MCC LAILAH NGOZI MGENI KONGAMANO LA NASIMAMA NA MAMA LITAKALOFANYIKA JIJINI TANGA

May 09, 2025
Na Mwandishi WETU,TANGA.

MJUMBE wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Lailah Burhan Ngozi anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Kongamano linalohusu Mchango wa Rais Samia Suluhu kwa mabinti na Wanawake wa Tanzania katika miaka minne ya uongozi wake litakalofanyika Mei 11 mwaka huu Jijini Tanga .

Kongamano hilo linatarajiwa kufanyika kwenye ukumbi swa Regail Naivera Jijini Tanga Mei 11 ambayo ni siku ya Mama Duniani ambalo litaanza saa tatu hadi saa kumi jioni

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwanamke na Uongozi ambao wameandaa Kongamano hilo Shamira Mshangama alisema lengo ni kuonesha mchango wa Rais Dkt Samia Suluhu kwa mabinti na wanawake wa Tanga na Tanzania kwa ujumla.

Alisema kwamba kongamano hilo limejikita katika kutambua jitihada zilizofanywa na Rais Dkt Samia Suluhu katika Sekta ya Afya,Elimu,Uchumi na Uongozi.

Shamira alisema kwamba Kongamano hilo linatarajiwa kuhudhuriwa na mabinti na wanawake takribani 400 kutoka mkoa wa Tanga na mikoa ya Jirani .

Share this

Related Posts

EmoticonEmoticon

:)
:(
=(
^_^
:D
=D
=)D
|o|
@@,
;)
:-bd
:-d
:p
:ng