DC ITUNDA AZINDUA OFISI YA WAENDESHA BAJAJI MBEYA

September 14, 2025


Na Mwandishi Wetu, Mbeya


MKUU wa Wilaya ya Mbeya, Solomon Itunda, amezindua rasmi Ofisi mpya ya Umoja wa Waendesha na Wamiliki wa Bajaji katika kanda ya Old Airport jijini Mbeya. 


Hafla hiyo ilihudhuriwa na mamia ya vijana, wajasiriamali, viongozi wa Serikali za mitaa na wadau wa sekta ya usafirishaji, ikiwa ni ishara ya kuimarisha mshikamano na kuchochea maendeleo ya vijana katika jiji hilo.

Katika hotuba yake, DC Itunda aliwataka vijana kutumia fursa zinazotolewa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan hususani mikopo ya asilimia 10 inayotolewa kwa makundi ya kinamama, vijana, na watu wenye ulemavu.


Ameeleza kuwa kwa mwaka wa Fedha 2024–2025, Halmashauri ya Jiji la Mbeya imefanikiwa kutoa mikopo ya zaidi ya shilingi bilioni 3.2, hatua inayodhihirisha dhamira ya serikali katika kuwawezesha wananchi kiuchumi.

Mkuu huyo wa Wilaya alimshukuru na kumpongeza Mhe. Rais kwa kuboresha mazingira ya kibiashara, hasa katika sekta ya usafirishaji.


Itunda amebainisha kuwa maboresho ya miundombinu, sera rafiki za kiuchumi, na uwezeshaji wa kifedha vimewapa nguvu vijana wajasiriamali ya kujiendeleza na kuchangia maendeleo ya Taifa. 


Uzinduzi huo umekuwa sehemu ya jukwaa la kujenga mshikamano, kuhamasisha uwajibikaji, na kuendeleza maadili ya kazi na utu akiwahimiza vijana kuendelea kushirikiana, kuwa na nidhamu ya kazi, na kutumia fursa zilizopo kwa manufaa ya muda mrefu. 



Ameisitiza kuwa maendeleo ya kweli hujengwa kwa juhudi za pamoja, mshikamano wa kijamii, na uongozi wenye maono.


Tukio hilo limeacha alama ya matumaini na mwelekeo mpya kwa sekta ya bajaji jijini Mbeya.

Mwisho

Share this

Related Posts

Latest
Previous
Next Post »