Mwenyekiti wa CCM na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt, Jakaya Mrisho Kikwete amezindua rasmi kampeni ya Ubunge na Udiwani ya CCM katika jimbo jipya la Kivule ambalo limemegwa kutoka jimbo la Ukonga wilayani Ilala jijini Dar es salaam siku ya Jumanne Septemba 9, 2025.
Huku akishangiliwa na nyomi ya watu Dkt Kikwete aliongea na wananchi na kisha kumtambulisha mgombea ubunge wa Kivue Bw. Ojambi Didas Msaburi na kumkabidhi ilani ya uchaguzi ya CCM.
Wanaogombea ubunge katika majimbo ya Ilala, Ukonga na Segerea, Naibu Spika Mhe. Mussa Hassan Zungu Mhe Jerry Silaa na Mhe Bona Kamoli pamoja na aliyekuwa mbunge wa Ukonga Mhe Mwita Waitara waliongea pia kabla ya mgombea mwenyeji kumwaga cheche
EmoticonEmoticon