Mwanasheria Baraka Chipamba wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), akizungumza na watu wenye ulemavu kutoka Jumuiya ya Wasioona Tanzania (TAB), Mkoa wa Dar es Salaam alipokuwa akitoa elimu kuhusu sheria ya watu wenye ulemavu Aprili 29, 2025.
.............................
Na Mwandishi
Wetu, Dar es Salaam
MWANASHERIA
Baraka Chipamba wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT) amesema ni kosa kisheria kujenga jengo ambalo
halina miundombinu ya kuwasaidia watu wenye ulemavu na faini yake ni Sh.
Milioni 20.
Chipamba
aliyasema hayo Aprili 29, 2025 wakati akizungumza na watu wenye ulemavu kutoka
Jumuiya ya Wasioona Tanzania (TAB), Mkoa wa Dar es Salaam alipokuwa akitoa elimu kuhusu sheria ya watu wenye
ulemavu mafunzo yaliyoratibiwa na LRCT na kufanyika ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa
ya Temeke jijini Dar es Salaam.
Alisema kosa hilo la kujenga jengo bila ya
kuwa na miundombinu ya watu wenye ulemavu likifanywa na Serikali faini yake ni
Sh. Milioni 2 na isizidi Milioni 20 na kama litafanywa na mtu binafsi ni faini
isiyopungua Sh. 500,000 hadi Sh.Milioni 7 au kifungo cha mwaka mmoja au vyote
kwa pamoja.
Alisema kwa mujibu wa sheria ya watu wenye ulemavu kama wananchi wengine wanayo haki ya kuheshimiwa, kutobaguliwa, kupata ajira, matunzo na stahiki zote wanazozipata watu wengine ikiwemo elimu.
“ Upo
umuhimu wa kuwepo vyama vya watu wenye ulemavu ili kuwakilisha na kujisemea
katika ngazi mbalimbali, kufanya utambuzi wa mahitaji yao pia kutathmini huduma
zinazotolewa na kuchochea maendeleo yao,” alisema Chipamba.
Alisema Serikali
ya Tanzania imeridhia au kuonesha nia ya kuwa sehemu ya juhudi za kimataifa ya
kuwainua na kuwalinda watu wenye ulemavu kwa kuwapatia fursa mbalimbali.
“Tunatambua
Tanzania imeridhia na kusaini Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Watu Wenye
Ulemavu (CRPD-2006 na Mkataba wa Nyongeza wa Haki za Watu Wenye Ulemavu 2009).
Lakini pia tunatambua kuwa kuna mambo mengi yamekwisha tekelezwa na Serikali,”
alisema Chipamba.
Mwanasheria
wa Tume hiyo, Vicky Mbunde ambaye alitoa elimu ya jinsi ya kuandika wosia na
kufungua shauri la mirathi alisema Watu wenye ulemavu wanayo haki na nafasi ya
kujiendeleza na kupata huduma katika jamii sawa na watu wasio na ulemavu.
Alisema ushiriki
wa watu wenye ulemavu katika maisha ya kila siku katika jamii hauna budi
kulenga katika kupunguza au kuondoa maisha ya utegemezi hivyo aliwahimiza
kufanya kazi kwa bidi kama vile ujasiriamali na shughuli zingine ili kujiletea
maendeleo yao badala ya kusubiri kusaidiwa.
Katika
mafunzo hayo mambo kadhaa yaliibuka ikiwa ni pamoja na jinsi wanavyoitwa ni ‘Watu
wenye Ulemavu au Walemavu’ ambao wanasheria wa Tume hiyo walieleza kuwa
wanatambulika kama ni Watu Wenye Ulemavu na siyo Walemavu.
Akichangia
mada kuhusu suala la kuandika wosia na mgawanyo wa mali zilizoachwa na marehemu
kwa wanufaika baada ya kufungua mirathi, Azamu Mohamed kutoka Yombo Dovya alisema
dini ya Kiislam haimtambui mtoto aliyezaliwa kwa mama mwingine nje ya ndoa
jambo ambalo linawafanya wanaume wengi kuwakataa watoto hao hivyo kushindwa
kupata mgao wa mali za baba zao pindi wanapofariki.
“Wanaume ule
ujasiri mliotumia wa kutoka kwa wake zenu na kwenda kuchepuka na kuwapata
watoto hao mnatakiwa kuuonesha kwa kuwatambulisha kwa wake zenu na ndugu ili
nao wajulikane na kupata mgao huo badala ya kuwakana,” alisema.
Mweka hazina
wa Jumuiya hiyo, Seif Jega, akizungumza baada ya kupata nafasi ya kushukuru kwa
niaba ya washiriki baada ya mafunzo hayo aliupongeza uongozi wa Tume hiyo kwa
kuandaa mafunzo hayo kwa watu wenye ulemavu na kuomba yawe endelevu ikiwa ni
pamoja na kuyafikisha vijijini wenzao na jamii waweze kuielewa jambo ambalo
litaweza kupunguza unyanyapaa kwa kundi hilo.
Kuhusu Tume hiyo, Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT) ni Idara ya Serikali
inayojitegemea chini ya Wizara ya Katiba na Sheria ambayo imeanzishwa kwa
mujibu wa Sheria ya Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania, Sura ya 171, na
ilianza kazi rasmi tarehe 21 Oktoba, 1983.
Kwa mujibu wa sheria, Tume ina jukumu la kufanya mapitio ya sheria zote za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili ziandane na mazingira ya wakati uliopo kwa maendeleo endelevu.
Mwanasheria Vicky Mbunde wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), akitoa elimu kuhusu namna ya kuandika Wosia pamoja na kufungua mirathi.Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo, Iddi Damka, akiongoza mafunzo hayo.
Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Judika Magezi akizungumza.
Washiriki wakiwa kwenye mafunzo hayo.
Mafunzo yakiendelea.
Maswali yakiulizwa kutoka kwa washiriki wa mafunzo hao.
Asha Kinyama akichangia jambo kwenye mafunzo hayo
Maswali yakiendelea kuulizwa.
Margareth Mhina, akizungumzia umuhimu wa faragha wakati wa kumuhudumia mtu mwenye ulemavu anapokwenda kupata matibabu hospitalini.
Maswali zaidi yakiulizwa.
Taswira ya mafunzo hayo.
Mafunzo yakiendelea.
EmoticonEmoticon