Kampuni ya sola ya SunKing imeendelea kusogeza karibu zaidi huduma kwa wananchi baada ya kufungua duka jipya katika eneo la stendi ya Kona ya Kayenze jirani na Kisesa, Wilaya ya Magu mkoani Mwanza.
Akizungumza Ijumaa Machi 28, 2028 wakati wa hafla ya ufunguzi wa duka hilo, Msimamizi wa Biashara wa kampuni hiyo, Juma Mohamed amesema hadi sasa jumla ya maduka 65 yamezinduliwa kote nchini na mkakati ni kuendelea kufungua maduka zaidi ili kuwafikia wananchi wengi zaidi.
"Kazi yetu ni kubuni, kutengeneza na kusambaza mitambo inayotumia nishati ya jua (sola) yenye uhakika wa mwanga ang'avu na salama kwa matumizi ya wananchi. Hili litakuwa duka la nne Mwanza ambapo tayari tumefungua Buhongwa, Buzuruga, Buswelu" alisema Mohamed.
Mohamed amebainisha kuwa kampuni hiyo ina mitambo ya gharama nafuu inayotolewa kwa mkopo kuanzia shilingi 350 kwa siku huku ikiwa na mitambo yenye uwezo wa kuwasha vifaa mbalimbali ikiwemo taa, TV na friji.
Ameongeza kuwa kampuni ya SunKing inaunga mkono jitihada za Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan zinazohamasisha nishati safi ili kuondokana na matumizi ya nishati chafu hatari kwa mazingira ikiwemo mkaa, kuni na mafuta ya taa.
Akizungumza kwa niba ya Mkuu wa Wilaya ya Magu, Afisa Tarafa ya Sanjo- Perpetua Chonja amewahimiza wananchi kuepuka matumizi ya nishati chafu ikiwemo vibatari kwani moshi wake ni hatari kwa macho na mapafu na badala watumie taa za SunKing kama nishati mbadala kwa hasa umeme unapokatika.
Chonja ameipongeza kampuni ya SunKing kwa kuunga mkono jitihada za Raid Dkt. Samia ambaye amekuwa akihamasisha nishati safi ikiwemo mitungi ya gesi ambapo kwa Tarafa ya Sanjo jumla ya majiko 800 yametolewa kwa wananchi.
Kwa upande wake balozi wa SunKing, mwanamuziki Mrisho Mpoto amesema bidhaa za SunKing ni bora kwani zinatoa nishati ya kutosha hata wakati wa mawingu huku pia ikitoa fursa kwa mtu yeyote kuwa wakala wa kuuza bidhaa hizo ambapo hadi sasa ina zaidi ya mawakala elfu tatu nchini.
Nao baadhi ya wananchi akiwemo Beatrice Michael na Kipara Luhiji wamesema bidhaa za SunKing ni mkombozi hasa kwa wajasiriamali wanaofanya shughuli zao nyakati za usiku ambapo hupata mwanga ang'avu ambao pia huwasaidia wanafunzi kujisomea wakiwa nyumbani.
Na George Binagi- GB Pazzo, Mwanza
Afisa Tarafa ya Sanjo wilayani Magu, Perpetua Chonja (wa tatu kulia) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa duka jipya la SunKing katika eneo la Stendi ya Kona ya Kayenye iliyopo Kijiji cha Isangijo Kata ya Bukandwe wilayani Magu. Wa tatu kushoto ni Msimamizi wa Biashara SunKing, Idd Mohamed. Wengine ni viongozi mbalimbali Kata ya Bukandwe.
Afisa Tarafa ya Sanjo wilayani Magu, Perpetua Chonja (wa tatu kulia) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa duka jipya la SunKing katika eneo la Stendi ya Kona ya Kayenye iliyopo Kijiji cha Isangijo Kata ya Bukandwe wilayani Magu. Wa tatu kushoto ni Msimamizi wa Biashara SunKing, Idd Mohamed. Kulia ni Balozi wa SunKing, Mrisho Mpoto.
Afisa Tarafa ya Sanjo wilayani Magu, Perpetua Chonja (wa pili kulia) akikata keki kuashiria uzinduzi wa duka jipya la SunKing katika eneo la Stendi ya Kona ya Kayenye Mwanza. Kulia ni Msimamizi wa Biashara SunKing, Idd Mohamed. Wengine ni viongozi wa Kata ya Bukandwe.
Afisa Tarafa ya Sanjo wilayani Magu, Perpetua Chonja (wa pili kulia) akimlisha keki Balozi wa SunKing, Mrisho Mpoto.
Afisa Tarafa ya Sanjo wilayani Magu, Perpetua Chonja (wa pili kulia) akimlisha keki mmoja wa wananchi.
Uzinduzi wa bidhaa za SunKing katika eneo la stendi ya Kona ya Kayenze Mwanza.
Wakazi wa Mwanza wakifuatilia uzinduzi wa duka jipya la SunKing katika eneo Kona ya Kayenye jirani na Kisesa.
Mmoja wa wakazi wa Mwanza akipatiwa huduma ya sola kutoka kampuni ya SunKing.
Mawakala wa SunKing wakiwa kwenye picha ya pamoja na mwanamuziki Mrisho Mpoto.
Burudani.
PIA>>> Bonyeza hapa kusoma zaidi
EmoticonEmoticon