UMMY MWALIMU ASHINDA KURA ZA MAONI JIMBO LA TANGA MJINI

August 05, 2025



Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Tanga Mjini wamemchagua ndugu. Ummy Ali Mwalimu kuwa mgombea ubunge wa Jimbo hilo kwa kura 5,750 kati ya kura 10,293 zilizopigwa.


Akitangaza matokeo hayo August 04, 2025 Msimamizi wa uchaguzi amesema kuwa Jimbo la Tanga Mjini linajumla ya wajumbe 12,620 na waliopiga kura ni 10,293 ambapo kura zilizoharibika ni 117, kura halali zilizopigwa ni 10,176 sawa na Wastani wa asilimia 56.5


Ummy Ali Mwalimu amepata kura 5,750 ambayo ni sawa na 56.5%, Omary Ayoub akipata 4,146 sawa na 40%, Kassim Mbaraka 80 sawa na 1%, Rajabu Abasi 130 sawa na 1% huku Arif Fazel akipata kura 70 sawa na 0%.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »