Showing posts with label Nishati. Show all posts
Showing posts with label Nishati. Show all posts

TPDC YAHIMIZA WANANCHI KULINDA MIUNDOMBINU YA BOMBA LA GESI ASILIA

May 25, 2026 Add Comment


Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kuwashirikisha  wananchi katika kulinda miundombinu ya bomba la gesi asilia, likieleza kuwa usalama wa miundombinu hiyo unategemea kwa kiasi kikubwa ushirikiano wa jamii nzima.

Katika kuimarisha ulinzi huo, TPDC inaendelea kutekeleza programu ya utoaji elimu kwa wananchi wanaoishi katika maeneo yanayopitiwa na bomba la gesi asilia mkoani Pwani, hususan katika wilaya za Rufiji, Kibiti na Mkuranga.

 Lengo la programu hiyo ni kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu umuhimu wa kulinda miundombinu hiyo pamoja na kuwajengea uwezo wa kutambua na kuripoti mapema vitendo au shughuli zinazoweza kuhatarisha usalama wake.


Akizungumza wakati wa utoaji wa elimu hiyo, Afisa Maendeleo ya Jamii wa TPDC, Bi. Ashura Hoja alisema “Bomba la gesi asilia ni rasilimali ya taifa hivyo  kila mwananchi ana wajibu wa kuwa mlinzi wa miundombinu hii na  kutoa taarifa mapema mnapoona shughuli zisizo za kawaida karibu na bomba la gesi,” alisema Bi. Hoja

Aidha, TPDC imewapongeza wananchi wa maeneo husika kwa mwitikio wao katika kushiriki kulinda miundombinu hiyo, huku ikiwataka kuendelea kuwa makini zaidi kwani uharibifu wowote unaweza kuathiri huduma muhimu pamoja na maendeleo ya taifa kwa ujumla.


Kwa upande wake, mwananchi wa Kijiji cha Jaribu Mpakani, Wilaya ya Kibiti, Bw. Kassimu Iddi alisema elimu inayotolewa na TPDC imeleta mabadiliko makubwa ya mtazamo kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kulinda bomba la gesi.

“Sasa tunaelewa kuwa kulinda bomba la gesi ni kulinda maisha yetu na maendeleo ya taifa letu. Tumeamua kuwa walinzi wa kwanza wa miundombinu hii,” alisema Kassimu

TPDC imeendelea kutoa wito kwa jamii zote zinazoishi karibu na bomba la gesi asilia kushiriki kikamilifu katika mfumo wa ulinzi wa pamoja, ili kuhakikisha miundombinu hiyo inalindwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

REA YAANDIKA HISTORIA LUDEWA

May 25, 2026 Add Comment








📌Yawasha umeme ukanda wa Nyasa kitongoji cha Nkanda

📌Yapongezwa kufikisha umeme kwenye mazingira magumu Njombe

📌Bodi ya REA yasisitiza wananchi kuchangamkia fursa uwepo wa nishati ya umeme




Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijni (REA), unaendelea kutekeleza miradi mbalimbali pamoja na kuwasimamia kwa karibu wakandarasi wote waliopewa na watakaopewa zabuni ya kutekeleza miradi ili kuhakikisha kuwa miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kwa ubora uliopangwa ili iweze kuwanufaisha wananchi.

Hayo yamebainishwa leo Mei 25, 2026 na Wajumbe wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), wakati wa hafla ya kukagua miradi, kutembelea na kuwasha umeme kitongoji cha Nkanda kilichopo wilaya ya Ludewa mkoani Njombe mradi uliokuwa unatekelezwa na Suma Jkt Electric Company Ltd.

Mha. Ahmed Chinemba amesema kuwa, mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji vya mwambao wilayani Ludewa unatekelezwa na mkandarasi M/S SUMAJKT ELECTRIC COMPANY LTD kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 3.2 ili wananchi wa mwambao wapate huduma ya umeme.

"Mradi huu umelenga kuongeza shughuli za kiuchumi kwa wananchi wa kitongoji cha nkanda ukiwa na chachu ya kutoa fursa za kibiashara kwa kuongeza thamani ya mazao ya uvuvi, kurahisiha upatikanaji wa huduma za kijamii na uwekezaji wa viwanda vidogo vidogo kama mashine za kusaga, mashine za kuchana mbao pamoja na mashine za kuchomelea," Amesema Mha. Chinemba.

Kwa upande wake, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Suma JKT Brigedia Jenerali Shija Lupi, ameishukuru REA kwa kuwapatia kazi hiyo ya kufikisha umeme katika maeneo ya mwambao kikiwemo kitongoji hicho cha Nkanda ambapo kazi imekamilika kwa ubora.

"Sisi Suma JKT tumefanisha kufikisha umeme kwenye mazingira magumu kama haya ambayo yalikuwa na changamoto nyingi lakini tumefanikiwa na sasa tunaona matunda yake, " Amesema Brigedia Jenerali Lupi.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu, Mha. Deogratius Nagu amesema katika kitongoji cha Nkanda takribani shilingi milioni 450 zimetolewa na Serikali kupitia REA ili kufikisha huduma ya umeme katika kitongoji hicho.

Aidha, amewataka wananchi wa Nkanda kuchangamkia fursa ya uwepo wa umeme kwa kuhakikisha wanafanya wiring katika nyumba zao na kuunganisha umeme kwa wingi ili wanufaike na umeme huo katika kitongoji chao.

Naye, Mwakilishi wa Mbunge wa Jimbo hilo Bw. Stanslaus Gowele amesema ujio wa umeme maeneo ya mwambao yanakwenda kuongeza chachu ya Maendeleo kiuchumi na kijamii kwa wananchi hao.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya wanufaika wa mradi huo wameeleza namna ambavyo Mradi huo umekuwa mkombozi kwao.


Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya wanufaika wa mradi huo wameeleza namna ambavyo Mradi huo umekuwa mkombozi kwao.




MRADI WA NJIA YA KUSAFIRISHA UMEME CHALINZE–DODOMA KUKAMILIKA AGOSTI 2026 : MD TWANGE

May 21, 2026 Add Comment



Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange, amesema mradi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovolti 400 kutoka Chalinze hadi Zuzu, Dodoma, unatarajiwa kukamilika ifikapo Agosti 18, 2026.

Akizungumza Mei 20, 2026 wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya mradi huo katika mikoa ya Morogoro na Dodoma, Bw. Twange amesema mradi huo ni muhimu kwa kuwa unasafirisha umeme unaozalishwa moja kwa moja kutoka katika Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere ambao unapita Chalinze hadi Dodoma.

Amesema utekelezaji wa mradi huo unaenda sambamba na upanuzi wa vituo vya kupokea na kupoza umeme vya Chalinze na Zuzu, Dodoma, ambapo kukamilika kwake kutaimarisha hali ya upatikanaji wa umeme kwa ajili ya shughuli za uwekezaji pamoja na kuongeza fursa mbalimbali za kiuchumi nchini.

Amesema Serikali Chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imetoa kiasi cha Shilingi Bil 514 kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi huo ambao utachochea shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii kuendana na kasi ya ongezeko la mahitaji.

“Leo tumefanya ukaguzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Chalinze hadi Dodoma. Njia hii ni muhimu kwa kuwa inaongeza uwezo wa kusafirisha umeme kutoka Bwawa la Mwalimu Julius Nyerere kwenda kwa watumiaji mbalimbali. Idadi ya watu imeongezeka na shughuli za kiuchumi zimeongezeka hivyo tumeingia makubaliano sasa mradi huu utakamilika Agosti 18, 2026,” alisisitiza Bw. Twange.

Ameeleza kuridhishwa na hatua iliyofikiwa huku akimtaka mkandarasi kuongeza kasi ya utekelezaji ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati.

“Tumekubaliana kuongeza wataalamu na vifaa vya kutosha ili kuhakikisha mradi huu unakamilika ndani ya muda ulioainishwa ,” ameongeza.

Kwa upande wake, Meneja wa Mradi, Mhandisi Newtone Lingstone, amesema mradi huo wenye urefu wa kilometa 345 Kutoka Chalinze hadi Dodoma unafadhiliwa kwa asilimia 100 na Serikali ya Tanzania, huku kazi za upanuzi wa vituo vya kupokea na kupoza umeme vya Chalinze na Dodoma zikiendelea vizuri.

Kukamilika kwa mradi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Chalinze hadi Dodoma wenye msongo wa Kilovoti 400 utaimarisha na hali ya upatikanaji wa umeme si kwa Mkoa wa Dodoma pekee, bali katika maeneo mbalimbali nchini.



MAAFISA UHUSIANO NA HUDUMA KWA WATEJA TANESCO WAPEWA MAFUNZO YA KITAALAMU JIJINI DODOMA

May 19, 2026 Add Comment

 

Maafisa wa Uhusiano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO wakiendelea kupewa mafunzo na makuzi ya kitaalamu kupitia mada mbalimbali zinazohusiana moja kwa moja na utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku, katika Mkutano Mkuu wa Mwaka unaoendelea kufanyika katika Hoteli ya Lavenda, jijini Dodoma.

Mkutano huo ulifunguliwa rasmi tarehe 18 Mei, 2026 na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, ambapo unalenga kuimarisha utoaji wa huduma bora kwa wateja pamoja na kuongeza ufanisi katika utendaji kazi wa maafisa hao.


#MkutanoMkuuWaMaafisaUhusianoNaHudumaKwaWateja2026#TupoKazini














TANESCO YAANZA UTEKELEZAJI WA MAELEKEZO YA WAZIRI NDEJEMBI, TRANSFOMA KUBWA YAWASILI NGARA

May 19, 2026 Add Comment




 ðŸ“Œ Siku 10’baada ya Mbunge Bahemu kuibua changamoto ya kukatika umeme Ngara.


Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeanza kutekeleza maelekezo ya Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, kwa kuanza kazi ya kufunga transfoma mpya yenye uwezo mkubwa katika Wilaya ya Ngara mkoani Kagera ili kuboresha upatikanaji wa umeme wa uhakika.

Hatua hiyo inakuja ikiwa zimepita siku tisa tangu Waziri Ndejembi alipolielekeza shirika hilo kuhakikisha ndani ya mwezi mmoja linapeleka transfoma kubwa kufuatia malalamiko ya kukatika kwa umeme yaliyowasilishwa na Mbunge wa Jimbo la Ngara, Mhe. Dotto Bahemu.

Leo Mei 19, 2026, transfoma hiyo kubwa imewasili katika kituo cha kupozea umeme cha Djululigwa wilayani Ngara huku wataalamu wa TANESCO wakianza kazi ya kuifunga.

Meneja wa TANESCO Wilaya ya Ngara, Eng. Amani Chidundo amethibitisha kuwasili kwa transfoma yenye uwezo wa 5MVA na kueleza kuwa kazi ya kuifunga inatarajiwa kuchukua takribani saa 12 kukamilika.


Eng. Chidundo amesema changamoto ya kukatika kwa umeme wilayani humo ilikuwa ikitokana na transfoma ya awali yenye uwezo wa 3MVA kuzidiwa uwezo kutokana na ongezeko la mahitaji ya umeme.

Akishuhudia kazi ya ufungaji wa transfoma hiyo, Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Ngara ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Nishati kwa kusikiliza na kufanyia kazi kwa haraka changamoto ya wananchi wa Ngara.

“Leo tunapokea transfoma kubwa inayoenda kuondoa changamoto ya WanaNgara. Tuombe wananchi mpokee na tutoe shukurani kwa Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhua Hassa, Waziri pamoja na Mbunge kwa kuletewa mtambo mkubwa wa transfoma kuhakikisha zile changamoto tulizokuwa tukizipata, zinakwenda kupungua” amesema Mkubila.