ZAIDI YA WANANCHI 9,450 KUNUFAIKA NA HUDUMA YA MAJI WILAYA YA KOROGWE

March 29, 2025



Na Oscar Assenga, TANGA


ZAIDI ya Wananchi 9,450 wa wilaya ya Korogwe Mkoani Tanga wanatarajiwa kuondokana na changamoto ya upatkanaji wa maji baada ya Serikali kuzindua mradi wa Kitaifa wa Ujenzi wa Visima 900 ambao unalenga kutatua changamoto hiyo.

Kati ya visima hiyo Mkoa wa Tanga watapata visima 53 ambavyo vitajengwa kila jimbo

Akizungumza mradi huo katika Kijiji cha Makorora wilaya Korogwe Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian alisema kwamba visima 8 vimejengwa na kati ya hivyo vitano vimejengwa katika Jimbo la Korogwe Vijiji na Vitatu Korogwe mjini.

Alisema kwamba hatua hiyo ni juhudi za Serikali za kuhakikisha wana watua ndoo kichwani wakina mama hapa nchini kwa kuwekwa huduma hiyo karibu na maeneo yao ili kuwaondolea adha ambazo walikuwa wanakumbana nazo awali.

“Leo hii tumekuja kushuhudia katika jimbo la Korogwe Visima vilivyochimbwa na hivyo yote ni kuhakikisha tunamtua Ndoo kichwani Mama kama ilivyo azma ya Rais wetu Dkt Samia Suluhu tumefanya hivyo kuonyesha maji yamefika kwa wananchi”Alisema

Awali akizungumza Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Tanga Mhandisi Upendo Lugongo alisema kwamba wataendelela kuboresha huduma za maji katika maeneo ya vijiji kwa kuendeleza miradi ya maji kila eneo ambalo halijaunganishwa na huduma hiyo

Alisema huduma hiyo iwafikie ndani ya muda mfupi ili waweze kuondokana na adha ya kufuata maji umbali mrefu na hivyo kuwawezesha kushiriki kwenye shughuli nyengine za maendeleo.

Lengo la Serikali ni kuwapatia maji wananchi kwa asilimia 85 vijiji na aslimia 95 maeneo ya mijini





Share this

Related Posts

Previous
Next Post »

EmoticonEmoticon

:)
:(
=(
^_^
:D
=D
=)D
|o|
@@,
;)
:-bd
:-d
:p
:ng