025 .
(Habari na Picha na OWM-KVAU)

Na OWM KVAU

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bi. Mary Maganga amewataka Watumishi wa Ofisi hiyo kuendelea kufanya kazi kwa ufanisi ili kuongeza tija katika utoaji huduma kwa wananchi.

Bi. Mary amebainisha hayo leo Oktoba Mosi, 2025 mkoani Morogoro wakati alipofungua Kikao Kazi cha watumishi wa Idara ya Kazi na Kitengo cha Huduma za Ajira kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Idara hizo.

“Ninataka mfanye kazi kwa ushirikiano, ubunifu na uwajibikaji ili kufanikisha utekelezaji wa majukumu ya Serikali katika usimamizi wa masuala ya kazi na huduma za ajira nchini” alisisitiza Katibu Mkuu huyo.

Awali, Kamishna wa Kazi Ofisi hiyo, Bi. Suzan Mkangwa, amesema kuwa kikao hicho kimehusisha watumishi kutoka Mikoa yote nchini, ambapo watajadili masuala mbalimbali yanayohusu kazi.

Naye Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Ajira Bi. Josephine Matiro amesema kikao hicho ni fursa muhimu ya kujadili changamoto na mafanikio yaliyopo pamoja na kubadilishana uzoefu wa kitaaluma ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Kikao hicho kimeandaliwa kwa lengo la kujadili kwa kina utekelezaji wa majukumu ya idara hizo pamoja na kujengeana uelewa wa pamoja kuhusu namna bora ya kuboresha utendaji kazi .

NSSC: Vyama vya Siasa Viepuke Kuwatumia Wanafunzi Katika Kampeni

October 01, 2025 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Umoja wa Kitaifa wa Asasi za Kiraia wa Shule Salama (NSSC) umetoa rai kwa vyama vya siasa na wagombea nchini kuepuka kuwatumia wanafunzi na watoto katika kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, ukisisitiza kuwa kitendo hicho ni ukiukwaji wa haki za watoto na kinyume cha sheria.