Showing posts with label Nishati. Show all posts
Showing posts with label Nishati. Show all posts
DC MKUDE AKABIDHI VYOMBO VYA USAFIRI TANESCO MKOA WA ARUSHA KUIMARISHA UTOAJI HUDUMA

DC MKUDE AKABIDHI VYOMBO VYA USAFIRI TANESCO MKOA WA ARUSHA KUIMARISHA UTOAJI HUDUMA

April 14, 2026 Add Comment






*Ni katika muendelezo wa mkakati wa TANESCO wa kuwahudumia wananchi kwa ufanisi zaidi.

*Awataka kutumia vyombo hivyo kwa kazi husika za TANESCO.

Na Mwandishi Wetu, Arusha

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mkoani Arusha Mhe. Joseph Mkude amekabidhi vitendea kazi vya usafiri kwa TANESCO Mkoa wa Arusha ili kuimarisha utoaji wa huduma mbalimbali za Shirika kwa wananchi.

Akizungumza tarehe 13, Aprili 2026 wakati wa hafla ya kukakabidhi vitendea kazi hivyo iliyofanyika katika Ofisi za TANESCO Mkoa wa Arusha amesema hatua hiyo ya kukabidhi vitendea kazi hivyo ni hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma za umeme wa uhakika bila vikwazo vyoyote.

Amesema vitendea kazi hivyo vinakwenda kuongeza ufanisi katika utendaji kazi kwa watumishi wa TANESCO katika wilaya za Mkoa wa Arusha na kuwawezesha kutatua changamoto za wateja kwa wakati kwani Magari pamoja na Bajaji zitawawezesha kuyafikia maeno mengi zaidi ili kufikisha huduma ya umeme.

Amewataka Watumishi wa TANESCO Mkoa wa Arusha kuhakikisha wanatumia vyema vitendea kazi hivyo kwa malengo yaliyokusudiwa na Shirika na wala sio kwa matumizi yao binafisi ambayo hayana faida wala mchango wowote kwa Shirika hasa katika kutoa huduma kwa wananchi.

“Haya Magari tuliyopatiwa katika Mkoa wetu yanakwenda kugawiwa katika kila wilaya naomba yakatumike ipasavyo kwa malengo yaliyokusudiwa, tusitumie Magari haya kwa mambo yetu binafsi yasiyo na tija katika kutoa huduma kwa wananchi”.

Kwa upande wake Meneja wa Huduma za Usalama TANESCO Bw. Lenin Kiobya amesema Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan iliwezesha kununuliwa kwa Magari Makubwa na Madogo zaidi ya 500 kwa mwaka wa fedha 2025/2026 ili kurahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Bw. Kiobya amesema kati ya Magari hayo zaidi ya 500, Malori ya ukubwa mbalimbali ikiwemo tani 10 na tani 7 yapo 215 ambayo yanakwenda kuwa msaada Mkubwa zaidi katika huduma za matengenezo ya umeme kwa wakati hali itakayochangia kuongeza ufanisi wa kazi ndani ya Shirika.

Aidha, amesema kwa Mwaka wa Fedha ujao 2026/2027 Serikali imetenga zaidi ya bilioni 200 ili kununua vitendea kazi hivyo lengo likiwa ni kumaliza kabisa upungufu wa vitendea kazi vya usafiri kwa TANESCO katika maeneo yote nchini.

“Serikali iliwezesha TANESCO kuweza kunua Magari 556 kwa mwaka huu wa fedha 2025/2026 ili kurahisisha utoaji wa huduma ya umeme kwa wananchi, na kwa mwaka ujao wa fedha 2026/ 2027 Serikali imetenga zaidi ya bilioni 200 ili kununua vitendea kazi hivyo lengo likiwa ni kumaliza kabisa upungufu wa vitendea kazi vya usafiri kwa TANESCO”

Meneja wa TANESCO Mkoa wa Arusha Mhandisi Kisika Kisika amesema TANESCO katika Mkoa huo wamepokea vitendea kazi mbalimbali ikiwemo Magari makubwa 2, Gari aina ya Landcruser (4), Bajaji moja (1) vitakavyokwenda kuboresha zaidi huduma kwa wateja katika Mkoa huo.

“Tunaishukuru Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa kutupatia vitendea kazi hivi ambavyo kwa sasa tunakwenda kuvitumia kufikisha huduma kwa wananchi kwa haraka zaidi.

WATENGENEZA MAUDHUI MTANDAONI WATAKIWA KUWA NGUVU YA KUBADILISHA JAMII KATIKA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

April 08, 2026 Add Comment




📌 Kupitia uelimishaji na uhamasishaji wa jamii


Katika mwendelezo wa mafunzo kwa watengeneza maudhui mtandaoni (Content Creators), awamu ya kwanza inayoendelea Jijini Arusha leo Aprili 8, 2026, Wizara ya Nishati imewahimiza washiriki kutumia majukwaa yao ya kidijitali kama chachu ya kuleta mabadiliko chanya katika jamii.


Akitoa wito huo, Mhandisi Benezeth Kabunduguru kutoka Kitengo cha Nishati Safi ya Kupikia amesema watengeneza maudhui wana nafasi kubwa ya kuelimisha umma kuhusu umuhimu wa matumizi ya nishati safi ya kupikia, pamoja na kuhamasisha jamii wanayoizunguka na wafuasi wao kubadili mitazamo na kuanza kutumia nishati hizo.

Akiwasilisha mada yake, Mhandisi Kabunduguru ameeleza kuwa watengeneza maudhui wanaweza kutumia mbinu mbalimbali zenye mvuto kama vile picha za video fupi, vichekesho, hadithi na simulizi za maisha halisi ili kufikisha ujumbe kwa ufanisi na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Aidha, amesisitiza kuwa nishati safi ya kupikia si aina moja tu, bali ipo katika mfumo mbalimbali ikiwemo gesi, umeme, mkaa mbadala na nyinginezo, ambazo zimeidhinishwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kuwa salama kwa afya ya binadamu na rafiki kwa mazingira.

Katika hatua nyingine, alibainisha kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kinara wa ajenda ya nishati safi ya kupikia barani Afrika. Hivyo amewataka watengeneza maudhui kumuunga mkono kwa vitendo ili kufanikisha lengo la kitaifa la kufikia asilimia 80 ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.

Ameongeza kuwa watengeneza maudhui wanapaswa kutumia ushawishi wao kubadilisha mitazamo hasi ya jamii kwa kutumia lugha sahihi, ubunifu na maudhui yenye kugusa maisha ya watu.

Kwa mujibu wa takwimu, takribani vifo 33,000 hutokea kila mwaka kutokana na matumizi ya nishati isiyo safi ya kupikia. Hivyo, kuna umuhimu mkubwa wa kuifikisha elimu hii kwa wananchi wengi zaidi kupitia majukwaa ya kidijitali yanayotumiwa na watengeneza maudhui.

Mafunzo hayo yameandaliwa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na Mfuko wa Utamaduni na Sanaa Tanzania, huku Wizara ya Nishati ikiwa miongoni mwa wadhamini wakuu.



WAZIRI NDEJEMBI AFANYA KIKAO KAZI CHA PAMOJA NA TAASISI ZILIZO CHINI YA WIZARA YA NISHATI

April 07, 2026 Add Comment

 


Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi amekutana na kufanya kikao kazi cha pamoja na Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati zinazoshughulikia mafuta leo Aprili 07, 2026 jijini Dodoma.


Lengo la kikao hicho ni kupitia na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu hali ya upatikanaji na bei za bidhaa za mafuta nchini itakayowasilishwa mbele ya kamati hiyo Aprili 08, 2026.

Kikao hicho kinatokana na agizo la Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Zungu alilolitoa Aprili 01, 2026 kwa Waziri wa Nishati akielekeza kukutana na Kamati ya Nishati na Madini ili kujadili hali na mwenendo wa kupanda kwa bei ya mafuta nchini.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, Katibu Mkuu Wizara ya Nishati anayeshughulikia Mafuta na Gesi, Dkt. James Mataragio, Wataalamu kutoka wizarani pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara zinazoshughulikia mafuta na gesi.



MKURUGENZI MKUU REA AAGIZA UFANISI KUSAMBAZA UMEME VITONGOJI 9,009

March 31, 2026 Add Comment


Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi, Hassan Saidy amewataka Watumishi wa Wakala kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi ili kuhakikisha ndani ya muda uliopangwa wanafikisha umeme kwenye vitongoji vyote vya Tanzania Bara.
Ametoa maelekezo hayo Machi 30, 2026 Makao Makuu ya REA, Jijini Dodoma wakati wa kikao kazi na Watumishi wote, ambapo amesema baada ya kusaini Mradi mkubwa wa HEP II (B); Mradi wa kusambaza umeme kwenye vitongoji 9,009 tarehe 17 Januari, 2026 na kuongeza kuwa kazi iliyombele ya kila Mtumishi ni kuhakikisha vitongoji hivyo vinafikishiwa umeme katika kipindi cha miaka mitatu yaani hadi 2029.

Awali ilielezwa kuwa Mradi huo wa HEP II (B) ni muendelezo wa jitihada za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) za kuhakikisha upatikanaji wa huduma ya umeme kwa Wananchi wote wa Tanzania Bara.

Mhandisi Saidy amesema kukamilika kwa Mradi huo wa HEP II (B) pamoja na miradi mingine inayoendelea kutafanya jumla ya vitongoji ambavyo tayari vitakuwa vimefikishiwa umeme kuwa takriban 51,000 kufanya vitongoji vitakavyobakia bila umeme na bila kuwa katika mradi wowote kuwa taklibani 13,000 ambavyo vimepangwa kuanza kusambaziwa umeme ifikapo mwaka 2030 kama ilivyoelekezwa katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2025 – 2030.

Mradi huo unatarajiwa kutoa manufaa ya moja kwa moja kwa Wananchi kwa kuongeza upatikanaji wa huduma ya umeme vitongojini; kuboresha huduma za kijamii hususan katika sekta za afya, elimu na maji; kuwezesha matumizi ya umeme katika shughuli za uzalishaji na kuongeza kipato cha Wananchi pamoja na kuchochea ukuaji wa uchumi wa maeneo ya vitogojini pamoja na kuimarisha ustawi wa jamii.

Aidha; Mhandisi, Saidy aliongoza Watumishi wa REA katika zoezi la kuchagua Viongozi wa TUGHE tawini hapo ambapo kwa kauli moja Watumishi waliwachagua Viongozi wao katika ngazi tofauti kama ifuatavyo: – Mwenyekiti wa Tawi ni Bwana Swalehe Kiloza, Katibu wa Tawi ni Mhandisi, Annet Malingumu; Mjumbe wa Halmashauri ya Tawi ni Bwana Issa Sabuni na Mwakilishi wa Kundi la Vijana, Mhandisi, Issac Sanga.

Viongozi wengine ni pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Wanawake ya Tawi la TUGHE REA ni kama ifuatavyo: – Mwenyekiti ni Bi. Wilhelmina Cheyo; Katibu ni Bi. Ruth Emmanuel; Mweka Hazina ni Bi. Aveline Wilfred; Wajumbe Kamati ya Wanawake ni Bi. Happiness Ndunguru na Mhandisi, Bertha Mwaituka.

Vilevile Watumishi wa REA pia walichagua Viongozi kwa upande wa Klabu ya Michezo ya REA ambapo itaongozwa na Bwana Selemani Mtunzy kama Mwenyekiti na Mwenyekiti Msaidizi ni Bwana Samwel Sumwa; Katibu ni Bwana Praygod Ng’hunda; Mweka Hazina ni Bwana Daniel Kisaka wakati Wajumbe wa Kamati Tendaji kwa upande wa Wanaume atakuwa Mhandisi, Thomas Mmbaga na kwa upande wa Wanawake atakuwa Bi. Beatrice Shelukindo.

Wakati huo huo Watumishi wa REA walishiriki kwenye zoezi la kuchagua Viongozi wa Chama cha Kijamii cha Wafanyakazi (REA Social Club) chenye lengo la kusaidiana wakati wa raha na changamoto mbalimbali. Viongozi wa Chama hicho waliochaguliwa ni kama ifuatavyo: Mwenyekiti ni Bwana Elias Gunzer; Katibu ni Bi. Theresia Mang’ung’ula; Mweka Hazina ni Bwana Shukuru Malebeto; Wajumbe wa Kamati Tendaji ni Bwana Pastory Mwijage na Bi. Emmy Chali.





WAANDAAJI WA MAUDHUI KUWEZESHWA KUNUFAIKA KIUCHUMI KUPITIA UHAMASISHAJI WA NISHATI SAFI

March 25, 2026 Add Comment


Mkurugenzi wa Nishati Safi ya Kupikia kutoka Wizara ya Nishati, Bw. Nolasco Mlay, ameshiriki mafunzo maalum kwa waandaaji wa maudhui (content creators) yanayofanyika leo Machi 25,2026, mkoani Dar es Salaam yakilenga kuwajengea uwezo ili kuboresha ubunifu na kuongeza tija ya kazi zao.

Mafunzo hayo yameandaliwa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na Mfuko wa Utamaduni na Sanaa Tanzania, huku Wizara ya Nishati ikiwa miongoni mwa wawezeshaji wakuu.

Kupitia mafunzo hayo washiriki watapatowa elimu kuhusu fursa za kiuchumi zilizopo kwa waandaaji wa maudhui kupitia uhamasishaji wa matumizi ya nishati safi ya kupikia. 

Namna Waandaaji wa maudhui wataweza kujipatia kipato kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali zinazohusika na nishati safi, kushiriki kampeni za udhamini, matangazo ya bidhaa na huduma zinazohusiana na nishati safi pamoja na kutengeneza maudhui ya kielimu yanayovutia hadhira. 

Kupitia ubunifu wao, wanaweza kuvutia wadau na wafadhili, hivyo kuchangia katika maendeleo ya kiuchumi na uhifadhi wa mazingira.

Ushiriki wa Wizara ya Nishati katika mafunzo hayo unaonesha kutambua mchango mkubwa wa waandaaji wa maudhui kama daraja muhimu la kufikisha elimu kwa umma na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kupitia majukwaa yao ya kidijitali.