Showing posts with label Nishati. Show all posts
Showing posts with label Nishati. Show all posts

DKT. BITEKO AHIMIZA UTEKELEZAJI WA MAAZIMIO VIKAO VYA KIMKAKATI VYA WENYEVITI WA BODI NA WAKUU WA TAASISI

August 26, 2025 Add Comment


📌 *Awakumbusha kuhusu dhamana waliyobeba ya kubadili maisha ya watanzania kupitia mtaji wa shilingi Trilioni 86 waliopewa*


📌 *Afunga Kikao kazi cha Tatu cha Wenyeviti wa Bodi, Wakuu wa Taasisi*


📌 *Asema Rais, Dkt. Samia anatambua mchango wa Taasisi za umma; ana matarajio makubwa kutoka kwao*


📌 *Awakumbusha kutekeleza Maagizo yaliyotolewa na Makamu wa Rais*


📌 *Kikao kazi chafanyika kwa mafanikio; chahusisha washiriki zaidi ya 600*


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko  amewahimiza Wenyeviti na Wakuu wa  Taasisi za Umma nchini kusimamia utekelezaji wa maazimio ya kimkakati yanayofikiwa katika vikao kazi wanavyofanya kwa kutambua kuwa wamebeba dhamana ya kuboresha maisha ya Watanzania kupitia mtaji wa shilingi Trilioni 86 ambao Serikali imewekeza kwenye Taasisi na mashirika yake.

Dkt. Biteko ameyasema hayo tarehe 26 Agosti 2025 jijini Arusha wakati akifunga kikao kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma (CEOs FORUM 2025).



 “Watanzania wanawategemea ninyi 

kuwabadilishia maisha, kama tunazungumza kuhusu umaskini wa watu, Serikali inapaswa kuwa kiongozi wa kuwaondolea watu umaskini wao, hivyo hamna budi kutambua  kuwa mnalo deni la 

kuboresha hali zetu na maisha yetu.” Amesema Dkt. Biteko

Dkt. Biteko amewahakikishia Watendaji hao kuwa Serikali katika ngazi zote inatambua mchango wa taasisi 

na mashirika katika ukuaji wa uchumi na pia inatambua mchango wa vikao kazi vya watendaji hao ambavyo vimepelekea mashirika kuongeza mchango wake katika mfuko mkuu wa Taifa.

" Vikao kazi hivi mnavyofanya vimeonesha mchango wake katika uchumi, mfano katika kikao kazi cha mwaka 2024 mliazimia mashirika ya umma yaboreshe utendaji na  kuongeza uchangiaji katika mfuko mkuu wa Serikali na  matokeo yameonekana mfano Shirika la Maendeleo ya Petroli ( TPDC) liliongeza uchangiaji wake kwa asilimia 100, shirika hili liliongeza uchangiaji wake kutoka shilingi bilioni 5.5 kwa mwaka 2023/2024 hadi shilingi bilioni 11.1 mwaka 2024/2025." Amesema Dkt.Biteko

Ameongeza kuwa, uchagiaji wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) umeongezeka kwa  asilimia 363 katika mfuko mkuu wa Serikali ambapo NHC ilichangia shilingi bilioni 1.2 mwaka 2023/ 24 na mwaka 2024/2025 ilichangia shilingi bilioni 5.5.


Dkt. Biteko amewaeleza Wenyeviti wa Bodi na Wakuu wa Taasisi kuwa “Rais Samia pamoja na kuthamini mchango wenu kwa Serikali anatarajia mengi kutoka kwenu na Watanzania wana matarajio makubwa hasa wakati tukielekea kwenye  utekelezaji wa Dira 2050, endeleeni  kuongeza mchango wenu kwenye  ukuaji wa uchumi, mjitegemee na muwe mfano wa taasisi binafsi."



Katika.hatua nyingine, Dkt. Biteko ametaka viongozi hao kufanyia kazi agizo lililotolewa na Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango la  kudhibiti mianya ya uvujaji wa mapato.


Pia amempongeza Msajili wa Hazina kwa kuwa na maono ya kuratibu kikao kazi hicho ili kujadili masuala yatakayosukuma mbele utendaji wa taasisi.



Katika hafla hiyo, Dkt. Biteko hakuacha kukumbusha kuhusu ushiriki wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ambapo 

amesema uchaguzi huo uwe ni ajenda ya watu wote wakiwemo Wenyeviti  wa Bodi na Wakuu wa Taasisi hivyo waone kuwa wana wajibu wa kuwasisitiza watu kwenye taasisi zao kujitokeza kusikiliza wagombea na baadaye kupiga kura  kwa amani kwani kukiwa na amani mashirika hayo pia yatafanya vizuri zaidi.


 Naibu Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Mhe. Stanslaus Nyongo kwa upande wake, amemshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan   kwa dira na muongozo katika kuendeleza mashirika ya umma ili yaweze kuwa na tija nchini.


Amesema katika siku tatu za kikao kazi washiriki wamejifunza na kubadilishana uzoefu kupitia watoa mada wa ndani na nje ya nchi waliobobea.


Amesema Wizara ya Mipango na Uwekezaji itahakikisha maazimio ya  kikao kazi hicho yanatekelezwa ipasavyo, pia Wizara itasimamia mageuzi ya kuhakikisha mashirika  ya umma yanachangia ukuaji wa pato la taifa hadi kufikia Dola  za Marekani trilioni 1  ifikapo 2050 ambapo  kwa sasa pato la taifa ni dola za Marekani bilioni 85.


Kwa upande wake Salim Kali, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha amesema wilaya 6 za Mkoa wa Arusha zimefikiwa na umeme hadi ngazi ya vijiji, pia  miradi ya maji imefanyika pamoja na  miundombinu ya Barabara ambayo imewezesha maisha bora kwa watu wa aina zote wakiwemo watalii. 


Awali, Msajili wa Hazina,  Nehemia Mchechu alisema kuwa katika kikao kazi hicho kampuni zaidi 300 zimeshiriki huku washiriki wakiwa ni zaidi ya 650.


Alisema kikao kilikuwa na  majadiliano mbalimbali ya kina yanayolenga kusukuma mbele uchumi wa nchi na kusimamia uwekezaji wa Serikali  kwa taasisi za umma wa zaidi ya shilingi trilioni 86.


Mkutano huo wa Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma uliongozwa na kaulimbiu ya  "Ushirikiano Endelevu wa  Kibiashara katika Mazingira Shindani Kimataifa- Nafasi ya Mashirika ya Umma."

DKT.BITEKO ATAKA WATUMISHI WIZARA YA NISHATI NA TAASISI ZAKE KUWA MFANO WA MATUMIZI NISHATI SAFI YA KUPIKIA

August 22, 2025 Add Comment


📌 *Lengo ni kutekeleza Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia kwa vitendo*


*📌Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia yapaa kutoka asilimia 6 hadi 20.3*


📌 *Agawa majiko yanayotumia umeme kidogo kwa Watumishi wa Wizara ya Nishati na REA*


*📌 Apongeza REA  kuhamasisha Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia nchini*


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko, amewataka watumishi katika Wizara ya Nishati na Taasisi zilizochini ya wizara hiyo kuwa mfano katika matumizi ya  Nishati Safi ya kupikia ili kuitekeleza kwa vitendo ajenda iliyoasisiswa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan  inayolenga kuhamasisha matumizi ya nishati safi na salama kwa afya


Maelekezo hayo ameyatoa tarehe 22 Agosti 2025 jijini Dodoma  wakati akigawa majiko yanayotumia umeme kidogo kwa watumishi wa Wizara ya Nishati na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ambapo amewataka Watumishi hao  wawe mabalozi katika  kutekeleza ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia.


" Leo tunagawa majiko haya kwa kuwa  nyinyi ndiyo wenye dhamana kuu ya kutekeleza Ajenda ya Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia hivyo wajibu wenu ni mabalozi wazuri kwa watu wanaowazunguka ili nao wahamasike kutumia nishati hii safi." Amesema Dkt. Biteko


Amesema kufuatia mwamko mkubwa unaoendelea sasa kwa wananchi kufahamu faida za matumizi ya nishati safi ya kupikia, kiwango cha watumiaji kimepanda kutoka asilimia 6 na  kufikia asilimia  20.3 huku lengo likiwa ni kufikia asilimia 80 ifikapo 2034.


Dkt. Biteko ametanabaisha kuwa Idadi ya watu wanaoendelea kutumia nishati isiyo safi na salama ya kupikia  bado ni kubwa duniani,  barani Afrika na hapa Tanzania  hivyo ni jukumu la watumishi wote wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake  kuhakikisha watanzania wanapata elimu sahihi ili waweze kubadilika na kufikia lengo lililokusudiwa.



Akigawa  majiko 220 kwa watumishi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Dkt. Biteko  amepongeza Taasisi hiyo kwa kuendelea kuhamasisha matumizi ya  nishati safi ya kupikia hususan katika maeneo ya vijijini ambapo kumeonekana kuwa bado changamoto ya kufikiwa na Nishati Safi ya Kupikia.

Pia ameipongeza REA kwa kuhakikisha  Vijiji vyote 12,318 nchini vinafikiwa na umeme.



Kwa Upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Mhandisi Felchesmi Mramba amemhakikisha  Dkt. Biteko kuwa atakahikisha agizo alilolitoa linatekezwa na Taasisi zote anazozisimamia.



Amesema  atahakikisha kwamba  Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia yanafikia malengo yaliyokusudiwa.


Amewasisitiza watumishi kutumia Majiko hayo waliyopewa na si kuyahifadhi.

AGIZO LA DKT.BITEKO LA MINADA YOTE NCHINI KUTUMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA LAANZA KUTEKELEZWA

August 21, 2025 Add Comment

📌 Wachoma nyama na Mama Lishe katika mnada wa Msalato Dodoma waanza kuonja matunda ya Nishati Safi ya Kupikia


📌 Dkt. Biteko asema ni matunda ya Rais, Dkt. Samia ambaye anayefahamu machungu ya kutumia Nishati isiyo safi ya Kupikia


📌 Atoa maagizo kwa Mkurugenzi Jiji la Dodoma kuweka miundombinu itakayohakikisha majiko ya Nishati Safi ya Kupikia ya Wachoma nyama yanakuwa salama


📌 Apongeza REA, Wizara ya Nishati kutekeleza agizo alilolitoa: STAMICO yatakiwa kuweka kituo cha kudumu cha mkaa mbadala Mnada wa Msalato


📌 Kituo kikubwa cha kusambaza umeme na kusimamia gridi ya Taifa kujengwa Dodoma


Agizo la Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko alilolitoa kwa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kuhakikisha kuwa minada yote nchini inakuwa na miundombinu itakayowawezesha Wachoma nyama, Mama Lishe na Baba Lishe kutumia nishati Safi ya Kupikia limeanza kufanyiwa kazi ikiwa ni utekelezaji wa ajenda ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha wananchi wote wanatumia Nishati iliyosafi ya kupikia.


Safari hiyo ya kuhakikisha minada yote nchini inatumia nishati safi ya kupikia, imeanzia katika Mnada wa Msalato jijini Dodoma ambapo tarehe 21 Agosti 2025, Dkt. Biteko amegawa majiko banifu kwa Mamalishe takriban 27 wanaohudumu katika mnada huo pamoja na majiko ya kuchomea nyama.

“Kama mnavyofahamu, Mhe. Rais alitoa maelekezo kuwa watanzania asilimia 80 ifikapo 2034 watumie nishati safi ya kupikia, maelekezo yake yanaendelea kutekelezwa, tulianza na taasisi zinazolisha watu zaidi ya 100  kuondoa matumizi ya kuni na mkaa ikiwemo  magereza yote nchini, shule za Sekondari , vyuo na taasisi nyinginezo lakini moja ya maeneo yaliyobaki ni pamoja na minada ambayo inahudumia watu wengi.” Amesema Dkt.Biteko

Dkt. Biteko ameeleza kuwa kazi ya kufunga mifumo ya Nishati Safi ya Kupikia kwenye minada ilianza na utafiti ili kupata hali halisi ya matumizi ya nishati hiyo ambapo katika utafiti huo, asilimia 89.5 ya wachoma nyama wote walisema hawana uelewa wowote kuhusu nishati safi ya kupikia, pia utafiti huo umeonesha asilimia 26.3 ya wachoma nyama wamewahi kutumia nishati safi ya kupikia na asilimia iliyobaki haijawahi kutumia. Hii ikionesha kuwa bado kuna kazi ya kufanya kuelekea kwenye matumizi ya Nishati Safi ya kupikia.

Amesisitiza kuwa, hatua hizo zinazochukuliwa na Serikali katika  Nishati Safi ya Kupikia, ni matunda ya Mhe. Rais, Dkt.Samia Suluhu Hassan ambaye amejipambanua kama kama kiongozi mwanamke anayejua machungu ya matumizi ya nishati isiyo safi na wakati wote anaelekeza kuwa yeye anachotaka kuona  ni watu wengi hawatumii nishati isiyo safi ya kupikia. 

Ameongeza kuwa, Tanzania ndiyo nchi pekee barani Afrika ambayo imezindua Mkakati wa Taifa wa matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia ambao umekuwa ni mfano barani Afrika na nchi nyingine zinakuja kujifunza hivyo lazima iwe mfano na kinara  kwa kuishi yale inayoyasema.

Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko amemuagiza Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kuweka miundombinu ambayo itafanya majiko ya nishati safi ya kupikia katika minada  mkoani Dodoma kuwa katika sehemu ya kudumu na zoezi hilo lianze mara moja.


Aidha, ameliagiza Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kuweka kituo cha kudumu cha kuuza mkaa mbadala katika mnada wa Msalato ili wananchi wasikwame pale wanapohitaji nishati hiyo.


Vilevile ameitaka REA, kuhakikisha majiko makubwa ya kuchomea nyama ambayo yanatumia Nishati Safi ya Kupikia yanapatikana ili wananchi wanaochoma nyama na wanaofuata huduma wasipoate madhara ya afya kuanzia sasa kwenda mbele.

Dkt. Biteko ameipongeza REA na Watendaji wa Wizara ya Nishati  kwa kupoeka agizo lake kwa haraka na kulifanyia kazi, pia amewaasa kuendelea na ubunifu utakaowawezesha wananchi kutumia nishati safi ya kupikia na wasisahau kufanya tathmini ya matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia katika minada hiyo.

Pia, amewaasa Mama lishe na Baba lishe kuiunga mkono ajenda ta nishati safi ya kupikia na kuwa mabalozi wa nishati hiyo kwani watu wakiona faida zinazotokana na kutumia nishati safi ya kupikia  kutoka kwao nao watavutika kuitumia. 

katika hafla hiyo,  Dkt. Biteko amemshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kufanya kazi kubwa ya mfano katika sekta ya Nishati ambapo amesema Mkoa wa Dodoma  muda si mrefu utakuwa ni kitovu cha usambazaji umeme katika mikoa mbalimbali ikiwemo Singida, Shinyanga, Tabora, Kigoma na Arusha na  pia kitajengwa  kituo kikubwa cha kusambaza umeme na kusimamia gridi ya Taifa.


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule kwa upande wake amesema walaji katika mnada wa Msalato  kwa wiki ni kati ya 2000 na 3000 hivyo kwa kutumia Nishati Safi ya Kupikia itawezesha kuokoa mazingira kwa kuondokana na kuni na mkaa ambao ulikuwa ukitumika kuhudumia idadi hiyo ya watu. 

Aidha ameomba a kampeni hiyo ya Nishati Safi ya Kupikia ifike kwenye masoko mbalimbali ambayo ina mama lishe na baba lishe.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba yeye amemshukuru Dkt. Biteko kwa maono yake ambayo yamewezesha Mnada wa Msalato kufikiwa na Nishati Safi ya Kupikia ikiwa ni mwanzo wa kusogeza huduma kwenye minada mingine.

Ameeleza kuwa kiwango cha matumizi ya nishati safi ya kupikia kimepanda kutoka asilimia 6.9  ya mwaka 2022 na hadi kufikia asilimia 20.3 na kusema kuwa kwa jinsi matumizi ya nishatil safi ya kupikia yanavyoongezeka Serikali itatimiza lengo lake ya kufikisha Nishati Safi ya Kupikia kwa watanzania wapatao asilimia 80 kama alivyoagiza Mhe.Rais.

Naye, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema amesema katika mnada wa Msalato kuna wachoma nyama kati ya 45 na 50 ambao watapatiwa majiko makubwa ya kuchomea nyama, pia kuna mama lishe 27  ambao tayari wote wamepatiwa majiko banifu.

Mwenyekiti wa Wachoma nyama katika Mnada wa Msalato, Mathias Raphael  amesema baada ya kupata elimu ya nishati safi ya kupikia katika mnada huo  ameanza kutumia jiko linalotumia mkaa mbadala ambao amesema kuwa unatumika kidogo huku ukichoma nyama nyingi, unakaa muda mrefu na hauna moshi.


Mwisho

REA KUSAMBAZA MAJIKO BANIFU 10650 MKOANI PWANI

August 18, 2025 Add Comment


*📌RC Kunenge aipongeza REA kwa kuhamasisha matumizi nishati safi*


*📌Mifumo ya umeme jua kuchochea upatikanaji wa umeme

kwa asilimia 100 ifikapo mwaka 2030*


📍Pwani


Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imetoa jumla ya Majiko Banifu 10,650 Mkoani Pwani ikiwa ni mwendelezo wa jitihada za Serikali za kuhakikisha  kila mwananchi anatumia Nishati Safi ya kupikia nchini. 


Akizungumza leo tarehe 18 Agosti, 2025 ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Meneja wa Teknolojia za Nishati kutoka REA, Mha. Michael Kyessi amesema mradi huo unalenga kuuza na kusambaza Majiko Banifu kwa bei ya ruzuku ambapo mwananchi atachangia asilimia ishirini (20%) za gharama ya jiko huku asilimia themanini (80%) zikitolewa na Serikali. 

“Mwananchi wa kawaida atachangia 20% tu za gharama za jiko ambapo bei ya jiko ni 56,000 na mwananchi atagharamika kuchangia shilingi 11,200 tu baada ya ruzuku kutolewa na Serikali” amesema Mha. Kyessi. 



Sambamba na hilo Mha. Kyessi amebainisha thamani ya mradi huo kwa ujumla ni milioni 596,400,00 ambapo Serikali kupitia REA imetoa ruzuku ya shilingi milioni 477,120,00 ambayo ni sawa na asilimia themanini. 

Katika hatua nyingine, REA inatekeleza lengo la Serikali ya Tanzania kufikia mpango wa Umoja wa Mataifa wa "Nishati Endelevu kwa Wote" (SE4ALL) wa upatikanaji wa nishati 

kwa asilimia 100 ifikapo mwaka 2030. Mradi huu utatumia nishati Jadidifu ili kuweza kufikia wananchi wa maeneo ya visiwani na utekelezaji wake ni kwa kupitia mradi wa Ufadhili unaotegemea Matokeo (RBF) kupitia Benki ya Dunia. 

"Serikali ya Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa kufunga mifumo ya umeme jua maeneo ya visiwani kwa 

kutoa ruzuku kwa bei ya mwisho ya mtumiaji wa mfumo wa Umeme Jua ili kufanikisha upatikanaji wa umeme katika maeneo hayo yaliyo mbali na Gridi ya Taifa, " Amesema Mha. Kyessi. 

Mha. Kyessi amesema katika Mkoa wa Pwani mradi wa umeme jua unategemea kuhudumia visiwa 13 na jumla ya watoa huduma wawili (2) wanategemea kuhudumia visiwa hivyo kupeleka jumla ya mifumo 2,243 ndani ya kipindi cha miaka miwili (2) na gharama za mradi kwa mkoa wa Pwani ni shilingi  bilioni 1.372 ambapo ruzuku ni shilingi milioni 935.7 sawa na asilimia 69 ya gharama zote ya mradi na shilingi milioni 436.6 ni fedha toka kwa wanufaika. 

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge ameipongeza REA kwa mkakati wa kuendelea kuongeza matumizi ya Nishati safi na kuondoa kero kwa wananchi kuhusu matumizi ya kuni na mkaa ambayo ni hatarishi kwa afya zao. 

 

Mradi huo utatekelezwa kwa muda wa miezi 15 katika mkoa wa Pwani na jumla ya Majiko Banifu 10,650 yatasambazwa kwa wananchi.

WANANCHI WAKARIBISHWA NANENANE KUFAHAMU KWA KINA MPANGO MAHSUSI WA NISHATI 2025-2030

WANANCHI WAKARIBISHWA NANENANE KUFAHAMU KWA KINA MPANGO MAHSUSI WA NISHATI 2025-2030

August 05, 2025 Add Comment


*Ni uliosainiwa katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika wa Misheni 300*

Wizara ya Nishati imekaribisha wananchi kuendelea kutembelea Banda la Wizara ya Nishati katika Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima- NANENANE jijini Dodoma ili kufahamu masuala mbalimbali ikiwemo Mpango mahsusi wa Taifa wa Nishati wa mwaka 2025-2030.

Imeelezwa kuwa mpango huo uliosainiwa katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika wa Misheni 300 mwezi Januari 2025 unalenga kuunganisha umeme kwa wananchi milioni 8.3 ifikapo 2030 na kufikisha nishati safi ya kupikia kwa asilimia 75 ya Watanzania ifikapo 2030.

Mpango huo pia unalengai kiwemo kuongeza upatikanaji wa umeme na kuongeza ushiriki wa nishati jadidifu katika uzalishaji wa umeme.