Showing posts with label Nishati. Show all posts
Showing posts with label Nishati. Show all posts

Rais Samia Suluhu Hassan Kinara wa Nishati Safi ya kupikia Duniani , aungwe Mkono - Sangweni

July 11, 2025 Add Comment

WhatsApp%20Image%202025-07-11%20at%2009.41.55


WhatsApp%20Image%202025-07-11%20at%2009.41.54%20(2)

WhatsApp%20Image%202025-07-11%20at%2009.41.54%20(1)

WhatsApp%20Image%202025-07-11%20at%2009.41.54

WhatsApp%20Image%202025-07-11%20at%2009.41.53



  • Apongeza kasi ya Dkt. Biteko na Uongozi Menejimenti ya Nishati katika kufanikisha Kampeni ya Nishati Safi ya Kupikia.
  • Amesifu juhudi za TANESCO  na REA katika kutekeleza  Kampeni ya Nishati Safi ya Kupikia.
  • Atoa Rai kwa Watanzania kuhamia kwenye Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia


Na Mwandishi Wetu,


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) Mh. Charles Sangweni ametoa Rai kwa Wananchi wote kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Dkt. Samia Suhuhu Hassan katika Kampeni ya Kitaifa  ya kuhamia kwenye Nishati Safi ya Kupikia.

Rai hiyo imetolewa tarehe 09 Julai, 2025  na Mhe. Charles Sangweni alipotembelea Banda la TANESCO  katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar-es-Salaam yanayoendelea jijini Dar-es-Salaam.

Amesema Tanzania tuna bahati kuwa, Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jemedari Mkuu wa Majeshi ya nchi yetu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa ndiye Kinara wa Kampeni ya Nishati Safi ya Kupikia Duniani.

Amesema, Wizara ya Nishati na Watanzania wote kiujumla, ni muhimu tuunge mkono juhudi zinazofanywa na Rais wetu katika kuhakikisha Watanzania wanahamia katika Nishati Safi ya Kupikia kwanza kwa  kuhakikisha tunapokea na tunaendana na Kauli Mbiu ya Nishati Safi ya Kupikia na kuunga mkono jitihada alizozianzisha.

Amesema, "kama Watendaji, tumefurahi kuona, wenzetu wa TANESCO wameunga Mkono juhudi za Mheshimiwa Rais kwa kuja na kampeni ya kuhamasisha  matumizi ya vyombo mbadala vya umeme vinavyotumia umeme kidogo na ambavyo vinahakikisha Nishati inayotumika kwa ngazi ya kawaida kabisa majumbani inakuwa ni  Nishati Safi." Ameeleza kwa hisia za kuvutiwa na hatua hiyo Mha. Sangweni.

Mha. Sangweni ameeleza zaidi kuwa, katika kutembelea Banda la TANESCO, ameona vitu vingi, ikianzia kwa REA  Usambazaji wa Umeme unavyofanyika kwa kasi na hii inaonyesha kuunga mkono Juhudi za Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Viongozi wengine wa Wizara akiwemo  Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko

Pia, Mha. Sangweni amesema vilevile katika Banda la TANESCO amekuta Wadau wanauza majiko ya umeme yanayotumia Nishati ya umeme kidogo sana ikilinganishwa na majiko mengine ya kawaida.

Mkurugenzi Mkuu wa PURA ameeleza  kufurahishwa kwake zaidi na  majiko hayo yanayotumia mfumo wa sumaku kupitisha moto  kuwa na mfumo wa ku-sence  pale ambapo sufuria haiko jikoni na namna yanavyopunguza kabisa upotevu wa umeme ambao hautumiki.

"Tumeona kwamba, usipoweka sufuria basi hakuna moto ambao unatoka na wakati mwingine ukiwa umejisahau, kunakuwa na timer ambayo inaweza ikazima jiko kulingana na jinsi ulivyo- set." Amesema Mha. Sangweni.

Amefafanua kuwa, hiyo yote ni katika kuhakikisha kwamba bili iliyokuwa inakuja kwa kiasi kikubwa ambayo ilikuwa inakuja kutokana na majiko ambayo hayana control kama hizo, inaenda kupungua kwa kiasi kikubwa sana.

"Hatua hiyo itatufanya sisi ambao vipato vyetu sio vikubwa kuona kuwa kutumia umeme sio anasa tena bali ni Matumizi Bora Kabisa ya Nishati ambayo iko safi na inayofaa kwa matumizi na ulinzi wa mazingira kama ambavyo Viongozi wetu wa nchi wamekuwa wakituhimiza na kusisitiza ili kama nchi tuingie kwenye Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia." Amesema Mha. Sangweni.