TUIBADILISHE HOFU YA WANANCHI KUWA UELEWA – WAZIRI MCHENGERWA

February 02, 2026

Na WAF, Dar es Salaam

Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa, amesema wahariri wa vyombo vya habari wana jukumu muhimu la kubadilisha hofu ya wananchi kuwa uelewa sahihi kuhusu Bima ya Afya kwa Wote, ili waweze kunufaika kikamilifu na huduma za afya.

Amesema hayo leo, Februari 2, 2026, wakati akizungumza katika kikao kazi na wahariri kilichofanyika Ukumbi wa Karimjee, Dar es Salaam.

“Hofu huzaa hasira, na hasira huzaa mgawanyiko. Sauti zenu ni dira, na kalamu zenu ni mwanga utakao waongoza wananchi kesho,” amesema Waziri Mchengerwa.

Ameongeza kuwa wahariri wanapaswa kutumia nafasi yao kuwaelimisha wananchi kwa usahihi kuhusu mfumo wa Bima ya Afya kwa Wote, ili kuondoa upotoshaji na kuongeza uelewa wa huduma zitakazotolewa.

Aidha Waziri Mchengerwa amesema kuwa Serikali imejipanga vyema ili kutekeleza mpango wa Bima ya Afya kwa wote husuasan ni eneo la makundi maalum pamoja na matibabu ya magonjwa sugu ili mwananchi aweze kufurahia huduma za afya nchini.

"Mhe. Rais atakapokwenda kuzindua Bima ya Afya kwa wote atazindua pia mpango wa matibabu ya wale wasiojiweza (wazee na makundi maalum) hasa kwenye matibabu ya magonjwa sugu, sisi kama wizara tumeshajipa na kujiandaa katika utekelezaji," amesema Waziri Mchengerwa


Share this

Related Posts

Previous
Next Post »